Tetesi: Wabunge washauri Luhaga Mpina afukuzwe CCM

Shakari

Senior Member
Jul 6, 2022
157
440
Wabunge kadhaa wamedaiwa kupeleka malalamiko kwa Rais Samia kwamba Luhaga Mpina afukuzwe CCM kutokana na kile wanachodai kukiharibu Chama cha Mapinduzi mbele ya Watanzania.

Wabunge wanaotajwa kumchongea Mpina kwa Rais ni Wajumbe NEC wakiongozwa na Livingstone Lusinde, Joseph Kasheku Msukuma, Januari Makamba, Mwigulu Nchemba, Hussein Bashe, Makame Mbarawa.

Wabunge hao wanatajwa kuendesha kampeni za chini kwa chini na kumshauri Mama amfukuze Mpina CCM. Tusubiri tuone CCM ni dude kubwa.

View: https://youtu.be/CwuDTuTXLS8?si=gk59OFFIcZwntzZi
 
Wabunge kadhaa wamedaiwa kupeleka malalamiko kwa Rais Samia kwamba Luhaga Mpina afukuzwe CCM kutokana na kile wanachodai kukiharibu Chama cha Mapinduzi mbele ya watanzania...
Haya ni majungu tu,mpuuzeni huyu.
 
Hana cha kupinga ufisadi wala nini ni makasiriko tu baada ya kukosa uwaziri, hana lolote CCM wote ni mafisi tu.
Hayo ya uwaziri ni yake cha msingi anaongea ukweli.Wananchi tunachokitaka nikuona nchi inafwata misingi bora ya utawala sio mambo yakulindana wakati nchi iko ovyo kila sekta.

Tatizo ni kwamba watu hamtaki kuambiwa ukweli ndo maana ikijitokeza miongoni mwenu mtu kaamua kua mkweli mnamuona hafai kwasababu mmekaririshana lazima muwe chawa wakusifia tu badala ya kukosoa.
 
Hayo ya uwaziri ni yake cha msingi anaongea ukweli.Wananchi tunachokitaka nikuona nchi inafwata misingi bora ya utawala sio mambo yakulindana wakati nchi iko ovyo kila sekta.Tatizo ni kwamba watu hamtaki kuambiwa ukweli ndo maana ikijitokeza miongoni mwenu mtu kaamua kua mkweli mnamuona hafai kwasababu mmekaririshana lazima muwe chawa wakusifia tu badala ya kukosoa.
je Kingwangwala?
 
Wabunge kadhaa wamedaiwa kupeleka malalamiko kwa Rais Samia kwamba Luhaga Mpina afukuzwe CCM kutokana na kile wanachodai kukiharibu Chama cha Mapinduzi mbele ya watanzania...
Ningeshangaa kama usingemtaja January
 
Hayo ya uwaziri ni yake cha msingi anaongea ukweli.Wananchi tunachokitaka nikuona nchi inafwata misingi bora ya utawala sio mambo yakulindana wakati nchi iko ovyo kila sekta.Tatizo ni kwamba watu hamtaki kuambiwa ukweli ndo maana ikijitokeza miongoni mwenu mtu kaamua kua mkweli mnamuona hafai kwasababu mmekaririshana lazima muwe chawa wakusifia tu badala ya kukosoa.
Hicho unachokitaka hakipo ndani ya CCM kilichopo ni kwamba wanapingana kimakundi tu ikiingia awamu fulani wanakuwa na kikundi chao wanapiga na kujifanya wao ndiyo wema na kuwananga wengine nao wakitoka kikiingia kikundi kingine nao ndiyo wanajifanya wazalendo wa kweli yaani ni hivyo lakini ukweli ndani ya CCM wote ni mashetani.
 
Wabunge kadhaa wamedaiwa kupeleka malalamiko kwa Rais Samia kwamba Luhaga Mpina afukuzwe CCM kutokana na kile wanachodai kukiharibu Chama cha Mapinduzi mbele ya watanzania.

Wabunge wanaotajwa kumchongea Mpina kwa Rais ni Wajumbe NEC wakiongozwa na Livingstone Lusinde, Joseph Kasheku Msukuma, Januari Makamba, Mwigulu Nchemba, Hussein Bashe, Makame Mbarawa.

Wabunge hao wanatajwa kuendesha kampeni za chini kwa chini na kumshauri Mama amfukuze Mpina CCM. Tusubiri tuone CCM ni dude kubwa.
Sasa wanataka wapate kujisahihisha kwa kupitia nani?Kama mwenzao ambaye anawajua vema anawapa ukweli halafu wanajichukiza,nani atawasahihisha?Ni vema wamuombe@MdudeNyagali awashauri kikamanda.
 
Back
Top Bottom