Wabunge wagoma kusalimiana

Wabunge wagoma kusalimiana

Hivi huyu naibu spika anashindwa kutumia busara ya kawaida tu kuwaita ukawa na kuzungumza nao ili kufikia mwafaka?Maana vita hii haina mshindi kama kila mmoja akijifanya kuziba masikio.
 
Kitila Mkumbo amewashauri wanasiasa wa upinzani wabadilishe style ya upinzani kipindi hiki ch Magufuli.. Magufuli ni nyakati nyingine compare to JK
Mwache awe kama alivyo na tutaendelea kupoteza diplomasia ya kimataifa maana nchi za wenzetu wanafatilia hali ya nchi ilivyo.Ukikosa ushirikiano mzuri na mataifa mengine hata uchumi utayumba kwa kiwango fulani.
 
tumepoteza muda wa kupiga kura leo hawaongei wanagindwa kuwa pamoja heri demokrasia iishe tu
 
upuuzi mtupu, hao ndo wawakilishi wa wananchi wanakua na mambo ya ajabu ajabu kama hayo
 
Kitila Mkumbo amewashauri wanasiasa wa upinzani wabadilishe style ya upinzani kipindi hiki ch Magufuli.. Magufuli ni nyakati nyingine compare to JK
Wabadili vipi wakati hata mikutano hawaruhusiwi..!!!!aruhusu kwanza demokrasia nchini
 
Tatizo ni pale tunapodhani tuna guarantee ya amani na mungu na kusahau kuwa hata nchi zenye machafuko leo zilikiwa na amani kama sisi ila kilichowafikisha kwenye machafuko ni kuzembea mambo madogo madogo kama haya.... Kwa ambao wamesoma human behaviour particulary kwenye macro level.. Siasa zina mchango mkubwa ktk kushape tabia za watu... Tusidhan na kujidanganya kilichofanywa na wabunge wa upinzani hakitaathir tabia za wananchi.. Tutegemee wananchi kuanza kususiana shughuli zao za kila siku kitu ambacho hakijawahi kuwa tabia ya watanzania...

Rai yangu naomba madai ya ipinzani yasikilizwe
 
Nadhani ni muda muafaka kurekebisha kanuni za bunge ili kuondoa huu ujinga unajitokeza. Mbunge yeyote atakaekosekana bungeni kwa shughuli zisizokuwa za kibunge kwa siku 3 anakosa sifa ya kuwa mbunge.
 
Kwa akili yako juzi walifanya mbwembwe kwa kujiziba midomo? Kaa chini ujiulize kwa haya ambayo upinzani umewahi kuyaibua na yakazua mijadala ndani na nje ya nchi, kufanyiwa kazi na mengine kupuuzwa je kusingekuwa na Upinzani Nchi hii ingekuwa wapi? Huyo Kangi Lugola alimuona tu huyo Mbuge wa kike au alikuwa na malengo mengine?
 
Upuuzi mtupu. Hatuombi itokee ila Ikitokea sasa hivi Naibu spika akafariki au mbunge wa CCM watasusia kwenda kwenye msiba? sijui jamii itawaelewaje?
 
Safi sana UKAWA. Kila njia iliyopo itumike. Tupo pamoja na UKAWA daima. Ccm wangekuwa na busara hali ilipofika inatosha kukaa chini na kutafuta maridhiano. Ubabe dhidi ya UKAWA hauna faida yoyote kwao ccm! Upinzani wameanza siku nyingi kutoka bungeni lakini kila uchaguzi idadi ya wabunge wa upinzani inaongezeka. Wananchi wapo pamoja nao. Kuna watu wanataka mpaka waone UKAWA wameshika bunduki ndipo wajue kuwa UKAWA wako siriasi.
 
