Wabongo tunapenda kujipendekeza kwa marehemu

Wabongo tunapenda kujipendekeza kwa marehemu

vyuku

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2012
Posts
503
Reaction score
87
Yaani wabongo ni waajabu sana,hukaa na mtu kwa chuki masengenyo na uadui mkubwa sana,lkn pindipo wanaposikia mtu huyo mefariki ndio wa kwanza kujifanya eti anauchungu sana na marehemu huyo kuliko ndugu zake,vilio vya kinafiki na kujipendekeza ili aonekane marehemu alikuwa mtu wake wakatibu sana,kumbe ni unafik mtupu,wacheni hizo bana usiwe double face.
 
hii imekaa kishari bila upembuzi yakinifu.Napita tu
 
Wewe wasubiri kesho hiyo watakavojazana KIHONDA na miwani myeusi eti wanamsindikiza Ngwea na baada ya mazishi tu hata mama yake Ngwea hatajua kama mwanae alikuwa Bongo fleva maana hakuna mtu atakaepita tena maeneo hayo ya KIHONDA
 
Sasa ile kuvaa miwani meusi ndio idhara ya nini mbona sielewi??
 
Hapo utasikia kila mtu anajisifia kuwa marehemu alikuwa swahiba wake!Sifagilii watu wanaojifanya kumthamini marehemu pindi anapofariki
 
Ile miwani mieusi zuga usijue analia au amefrahi.
 
Hata sisi wananchi ni wanafiki wasanii wakiwa hai hatuwapi sapoti ila wakifaa tu ndio tunajifanya kutakaa kusukuma gari la maiti. HUU NI UNAFIKI MKUBWA......sasa kila kona ukipita ngwea ngwea muda wote mlikuwa wapi hadi mje kuonekana baada ya kifo....acheni unafiki!! kazi yetu ni ku burn CD badala ya kununua kazi original za wasanii mnasubiri wafe ili mjifanye mmeguswa na msiba...
 
Mtu akiumwa au akiwa na matatizo huwaoni na wala hawana taim,zaidi watakusema tu,wakiskia umefariki tu haraka haraka kuja kujifanya swahiba sana
 
jaman haya mambo ya kuiga hayatatufikisha kokote,siku hz hata khanga msiban ni chache,zimekuwa fashion za kparty,tuacheni kuiga jaman kuna vingine sio ustaarabu wetu havifai
 
sasa si redio yetu bana aaah,nao waanzishe yao
Yaani wabongo ni waajabu sana,hukaa na mtu kwa chuki masengenyo na uadui mkubwa sana,lkn pindipo wanaposikia mtu huyo mefariki ndio wa kwanza kujifanya eti anauchungu sana na marehemu huyo kuliko ndugu zake,vilio vya kinafiki na kujipendekeza ili aonekane marehemu alikuwa mtu wake wakatibu sana,kumbe ni unafik mtupu,wacheni hizo bana usiwe double face.
 
Back
Top Bottom