Wabunge wafahamishwe matatizo ya msingi ya mfumo wa elimu nchi hii

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,716
46,432
Ukiwasikiliza wabunge asilimia 99 wakati wanachangia bajeti ya wizara ya elimu ni kama hawafahamu vizuri mzizi wa matatizo ya elimu nchi hii. Wengi wanazungumzia vitu vyepesi sana

Kuwasadia kwa uchache haya ni baadhi ya matatizo makubwa hasa katika shule na vyuo vya serikali;

1. Upungufu mkubwa wa walimu na wakufunzi unaosababisha ufundishaji duni.

2. Uhaba wa madarasa unaosababisha mrundikano wa wanafunzi darasani.

3. Kukosekana kwa chakula shuleni; watoto wanaosoma na njaa watatoka vilaza tu

4. Umbali mrefu kufika shule; Kuna wanafunzi wanavizia lifti kila siku kwenda shule!

5. Uhaba wa vitabu; kila mtoto anatakiwa awe na kitabu chake mwenyewe katika kila somo.

6. Maslahi duni kwa walimu, ili watu wafanye kazi yao vizuri wanahitaji motisha.

7. Vyuo vikuu kushuka ubora. Vimegeuka sehemu za kukariri na kupata vyeti tu badala ya sehemu za midahalo, "critical thinking" na kuzalisha mawazo mapya.

Jikiteni humu badala ya kulalamikia lugha, kutaka kusoma masters bila kufanya mtihani wa kidato cha nne, elimu ya ujasiriamali n.k
 
Nadhani ili tatizo si la wabunge tu kutokujua bali hata wizara ya elimu nayo pia ni kama ipo gizani haifahamu nini inahitaji katika elimu ,ni aina gani ya elimu inapaswa kutolewa katika ardhi ya Tanzania kutokana na mazingira yetu na aina ya watu tuliopo.

Mpaka sasa mtaala wa elimu yetu haueleweki au au endani na mazingira na pia hautaki kubadilika kutokana na dunia inavyoenda wakati tuliopo na tunapopaswa kwenda elimu yetu haizingatii hivi vitu Bali inatolewa tu Kama kukamilisha ratiba tu
 
Leo hii wenzetu wa mataifa ya dunia ya kwanza mfano U.S.A, Japan, China, South Korea, India, Uingereza n.k serikali zao zinapambana na kuwekeza katika elimu bora ya sayansi na teknolojia lakini kwetu bado tunao ule mfumo wa elimu aliokuwa ana utumia Uingereza/Ujerumani katika tawala zao wakati wa ukoloni
 
Inabidi warudi shule mazima. Juzi kati nimeshangaa wabunge wanapiga kelele eti kwanini watoto wanafundishwa binadamu tumetokana na sokwe. Eti mbona leo sokwe hawabadiliki kuwa watu? Halafu wanashangilia sana.

Kama walitoka shule na elimu kuwa binadamu alitokana na sokwe warudi tu shule mazima.
 
Utawekeza katika sayansi na teknolojia bila maabara na kompyuta mashuleni?

Mitaala yetu haina tatizo kubwa, mambo tunayosoma sisi ndio wanayosoma wengine wote duniani, tofauti inakuja kwenye uwezeshaji, miondombinu, ufundishaji na ukosefu wa sehemu za kujifunza kwa vitendo.
Leo hii wenzetu wa mataifa ya dunia ya kwanza mfano U.S.A , Japan, China, South Korea,India, Uingereza n.k serikali zao zinapambana na kuwekeza katika elimu bora ya sayansi na teknolojia lakini kwetu bado tunao ule mfumo wa elimu aliokuwa ana utumia Uingereza/Ujerumani katika tawala zao wakati wa ukoloni
 
Utawekeza katika sayansi na teknolojia bila maabara na kompyuta mashuleni?

Mitaala yetu haina tatizo kubwa, mambo tunayosoma sisi ndio wanayosoma wengine wote duniani, tofauti inakuja kwenye uwezeshaji, miondombinu, ufundishaji na ukosefu wa sehemu za kujifunza kwa vitendo.
Ni kweli vitu tunavyosoma sisi na Duniani wanasoma hivyo Ila tunavisoma katika njia gani mfano science imebase kwenye theoritically na practically. Lakini sisi tumebase theoritically zaidi uku nguvu kidogo ikitumika katika practically ndio maana nasema sisi tupo tofauti na dunia ya kwanza.wao wanafanya kwa ujazo sawa
 
Utawekeza katika sayansi na teknolojia bila maabara na kompyuta mashuleni?