Jamani, hili jambo siyo la kufurahia kwa mtu yeyote yule mwenye hekima.
Sasa, leo humsalimii kwa mfano, Waziri wa Nishati na Madini, na inatokea kuwa jimboni kwako panahitaji umeme, Waziri anakuja pale jimboni kwako kuleta ufumbuzi JIULIZE HAYA MASWALI KISHA UTAONA KINACHOFANYIKA KUWA NI SIASA ZA WATU WA ELIMU YA CHEKECHEA.
je, utaziba mdomo?
Je hutamsalimu?
je hutamkaribisha wakati wa kuhutubia wananchi?
Je, utasema yeye ni chama tofauti na chama chako hivyo hupaswi kumsikiliza?
Je, utasema hutahudhuria kwa sababu ni chama tofauti na chako 'ukawa'

Mi naona vyama vyote vya siasa [tawala na upizani kwa ujumla wake] viache hayo maigizo ya wanafunzi wa chekechea.

Na pia, hapa tunajenga fukira finyu sana hata kwa wananchi kuelewa kuwa mtu akiwa chama tofauti na wewe huyu anakuwa ni adui.
Mi nilikuwa Tarime, miaka fulani hivi nikaona siasa kama hizo hadi katika ngazi ya familia, nilishangaa sana, nikasema kama ndiyo hivi tuendako pana giza sana mbele, ashukuliwe Mungu watu wakaona wanapotea ikabidi wabadilike kabisa.

Vyama vinapaswa viwe daraja tu ya kutuvusha kutoka mtu huyu kuwa kiongozi hadi kuleta mtu mwingine kuwa kiongozi na sio ugomvi kati ya hao viongozi wa vyama na ni jambo ambalo linaweza hamia kwa wananchi kama hatua za mapema hazitachukuliwa za kuwaelimisha hao wanaoijiita wawakilishi wa wananchi.

Kama ndiyo hivyo basi mimi naona, vyama vinakuwa vimepoteza maana na msingi wa kuwepo kwake katika jamii ya watu ya dunia ya sasa ya jamii iliyostaarabika kama hapa Tanzania.

Mfano, hadi mahusiano ya mke na mme kwa wabunge duuuh, sasa hii sio ndiyo kuleta watoto yatima katika taifa jamani?
Hebu fikili pale ambapo mbunge wa kike labda tayari kashika ujauzito si watasabisha mtoto awe yatima siku akizaliwa?

Pia, ukawa kuziba mdomo, kutoka bungeni hakuwasaidii wananchi hata tone bora wake waseme huko bugeni ili hata wakiwa na mkutano wanaweza kuwa na hoja ya msingi kuwa tulishauli wakataa, sasa leo wanaziba mdomo, wanatoka nje ya bunge hapo watasema waliwakilisha wananchi kweli?

Mambo mengine, siyo ya kuchekelea ama kukaa kimya ni ya kuwaonya watu walioshindwa kutambua wapelekapo taifa tena pasipo kuangalia wewe ni chama kipi au unatoka katika eneo gani.
Mfano, hii haimuathiri kabisaa aliyenacho ila asiyenacho ndiye ataumia kwa kauli kama hizi na vitendo hivi. Mimi nahisi tunahitaji vyama vya upinzani vipya kama mawazo na mwenendo wa vilivyopo ndiyo vinawaza hivi kama watoto wadogo.

Maana , hapa naona kama tamhthiliya fulani hivi inayoisha bila maudhui yoyote kwa mtizamaji/msomaji kuelewa chochote.

Asanteni.
 
Watu wenye elimu ya hapa na pale ndio think tank ya wabung wa ukiwa...inasikitisha sana.

Haya eti kusitisha mahusiano ya kimapenzi...mtu apate ugwadu afe kimyakimya eti chama...aha!!!
 
Hakuna anayejali hiyo mkuu , Tanzania ndio inaisha hivyo , kama ulikuwa hujui chukua hiyo @ crocodile .
 
Wabadili vipi wakati hata mikutano hawaruhusiwi..!!!!aruhusu kwanza demokrasia nchini
Ndio mambo kama hayo.... Bila shaka na wewe upo kwenye kundi hili hili lisilojua kuwa huu sio utawala wa Kikwete Kitila Mkumbo ameshauri kitu kizuri sana sasa ni upinzani wenyewe kukaa chini na kubadili tactics.
 
Back
Top Bottom