Wabongo dili hilooo...

malisak

JF-Expert Member
Mar 16, 2006
694
772
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya jiji wameonekana kufurahia ujio wa kiwanda cha Wachina kilichoamua kununua soli za viatu ambavyo vimetumika.

Shuhuda wetu alishuhudia idadi kubwa ya vijana na wazee wakiwa wamejitokeza kwa wingi kiwandani hapo Keko Mwanga tayari kwa ajili ya kupima na kuuza soli za viatu ambazo zimechakaa katika kiwanda hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti vijana hao walisema kuwa, wanauza kilogramu moja ya soli hizo za viatu kwa sh. 400 hivyo wanaona ni bei nzuri na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi kuliko hata vibarua wa viwandani.

Walisema kuwa kwa siku mtu anaweza kupata sh. 30,000 huku wachapakazi wakijinyakulia sh.50,000 hali ambayo inaonyesha kuboresha maisha ya watu wengi.

Baadhi ya wananchi wamesema huenda soli hizo wanunuzi wake hutumia kutengenezea viatu aina ya Yeboyebo wanavyovizalisha.

Biashara ya ununuzi wa soli hizo umezaa matunda kwa kuondokana na kero ya utupaji uchafu uliokithiri ndani ya solo la Mchikichini ambapo hiivi sasa huwezi ukakuta kiatu kichakavu au soli vikiwa vimezagaa.

Baadhi ya vijana walisema kuwa awali wao walikuwa na vibarua katika viwanda vya jirani na hapo lakini walipo ona kuwa dili hilo linalipa ikawalazimu kusimama kazi katika viwanda hivyo kwa ajili ya kujiongezea kipato mpaka hapo watakapo sitisha zoezi hilo hapo baadae.



KWA HISANI YA DARHOTWIRE.COM
 
Hii imekaa vizuri , angalau inapunguza utupaji taka ovyo, Good news.
 
Ndo mwanzo wa kuibiwa viatu ile desturi yetu watanzania ya kuvua viatu kuviacha mlangoni unapoingia ndani kwako au kwa rafiki yako itabidi isitishwe maana viabaka hawatachelewa kuvipitia.............:smile-big:
 
Ndo mwanzo wa kuibiwa viatu ile desturi yetu watanzania ya kuvua viatu kuviacha mlangoni unapoingia ndani kwako au kwa rafiki yako itabidi isitishwe maana viabaka hawatachelewa kuvipitia.............:smile-big:

..itachekesha ikiwa watachukua kiatu chako kwa ajili ya soli, kwa kuwa watahitaji viatu kadhaa kabla hawajapata 1kg na kujipatia shilingi 400 :smile:
 
Ndo mwanzo wa kuibiwa viatu ile desturi yetu watanzania ya kuvua viatu kuviacha mlangoni unapoingia ndani kwako au kwa rafiki yako itabidi isitishwe maana viabaka hawatachelewa kuvipitia.............:smile-big:

jamani mbavu zangu.

mi nafikiri kiatu ni ghali kuliko soli.

Hata kama kimechakaa akikiosha akapita nacho tandale akatangaza dau la 500, anauza fasta...
 
Watanzania bado tuna kazi ndefu!
Mtu anabandika Tangazo kwenye business forum kuhusu biashara ya sole chakavu kwa wachina!! Kuna biashara nyingi za uzalishaji zinalipa sana tu, vijana acheni uzembe wa mjini, njooni shambani jamani tulime na kufuga, pesa zipo shamba jamani, kuajiriwa ni kumzalishia mtu!
 
Watanzania bado tuna kazi ndefu!
Mtu anabandika Tangazo kwenye business forum kuhusu biashara ya sole chakavu kwa wachina!! Kuna biashara nyingi za uzalishaji zinalipa sana tu, vijana acheni uzembe wa mjini, njooni shambani jamani tulime na kufuga, pesa zipo shamba jamani, kuajiriwa ni kumzalishia mtu!

Akarudi baba mmoja,toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja,na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli,iwafae maishani.

Mgonjwa aliwaambia kama mnataka mali mtayapata shambani. Hao madogo wakishamaliza kuokota soli za viatu zote nini kitafuata. Kwa sababu soli hazitupwi kila siku jamani.
 
Watanzania bado tuna kazi ndefu!
Mtu anabandika Tangazo kwenye business forum kuhusu biashara ya sole chakavu kwa wachina!! Kuna biashara nyingi za uzalishaji zinalipa sana tu, vijana acheni uzembe wa mjini, njooni shambani jamani tulime na kufuga, pesa zipo shamba jamani, kuajiriwa ni kumzalishia mtu!


