Mhadzabe
JF-Expert Member
- May 20, 2009
- 3,246
- 4,755
Mkuu Mr Millerhii dhana ya kutegemea kutekelezewa na serikali nayo naiona imepitwa na wakati,
mimi nilikua nawaza kwamba hawa wabunge wanaochaguliwa kwenda kuwakilisha wananchi sio tu wakawakilishe bungeni...hapana,
mbunge akishakua ktk ile position anakua na exposure kubwa na conection nyingi...kwanini asirudi jimboni kwake akae na watu wake waone changamoto zao na wajadili jinsi ya kuzikabili,
lets say...jimboni kwangu kuna vijiji vinatenganishwa na mto hivyo kukosa mawasiliano ya uchukuzi na mambo mengine....mimi kama mbunge naongea na wananchi tunakubaliana kama hatuna ela ya kujenga daraja basi tutafute mwekezaji (mwisani) atujengee daraja alafu ndani ya muda fulani tuwe tunalipia na huo muda ukiisha daraja liwe letu,
naamini wabunge uwezo wa kutafuta wawekezaji wanao sio lazima mpaka serikali ije ilete suruhisho.....hiyo ndio maana ya kiongozi, kiongozi lazima uwe na VISION bwana.
Haya ni mawazo mazuri sana. Ila kiuhalisia hatuwezi kusema dhana ya kuitegemea serikali mathali katika kuhakikisha miundombinu bora imepitwa na wakati na kwamba iwe ni jukumu la wananchi wa eneo husika na mwakilishi wao.
Kama tukienda na dhana hii, ile dhana ya kukusanya kodi, kulipa ushuru ili ituletee maendeleo tutaifuta?
Kwamba sasa hatuna haja ya kulipa kodi kwa sababu kodi ndio hutuletea miundombinu, madawa kati hospitali zetu na pia kulipa watumishi?
Kama tukienda na dhana hii, si ajabu baada ya kujenga madaraja yetu kwa mfano, tutenda mbele zaidi kuwalipisha wapitaji ambao si wamaeneo yetu!....hii italeta utengano na hata uasi!
Lakini pia lazima tutambue hata kama Mbunge atakuwa na connections za namna gani akipata wafadhili lazima wapitie serikalini!...la mradi huo hautaruhusiwa.
Mifano ipo mingi. Kule kwa Lema na Gambo jambo kama hili liliwahi ripotiwa!
Hii inadhihirisha kwamba kila jambo lifanyikalo lazima kuwepo na ushawishi au mkono wa serikali. Ku undermine kuitegemea serikali ni jambolisilokubalika kabisa!
Hata swala la kujikusanyia hela mumlipe huyo muhisani lazima mkono wa serikali na vibali vitolewe.
Nachoweza kusema ni kwamba, mahali pekee ambapo serikali inaweza kubanwa kupeleka maendeleo kwa wananchi ni kupitia BUNGE lenye meno makali ya kuisimamia serikali, kutunga, kufuta au kuboresha sheria na sera lakini pia khiwajibisha serikali pae ambapo imeshindwa kutimiza wajibu wake.
Je tuna BUNGE le ye uthubutu wa kuyatenda haya?