Wabunge walazimishwe kutembelea majimbo yao..

Wabunge walazimishwe kutembelea majimbo yao..

Rebeca 83 bwana huyu kakujibu sawia kabisa.

Msome taratibu utamuelewa!

nimemuelewa ila hii top down process haitufai kwa sasa,tunahitaji bottom up process kutoka kwa mwananchi to Magufuli,lol..nimeona mahali umesema kazi za wabunge ni seasonal..kwani hio mara 12 nao si muda tu ,kwani wanashindwa nini kufanya mengine?primarily wamewekwa kutumikia wananchi sio just kuhudhuria vikao vya bunge lol
 
hii itakua nzuri sana, pia wakitembelea huko wawe na majibu ya kwanini huduma muhimu za kijamii hazipo na wakati wao wapo!

nilipata kwenda kijiji kimoja huko kusini, aisee kwanza barabara tu ukiacha ile main road ya rami huko ndani ni udongo na vumbi tu..

hospitali ipo moja tu tena ya mission, nikaulizia kuhusu viongozi wa kule nikaambiwa huyo mbunge wao ni mzawa wa kule kabisa na amekulia kule lkn tangu achaguliwe kumpata ni shida japo amejenga nyumba kule ya kuwazuga wananchi,

safari moja nakumbuka nilichelewa kutoka kule...saa mbili usiku ndio nikaanza kutoka alafu plus na mvua, kuja kuipata barabara kubwa ni saa saba usiku...

hakufai kupeleka gari kipindi cha mvua kule....ukienda jua linawaka mvua ikakukuta kule hautaweza kurudi, pikipiki wengine tunaziogopa.

wabunge waache kutanua tu mjini warudi makwao huko.
Wasiwasi wangu ni kwamba wanaweza kutembelea majimbo yao lakini bado wakashindwa kutatua shida zilizopo majimboni. Japo, ni vyema kutembelea majimbo yao na kuona shida tulizonazo wapiga kura wao
 
Juzi juzi nimemsikia mbunge wa Tarime vijijini nafikiri, anaishi GOBA Dar es salaam. Hii ndio sampobya wabunge karibu wote.
Ndio anaishi goba lakini kulibgana na video iliyokuwa ikionyesha maisha yake ya kifamilia alisema huwa anakuwa dar es salaam wakati wa likizo au kama kafika dar es salaam kikazi, nilimsikia akisema mara nyingine anaweza kuwa kuwa dar es salaam na nyumbani kwake huko goba asifike, nadhani tusimtolee mfano, tutafute wengine kweli wanaojiita wabunge wa sehemu flani na huku hata mitaa ya maeneo yao wanayojitambia kuwa wabunge hawayajuiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sana tu, mbunge wa jimboni kwetu yupo madarakani tangu enzi za mwalimu japo hana alolifanya jimboni zaidi ya kuja kipindi cha uchaguzi kutushukuru kwa kumchagua na kutuomba tumchague tena![emoji53]

mkuu ikianzishwa hii system itwa flush wote wabunge wabovu,ukiona unakutana na mbunge kijijini kwenu,mnamuambia shida hii hafanyi,mnamwambia ile hafanyi wala hana sababu eventually mtamchoka tu..na hamtamchagua tena..
 
nimemuelewa ila hii top down process haitufai kwa sasa,tunahitaji bottom up process kutoka kwa mwananchi to Magufuli,lol..nimeona mahali umesema kazi za wabunge ni seasonal..kwani hio mara 12 nao si muda tu ,kwani wanashindwa nini kufanya mengine?primarily wamewekwa kutumikia wananchi sio just kuhudhuria vikao vya bunge lol
Kuhudhuria vikao vya Bunge ndio a sole role of a parliamentarian!.... hayo ya kukaa na wananchi ni minors chini ya role hii kuu!

Kwanza si kweli kwamba tuna Top-down process katika mfumo wetu.

Hii top down hutumika pale tu maamuzi yakishafanywa na High level street bureaucrats, na kushushwa kwa ajili ya utekelezaji. Hujenga strong chain of commands kuhakikisha kilichiamuliwa KINATEKELEZEKA!

