Wabunge CCM Wataka Ndugai ang'oke

Wabunge CCM Wataka Ndugai ang'oke

Mnacheza na Ndugai usikute keshaenda kwa sangoma wake kuweka mambo sawa!
 
Ukweli hata ufichwe gizani kwa kipindi kirefu sana ipo siku tu utajitokeza hadharani na watu watashangaaa sana, bunge letu linahitaji reformation kubwa sana tena ya kimfumo ili watu wajue kuwa bunge halisimami kuitetea serikali kwani kwa kufanya hivyo ile dhana ya three pillars of the state inapotea na tunashindwa kabisa kujua nani watetezi wa wananchi
 
Tuache ya msikiti hayatusaidii sana ila kutugawanya zaidi, tatizo letu ni umaskini, utawala mbovu na ubinafsi wa viongozi.. haya ni mambo yanayotuathiri zaidi kuliko nani kasali wapi na nani kachochea udini.. kikubwa ni sis vijana kutokubali kugawanywa ama kwa itikadi za kisiasa ama dini zetu.

hoja ya naibu spika na hili kundi la kupambana na ufisadi nadhani ni uzushi na hata kama lipo halina mantiki mana alichokifanya kinanufaa chama na si vinginevyo na amekuwa na desturi ya kubeba chama chake kadiri awezavyo ingawa najua inawezekana adhabu waliopewa wabunge wa chadema ikafutwa kwa kutofata kanuni na hilo linaweza fanyika na Makinda pamoja na kamati ya maadili na wabunge husika kupewa karipio au onyo.
 
Wamwondoe ndugai kwa lipi wasilolijua ccm jamani?, niliangalia malumbano ya hoja ITV jana usiku nilivyokuwa nasikiliza wachangiaji nikawa nawaza hivi ccm haya hawayajui kweli kwa nini wanaziba masikio, nikajijibu mwenyewe kuwa hii ni style waliyochagua hata mngepiga kelele kiasi gani hawashituki. Wananchi style hii ya ccm iwe ni hamasa ya kushiriki mchakato wa kupata viongozi wapya 2015.
 
Wabunge inabidi waangalie njia nyingine za kujenga hoja na kutetea wananchi nje ya mfumo wa bunge kwani kwa kutegemea bunge hawawezi kama ilivo tokea kwa Mbatia alivyokuja na hoja yake nzuri ya udhaifu wa elimu ikapigwa chini wiki mbili baadae aibu ikalikumba taifa hili kwa kiasi cha kushangaza. Hakuna anaye jail nchi hii hata kama mambo yanaenda ovyo kiasi gani mandhari wanapata wakitakacho hata kama ni kwa njia za kifisadi no body cares.
 
CCM wamechangaikiwa sasa hivi hawajielewi.

CCM hawana utamaduni wa kuheshimu demokrasia ndiomaana hata Pinda na Lukuvi wameonyesha wazi kumchukia Filikunjombe kisa hajaunga mkono hoja ya pinda na ametoa maoni yake kwa mujibu wa katiba ya JMT .
Hivi ni sahihi kweli kwenye nchi hii ya DEMOKRASIA waziri mkuu kuwanunia na kuwatisha kwa lugha flani wabunge wawili wa chama chake kisa hawajaunga mkono hoja ya ofisi ya waziri??

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ninachokiona katika mjadala wa sasa wa bunge ni kuwa bunge limevunja katiba ya nchi, kutokana na ukweli kuwa viongozi wa bunge hawaruhusu wabunge kuzungumza kwa kina yale waliyotumwa na wananchi, lakini pia wamekuwa wanaonyesha upendeleo wa wazi kwa wabunge wa chama cha zamani!

Katiba ya Tanzania imeeleleza majukumu ya kikatiba ya mtu anayeitwa Mbunge wa Bunge, Cha ajabu ni kuwa watu hao wanaoitwa wabunge wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya kikatiba kutokana na kuminywa!!1
 
kumbe ndani ya CCM bado kunawatu wanaakili;.
Wapo wengi tu...hujamsikia yule mama anaitwa sijui kitu gani.....Madabida akichangia bungeni kwamba Dar ziongezwe wilaya zingine saba ili kupunguza foleni?

Wana akili sana hawa!!:lying:
 
Kweli mm nilikuwa nakwenda sana mskitini mwenge pale bt kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 wakawa wanahubili udini mpaka leo sijui mlango wa msikiti.
 
Wapo wengi tu...hujamsikia yule mama anaitwa sijui kitu gani.....Madabida akichangia bungeni kwamba Dar ziongezwe wilaya zingine saba ili kupunguza foleni?

Wana akili sana hawa!!:lying:
heee eeeh kweli hii ndo top layer ya taifa!
 
Bora wamwage ubwabwa tu,hakuna speaker na naibu speaker.
 
