Wabunge wa CHADEMA waliohudhuria Bungeni, watakiwa kujiuzulu nafasi za uongozi Bungeni

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,239
_Wabunge wa Chadema wamemtaka David Silinde ajiuzulu nafasi zake zote za uongozi ( 416 X 640 ).jpg

Wabunge wa Chadema kwa kauli moja wamependekeza kwamba Wabunge wasaliti walioamua kuhudhuria bunge la corona na kupuuza msimamo wa chama chao wa kujitenga na bunge hilo kwa wiki mbili kama mwongozo wa WHO unavyoelekeza ili kuzuia maambukizi ya Virus hatari vya corona , wametakiwa kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama ukiwemo ujumbe wa kamati kuu

Kauli hiyo imetolewa na Mnadhimu wa Kambi rasmi bungeni Mh Ester Bulaya , amesema kwamba ni aibu kwa kiongozi anayeshiriki vikao vya maamuzi vya chama kwa nafasi yake ya uongozi halafu baada ya muda mfupi anapuuza mambo aliyoshiriki kuyaamua .

Ikumbukwe kwamba Chadema haihangaiki na Ubunge wa mtu yeyote , bali wasaliti wanatakiwa kuachia nafasi za uongozi ndani ya chama , ndio maana mpaka sasa Anthony Komu na Joseph Selasini bado ni wabunge .

Mnadhimu wa Kambi rasmi bungeni Mh Ester Bulaya ameandika hivi kwenye mtandao wa Twitter.

Wabunge wa Chadema wamemtaka David Silinde ajiuzulu Nafasi zake zote za Uongozi kwa kushindwa kusimamia makubaliano ya wabunge na Maelekezo ya Chama . Kama Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Naunga Mkono anapaswa kujiuzulu.

Wabunge wa Chadema pia Wamemtaka Mh Mariam Msabaha Ajiuzuru nafasi yake ya ujumbe wa Kamati Kuu kwa kushindwa kufuata makubaliano ya wabunge na Maelekezo ya Chama, Mariamu Msabaha alipata nafasi hiyo kwa kuchaguliwa na Wabunge . Mimi kama Mnadhimu Naunga mkono

=====

UPDATES:

DAVID Silinde, Mbunge wa Momba, Songwe kupitia Chadema ametangaza kujizulu nafasi ya katibu wa wabunge wa chama hicho kuanzia jana Jumatatu tarehe 4 Mei 2020

Silinde ambaye amekuwa mbunge kwa miaka kumi mfululizo amesema amechukua hatua hiyo ya kujiuzulu na tayari barua yake ya imemfikia Freema Mbowe.

Amesema, licha ya barua hiyo kumpelekea Mbowe, pia nakala yake ameipeleka kwa John Mnyika, Katibu Mkuu wa chama hicho.

“Nilijiuzulu jana nafasi ya Katibu wa Wabunge wa Chadema, kwa sababu nimeshindwa kusimamia maagizo ya chama ya kutohudhuria bungeni,” amesema Silinde. Hata hivyo, Silinde hajaweka wazi kama atakihama chama hicho au la.

Wabunge wengine walioingia bungeni jana ni; Joseph Selasini (Rombo), Anthony Komu (Moshi Vijijini), Peter Lijualikali (Kilombero), Jafary Michael (Moshi Mjini) na wabunge viti maalumu, Ratifa Chande, Mariam Msabaha na Sabrina Sungura.

Baada ya Silinde kuchukua uamuzi huo, wabunge wa Chadema wamemtaka Mariam Sabaha kujiuzulu nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, kufuatia hatua yake ya kukiuka maagizo ya chama.

=======

NYONGEZA :

David Silinde hakutia nia kugombea ubunge kwenye jimbo lake la Momba kama Chadema ilivyowataka wagombea wanaotaka kugombea ubunge na udiwani kupitia chama hicho , bali ametia nia kugombea Jimbo la Tunduma ambalo linaongozwa na Mh Mwakajoka .
 
Wabunge wanawakilisha wananchi hawawakilishi Chadema.

Ubunge unaisha 30/5/2020 hawana cha kupoteza!
Wabunge wote wa JMT wanawakilisha vyama vyao, hakuna mbunge binafsi, sasa ninyi ambao kutwa ni siasa za CCM vs Chadema sasa mpate akili ma kuona umuhimu wa katiba mpya ambayo uwakilishi binafsi utambuliwe.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabunge wote wa JMT wanawakilisha vyama vyao, hakuna mbunge binafsi, sasa ninyi ambao kutwa ni siasa za CCM vs Chadema sasa mpate akili ma kuona umuhimu wa katiba mpya ambayo uwakilishi binafsi utambuliwe.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kwamba umeshindwa tu kuitafsiri katiba.

Unadhani Selasini na Komu mle bungeni wanaitumikia Chadema?!!
 
Hayo yamebainishwa leo na na mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni Mh Ester Bulaya.

Anasema wabunge hao ni pamoja na David Silinde anatakiwa kujiuzulu nafasi zake zote ndani ya chama.

Pia mbunge Marian Msabaha wamemtaka ajiuzulu nafasi yake ya ujumbe wa kamati kuu kwa kile kinachodaiwa kushindwa kufuta makubaliano na maagizo ya Chama.

Mh Ester Bulaya anasema kuwa hawawezi kamwe kuwavumilia wasaliti.

"Mimi kama mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani naunga mkono hatua zilichukuliwa na Chama" amesema Ester Bulaya.
 
Back
Top Bottom