Wabunge wagoma kusalimiana

Wabunge wagoma kusalimiana

Pemba hupandi boti ya mtu kama wewe ni mamluki .
Bibi wa kihindi hujambo? Mmeo anakazi kweli. Hivi huwa ukielezwa unaelewa?
Unaposema mamluki unamaanisha cuf au chadema? Je huu ujinga wa wakos adabu wa chadema huko Dodoma watakuwa wamefundishwa na cuf? Je lengo lao ni kuhurumiwa na NS au wananchi?
Waambieni waache ujinga. Kwao wateule wa ccm hawakwepeki kuwasogelea na kuwalilia shida. Wananchi wako wakihitaji maji utaenda kwa mkurugenzi naye wakati mwingine atakutaka uende kwa waziri alitazame swala kisera.
 
nimesema mara kadhaa hapa. bunge hili limeanza kuongozwa kiubaguzi. wabunge wa ccm hata wakikosea bungeni hawaadhibiwi kamwe. ila upande wa wabunge wa upinzani muda mwingi huadhibiwa kwa makosa yaleyale ambayo hata wabunge wa ccm hufanya. uongozi wa bunge uliangalie jambo hili vizuri. umoja wetu ni muhimu sana kuliko vyama vyetu....
 
Hivi kuna haja ya kusalimia mtu ambae hataki kujibu,salamu ni mara moja akikataa basi,,kwann upoteze mda,,,kila mtu afanye lake,
 
Naomba hii dhambi ya ubaguzi isifike huku mitaani maana tutaanza kuikaribisha hali ya Rwanda 1994.

Hatufiki huko kabisa. Ujinga wa bungeni utaishia huko huko. Wasidhani wananchi ni wajinga. Watatoa jibu 2020
 
Wanachama wataiga kutoka kwa kitendo wanachofanya viongozi wao,wao wapinzania wanadhani wanamkumoa madame spika kumbe wanajikomoa wenyewe na wao ndio wameanza kupandikiza mbegu za chuki na tabia mbaya ,sidhani mtu kama mimi ambaye ndie mpiga kura kususa kwao kunanisaidia kitu ,hapa wanaoumia sio CCM na serikali yake bali wapiga kura majimboni,na sasa ndio tunajua kwamba mpiga kura hana haki na mbunge wake bali viongozi wa vyama ndiowana haki na hao wabunge..

Tumia akili hiyo hiyo ukiyotumia kufikiria mamlaka ya bunge kwa serikali, serikali kwa bunge, wabunge wa ccm kwa wananchi n.k
 
Hatufiki huko kabisa. Ujinga wa bungeni utaishia huko huko. Wasidhani wananchi ni wajinga. Watatoa jibu 2020
Mkuu kumbuka influence ya wanasiasa kwa jamii, pia kumbuka haka kadhambi ka ubaguzi huanza taratibu mwishowe huchipua kama uyoga
 
Nadhani ni muda muafaka kurekebisha kanuni za bunge ili kuondoa huu ujinga unajitokeza. Mbunge yeyote atakaekosekana bungeni kwa shughuli zisizokuwa za kibunge kwa siku 3 anakosa sifa ya kuwa mbunge.

Halafu akishakosa sifa ya kuwa mbunge kinafuatia nini?uchaguzi upya au wanateuliwa na chama au serikali?mbunge kachaguliwa na wananchi na wananchi ndio watakaomtoa, vinginevyo ni kutafuta ugomvi, fujo na machafuko

Vipi kuhusu kubadilisha kanuni kwa ajili ya wabunge wanaofanya mzaha bungeni kama huyu kijana Goodluck?
 
Halafu akishakosa sifa ya kuwa mbunge kinafuatia nini?uchaguzi upya au wanateuliwa na chama au serikali?mbunge kachaguliwa na wananchi na wananchi ndio watakaomtoa, vinginevyo ni kutafuta ugomvi, fujo na machafuko

Vipi kuhusu kubadilisha kanuni kwa ajili ya wabunge wanaofanya mzaha bungeni kama huyu kijana Goodluck?

Siungi mkono anachofanya huyo badluck the same way nisivyounga mkono watu wazima kufanya mambo ya kitoto. Kifuatacho ni uchaguzi upya ili tupate mtu anaevaa matatizo ya wananchi badala ya bunge live
 
Wanachama wataiga kutoka kwa kitendo wanachofanya viongozi wao,wao wapinzania wanadhani wanamkumoa madame spika kumbe wanajikomoa wenyewe na wao ndio wameanza kupandikiza mbegu za chuki na tabia mbaya ,sidhani mtu kama mimi ambaye ndie mpiga kura kususa kwao kunanisaidia kitu ,hapa wanaoumia sio CCM na serikali yake bali wapiga kura majimboni,na sasa ndio tunajua kwamba mpiga kura hana haki na mbunge wake bali viongozi wa vyama ndiowana haki na hao wabunge..
Wewe ni mfiachama,sio nchi
 
Huwezi ukabaka demokrasi nchini halafu utegemee eti wapinzani ndiyo wabadilike kwa sababu tu kuna mbakaji demokrasi.

Kitila Mkumbo amewashauri wanasiasa wa upinzani wabadilishe style ya upinzani kipindi hiki ch Magufuli.. Magufuli ni nyakati nyingine compare to JK
 
Mwache awe kama alivyo na tutaendelea kupoteza diplomasia ya kimataifa maana nchi za wenzetu wanafatilia hali ya nchi ilivyo.Ukikosa ushirikiano mzuri na mataifa mengine hata uchumi utayumba kwa kiwango fulani.
China wapo wanatosha
 
vitu vingne bnaa... ila poa... hyo ndo tz.... mwaka mzima n siasa2...
 
Hii ni ki sana labda wamelenga wabunge wa ccm wapime tena uzito wa hili jambo la kubana upinzani.
 
Hahaha duu hilo la kusitisha mahusiano ya kimapenzi limenivunja mbavu ,
 
Hizi chuki za kutisha miongoni mwa Wabunge chanzo chake ni mbakaji demokrasi na jipu Tulia. Kisha utamsikia tuliombee Taifa letu, utaliombeaje Taifa huku ukipandikiza chuki za kutisha miongoni kwa Watanzania!?
 
Back
Top Bottom