Ccm wamemkosa lema mahakamani watamtafuta bungeni.adhabu aliyotoa mhe.ndugai kwa wabunge wa chadema haikustahili kabisa.lengo ni kupunguza'fire power' ya majembe ya cdm mkae mkijua.hata wakibaki cdm wawili bungeni ccm wajue kuwa cha moto watakiona.nawashangaa ccm.wanawanyanyasa wabunge wanaotetea future ya vijukuu vyao!?duh!
 
Ccm wamemkosa lema mahakamani watamtafuta bungeni.adhabu aliyotoa mhe.ndugai kwa wabunge wa chadema haikustahili kabisa.lengo ni kupunguza'fire power' ya majembe ya cdm mkae mkijua.hata wakibaki cdm wawili bungeni ccm wajue kuwa cha moto watakiona.nawashangaa ccm.wanawanyanyasa wabunge wanaotetea future ya vijukuu vyao!?duh!

Mkuu hapo ndipo penye utata, hadi wanashangilia matusi na kukebehi hoja zenye kujenga? Ama kweli ukiwa umagambani akili yote inaota magamba!
 
Ccm wamemkosa lema mahakamani watamtafuta bungeni.adhabu aliyotoa mhe.ndugai kwa wabunge wa chadema haikustahili kabisa.lengo ni kupunguza'fire power' ya majembe ya cdm mkae mkijua.hata wakibaki cdm wawili bungeni ccm wajue kuwa cha moto watakiona.nawashangaa ccm.wanawanyanyasa wabunge wanaotetea future ya vijukuu vyao!?duh!
Hata wakiwafukuza bungeni lakini wananchi wanajua kinachoendelea,Watanzania wa leo siyo wale wa mwaka arobaini na saba.
 
Kwa taarifa za uhakika kutoka kwa mwandishi wa habari aliyeko Dodoma, anasema wabunge wa CCM hasa wale wanaojulikana kama wapambanaji wa ufisadi na wengine,wamekuwa na vikao juzi, jana na leo asubuhi wamekubaliana kuwa ni lazima aondoke kwenye unaibu spika kwa vile amekuwa akitumia jazba badala ya kuzingatia kanuni kwa vile hakuna kanuni inayomruhusu spika kumfungia vikao 5 papo kwa papo.

Pia wanadai amewaharibia mkakati wao ambao walikwisha upanga wa kumfungia Lema kufuatia tuhuma za kumsema Rais kuwa ni mdini, wanadai akifungiwa tena ataonekana anaonewa na hivyo kumpandisha juu kisiasa, kilichowaudhi ni pale walipomwita na hakwenda kuwasikiliza zaidi ya kuwaambia kuwa yupo bize na hakuna kanuni iliyovunjwa, pia akasikika akisema kuwa hizo ni fitna za Sitta kukosa uspika.

Leo wamekubaliana kupeleka azimio lao kwa Pinda na Jenister Mhagama kwa hoja kuwa Ndugai kwa kutumia jazba bila kufuata kanuni anasabisha chama kionekane dhaifu kuwa kinaogopa wapinzani hivyo kukifanya kidharauliwe na kuchukiwa na jamii.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa maazimio yamewekwa kwa maandishi na wamechaguliwa watu wawili kuyapeleka mbele.

Mchakato unaendelea tusubiri tuone.

uhayi wa nyavi ni matundu hayo ndo uhayi wa ccm usidanganye watu nani atamugusa ndungai
 
Kwa taarifa za uhakika kutoka kwa mwandishi wa habari aliyeko Dodoma, anasema wabunge wa CCM hasa wale wanaojulikana kama wapambanaji wa ufisadi na wengine,wamekuwa na vikao juzi, jana na leo asubuhi wamekubaliana kuwa ni lazima aondoke kwenye unaibu spika kwa vile amekuwa akitumia jazba badala ya kuzingatia kanuni kwa vile hakuna kanuni inayomruhusu spika kumfungia vikao 5 papo kwa papo.

Pia wanadai amewaharibia mkakati wao ambao walikwisha upanga wa kumfungia Lema kufuatia tuhuma za kumsema Rais kuwa ni mdini, wanadai akifungiwa tena ataonekana anaonewa na hivyo kumpandisha juu kisiasa, kilichowaudhi ni pale walipomwita na hakwenda kuwasikiliza zaidi ya kuwaambia kuwa yupo bize na hakuna kanuni iliyovunjwa, pia akasikika akisema kuwa hizo ni fitna za Sitta kukosa uspika.

Leo wamekubaliana kupeleka azimio lao kwa Pinda na Jenister Mhagama kwa hoja kuwa Ndugai kwa kutumia jazba bila kufuata kanuni anasabisha chama kionekane dhaifu kuwa kinaogopa wapinzani hivyo kukifanya kidharauliwe na kuchukiwa na jamii.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa maazimio yamewekwa kwa maandishi na wamechaguliwa watu wawili kuyapeleka mbele.

Mchakato unaendelea tusubiri tuone.

acha tu niitwe Tomaso katika hili siamini hata chemebe nasubiria yatokee kweli ndo ntaamini ......................................
 
Back
Top Bottom