malisak
JF-Expert Member
- Mar 16, 2006
- 694
- 772
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya jiji wameonekana kufurahia ujio wa kiwanda cha Wachina kilichoamua kununua soli za viatu ambavyo vimetumika.
Shuhuda wetu alishuhudia idadi kubwa ya vijana na wazee wakiwa wamejitokeza kwa wingi kiwandani hapo Keko Mwanga tayari kwa ajili ya kupima na kuuza soli za viatu ambazo zimechakaa katika kiwanda hicho.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti vijana hao walisema kuwa, wanauza kilogramu moja ya soli hizo za viatu kwa sh. 400 hivyo wanaona ni bei nzuri na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi kuliko hata vibarua wa viwandani.
Walisema kuwa kwa siku mtu anaweza kupata sh. 30,000 huku wachapakazi wakijinyakulia sh.50,000 hali ambayo inaonyesha kuboresha maisha ya watu wengi.
Baadhi ya wananchi wamesema huenda soli hizo wanunuzi wake hutumia kutengenezea viatu aina ya Yeboyebo wanavyovizalisha.
Biashara ya ununuzi wa soli hizo umezaa matunda kwa kuondokana na kero ya utupaji uchafu uliokithiri ndani ya solo la Mchikichini ambapo hiivi sasa huwezi ukakuta kiatu kichakavu au soli vikiwa vimezagaa.
Baadhi ya vijana walisema kuwa awali wao walikuwa na vibarua katika viwanda vya jirani na hapo lakini walipo ona kuwa dili hilo linalipa ikawalazimu kusimama kazi katika viwanda hivyo kwa ajili ya kujiongezea kipato mpaka hapo watakapo sitisha zoezi hilo hapo baadae.
KWA HISANI YA DARHOTWIRE.COM
Shuhuda wetu alishuhudia idadi kubwa ya vijana na wazee wakiwa wamejitokeza kwa wingi kiwandani hapo Keko Mwanga tayari kwa ajili ya kupima na kuuza soli za viatu ambazo zimechakaa katika kiwanda hicho.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti vijana hao walisema kuwa, wanauza kilogramu moja ya soli hizo za viatu kwa sh. 400 hivyo wanaona ni bei nzuri na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi kuliko hata vibarua wa viwandani.
Walisema kuwa kwa siku mtu anaweza kupata sh. 30,000 huku wachapakazi wakijinyakulia sh.50,000 hali ambayo inaonyesha kuboresha maisha ya watu wengi.
Baadhi ya wananchi wamesema huenda soli hizo wanunuzi wake hutumia kutengenezea viatu aina ya Yeboyebo wanavyovizalisha.
Biashara ya ununuzi wa soli hizo umezaa matunda kwa kuondokana na kero ya utupaji uchafu uliokithiri ndani ya solo la Mchikichini ambapo hiivi sasa huwezi ukakuta kiatu kichakavu au soli vikiwa vimezagaa.
Baadhi ya vijana walisema kuwa awali wao walikuwa na vibarua katika viwanda vya jirani na hapo lakini walipo ona kuwa dili hilo linalipa ikawalazimu kusimama kazi katika viwanda hivyo kwa ajili ya kujiongezea kipato mpaka hapo watakapo sitisha zoezi hilo hapo baadae.
KWA HISANI YA DARHOTWIRE.COM