Mitaala yetu haina tatizo kubwa, mambo tunayosoma sisi ndio wanayosoma wengine wote duniani, tofauti inakuja kwenye uwezeshaji, miondombinu, ufundishaji na ukosefu wa sehemu za kujifunza kwa vitendo.
Na maabara zikiwepo bila vifaa au vifaa vikawa vichache na wataalamu pia wa maabara[Laboratory technician] wakawa wachache au wasiwepo inakuwa ni kazi bure
 
Ukiwasikiliza wabunge asilimia 99 wakati wanachangia bajeti ya wizara ya elimu ni kama hawafahamu vizuri mzizi wa matatizo ya elimu nchi hii. Wengi wanazungumzia vitu vyepesi sana

Kuwasadia kwa uchache haya ni baadhi ya matatizo makubwa hasa katika shule na vyuo vya serikali;

1. Upungufu mkubwa wa walimu na wakufunzi unaosababisha ufundishaji duni.

2. Uhaba wa madarasa unaosababisha mrundikano wa wanafunzi darasani.

3. Kukosekana kwa chakula shuleni; watoto wanaosoma na njaa watatoka vilaza tu

4. Umbali mrefu kufika shule; Kuna wanafunzi wanavizia lifti kila siku kwenda shule!

5. Uhaba wa vitabu; kila mtoto anatakiwa awe na kitabu chake mwenyewe katika kila somo.

6. Maslahi duni kwa walimu, ili watu wafanye kazi yao vizuri wanahitaji motisha.

7. Vyuo vikuu kushuka ubora. Vimegeuka sehemu za kukariri na kupata vyeti tu badala ya sehemu za midahalo, "critical thinking" na kuzalisha mawazo mapya.

Jikiteni humu badala ya kulalamikia lugha, kutaka kusoma masters bila kufanya mtihani wa kidato cha nne, elimu ya ujasiriamali n.k

Ndio maana dawa ya corana madaktari wetu wakatengeneza chachangu (pili pili-ilikosa chumvi tu ila unaweza kulia ugali).

Mpaka nikashangaa madaktari bingwa kweli wakutegemewa wanatengeneza chachandu ndio dawa ya corona yaani aibu sana.
 
Nadhani ili tatizo si la wabunge tu kutokujua bali hata wizara ya elimu nayo pia ni kama ipo gizani haifahamu nini inahitaji katika elimu ,ni aina gani ya elimu inapaswa kutolewa katika ardhi ya Tanzania kutokana na mazingira yetu na aina ya watu tuliopo.

Mpaka sasa mtaala wa elimu yetu haueleweki au au endani na mazingira na pia hautaki kubadilika kutokana na dunia inavyoenda wakati tuliopo na tunapopaswa kwenda elimu yetu haizingatii hivi vitu Bali inatolewa tu Kama kukamilisha ratiba tu
Wizara ya elimu inajua sana tu. Huko kuna research nyingi zimo kabatini tu.

Yaani mimi, wewe na wanasias tujue halafu maprofesa wa elimu wasijue?

Tatizo lililopo ni utayari wa wanasiasa kuwekesa katika elimu. Je, wanasiasa wapo tayari kutumia pesa nyingi katika elimu? Au wanaona watakosa posho?

Maoni yangu, ni bora siku moja wanasiasa wafumbe macho watenge bajeti kubwa katika elimu kuliko kuendelea kufumbia macho huku tatizo linazidi kuwa kubwa.

Wanasiasa wa bongo walivyo, wanataka wafanye mambo yanayowagusa wapiga kura moja kwa moja ili waendelee kushika dola, mfano, kujenga barabara, kugawa hela kwa wanajimbo, kuchimba visima, nk.

Lakini ukiwekeza katika elimu, unasubiri muda mrefu kupata matokeo, kitu ambacho wanasiasa wa bongo wanaona ni kupoteza muda na posho, hivyo wanawapeleka watoto wao kupata elimu bora nje ya nchi, huku wakituacha makapuku tunapiga kelele. Na ukifika uchaguzi wanatupa hela mkononi, tisheti na kofia tunawachagua tena
 
Back
Top Bottom