Ila katika mchakato wowote wa ku innitiate jambo, serikali imekuwa ikitumia Bottom up approach!...kuanzia katika utungwaji wa sera, sheria na maswala kama hayo.

Na si jambo jema, kubadirisha mfumo rasmi kwa sababu ya kuenenda kwa kadri ya matakwa ya kiongozi wa nchi ili tu kukidhi hitajio lake pasipo kufanya UTAFITI makini kama kweli mfumo uliopo hauwezi kuleta tija kwa mtawala tuliyenae!
 
Kutembelea hakuna TIJA kama yale unayoyachukua kutoka kwa wananchi wako HAYATIMILIZWI na kuhemiwa na Watekelezaji.

Kutembelea ni kupea matumaini MFU tu, kwamba tunaye mwakilishi ingawa kiuhalisia HALETI lolote tunalolitaka tulilomwagiza akatusemee!

Leo nafasi hizo zimewekwa mikononi mwa Mhimili uliojichimbia zaidi yani kwa Wakuu wa Wilaya, Mikoana Mawaziri!
hii dhana ya kutegemea kutekelezewa na serikali nayo naiona imepitwa na wakati,

mimi nilikua nawaza kwamba hawa wabunge wanaochaguliwa kwenda kuwakilisha wananchi sio tu wakawakilishe bungeni...hapana,

mbunge akishakua ktk ile position anakua na exposure kubwa na conection nyingi...kwanini asirudi jimboni kwake akae na watu wake waone changamoto zao na wajadili jinsi ya kuzikabili,

lets say...jimboni kwangu kuna vijiji vinatenganishwa na mto hivyo kukosa mawasiliano ya uchukuzi na mambo mengine....mimi kama mbunge naongea na wananchi tunakubaliana kama hatuna ela ya kujenga daraja basi tutafute mwekezaji (mwisani) atujengee daraja alafu ndani ya muda fulani tuwe tunalipia na huo muda ukiisha daraja liwe letu,

naamini wabunge uwezo wa kutafuta wawekezaji wanao sio lazima mpaka serikali ije ilete suruhisho.....hiyo ndio maana ya kiongozi, kiongozi lazima uwe na VISION bwana.
 
Wasiwasi wangu ni kwamba wanaweza kutembelea majimbo yao lakini bado wakashindwa kutatua shida zilizopo majimboni. Japo, ni vyema kutembelea majimbo yao na kuona shida tulizonazo wapiga kura wao
wakishindwa waje na sababu za kwanini wameshindwa na watuonyeshe kwamba walijaribu wakashindwa ili tujue tunamchagua nani kwenye uchaguzi ujao.
 
Sana tu, mbunge wa jimboni kwetu yupo madarakani tangu enzi za mwalimu japo hana alolifanya jimboni zaidi ya kuja kipindi cha uchaguzi kutushukuru kwa kumchagua na kutuomba tumchague tena![emoji53]
nyie ndio wa kulaumiwa sasa
 
mkuu ikianzishwa hii system itwa flush wote wabunge wabovu,ukiona unakutana na mbunge kijijini kwenu,mnamuambia shida hii hafanyi,mnamwambia ile hafanyi wala hana sababu eventually mtamchoka tu..na hamtamchagua tena..
exactly
 
wakishindwa waje na sababu za kwanini wameshindwa na watuonyeshe kwamba walijaribu wakashindwa ili tujue tunamchagua nani kwenye uchaguzi ujao.
Tatizo ni hao wakuhoji wenyewe wapo? Au wanasubiria tu wakati wa uchahuzi wspewe kofia na t-shirt na kuongezea sh.200/= za chumvi
 
Tutalaumiwaje wakati uwezo wetu wa kufikiri umeisha hapo![emoji53]
kwanini uwezo wenu uishie hapo...halafu hilo kundi ndio kubwa hasa ktk jamii na ndio linalochelewesha maendeleo.
 
Back
Top Bottom