Kaka hujui kuwa sisi wabongo ni mabingwa wa kupenda "shortcuts"? kilimo matunda yake mpaka msimu upite au ng'ombe mpaka akue ndio unaanza kumkamua maziwa wakati soli ya kiatu unaokota na kuuza chapu kwa haraka, hivyo ndivyo tunavyopenda wabongo. Hata hivyo ndugu yangu naunga mkono hoja yako kwa 100%, mimi zamani nilikuwa nafikiri wazungu wametushinda maendeleo kwa bahati tu lakini tangu nije hapa nimegundua wenzetu kumbe wako "serious" sana na kufanya kazi, hata hicho kilimo tunachokikwepa wenzetu wanakithamini vilevile. Sehemu ya umaskini wetu inatokana na UVIVU KATIKA KAZI NARUDIA TENA, UVIVU. Pia tunaendelea tu kuwaangalia wageni wanakuja na kuchukua fursa zetu halafu sisi tunabaki watu wa kuzunguka na kuokota soli chakavu ili tukawauzie hao wageni kwa ajili ya shughuli za kiwanda chao......hii kali mgeni anakua bosi mwenyeji unageuka kibarua....mmmh! na wachina sasa mpaka wataanza kugombea nafasi za uongozi manake wamejaa kila kona!
 
Watanzania bado tuna kazi ndefu!
Mtu anabandika Tangazo kwenye business forum kuhusu biashara ya sole chakavu kwa wachina!! Kuna biashara nyingi za uzalishaji zinalipa sana tu, vijana acheni uzembe wa mjini, njooni shambani jamani tulime na kufuga, pesa zipo shamba jamani, kuajiriwa ni kumzalishia mtu!

Biashara gani nyingi zinazolipa unazome tupe mfano. zinahitaji min capital ya shilingi ngapi? We jiulize wabunge wangapi wana mashamba japo ya mifano majimboni kwao. Sioni kama hii issue ni ya kuzalilisha. Tuache siasa.

Kuna biashara nyingi zinalipa lakini hii ni ya soli chakavu. hii ni sawa sawa biashara ya vitu vya plastic.
 
Ndo mwanzo wa kuibiwa viatu ile desturi yetu watanzania ya kuvua viatu kuviacha mlangoni unapoingia ndani kwako au kwa rafiki yako itabidi isitishwe maana viabaka hawatachelewa kuvipitia.............:smile-big:


Wacha uongo sio desturi ya Watanzania wote kuvua viatu na kuviacha mlangoni. Labda useme waislam wanapokwenda kusali ijumaa kwenye misikiti.
 
Wacha uongo sio desturi ya Watanzania wote kuvua viatu na kuviacha mlangoni. Labda useme waislam wanapokwenda kusali ijumaa kwenye misikiti.
Sio waislam wanapokwenda kuswali tu, watu wengi wanavua viatu hata kwenye milango ya nyumba zao. Si vyema na kukurupuka na neno WACHA UONGO.
 
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya jiji wameonekana kufurahia ujio wa kiwanda cha Wachina kilichoamua kununua soli za viatu ambavyo vimetumika.

Shuhuda wetu alishuhudia idadi kubwa ya vijana na wazee wakiwa wamejitokeza kwa wingi kiwandani hapo Keko Mwanga tayari kwa ajili ya kupima na kuuza soli za viatu ambazo zimechakaa katika kiwanda hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti vijana hao walisema kuwa, wanauza kilogramu moja ya soli hizo za viatu kwa sh. 400 hivyo wanaona ni bei nzuri na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi kuliko hata vibarua wa viwandani.

Walisema kuwa kwa siku mtu anaweza kupata sh. 30,000 huku wachapakazi wakijinyakulia sh.50,000 hali ambayo inaonyesha kuboresha maisha ya watu wengi.

Baadhi ya wananchi wamesema huenda soli hizo wanunuzi wake hutumia kutengenezea viatu aina ya Yeboyebo wanavyovizalisha.

Biashara ya ununuzi wa soli hizo umezaa matunda kwa kuondokana na kero ya utupaji uchafu uliokithiri ndani ya solo la Mchikichini ambapo hiivi sasa huwezi ukakuta kiatu kichakavu au soli vikiwa vimezagaa.

Baadhi ya vijana walisema kuwa awali wao walikuwa na vibarua katika viwanda vya jirani na hapo lakini walipo ona kuwa dili hilo linalipa ikawalazimu kusimama kazi katika viwanda hivyo kwa ajili ya kujiongezea kipato mpaka hapo watakapo sitisha zoezi hilo hapo baadae.



KWA HISANI YA DARHOTWIRE.COM
kasheshe
 
Ndo mwanzo wa kuibiwa viatu ile desturi yetu watanzania ya kuvua viatu kuviacha mlangoni unapoingia ndani kwako au kwa rafiki yako itabidi isitishwe maana viabaka hawatachelewa kuvipitia.............:smile-big:

JS watu wanaiba katika nyumba za ibada mpaka ndala papa na nguru husgangai?, na hata vile viatu vilivyooza na kunadiwa mpaka 500 mchikichini vitapanda bei
 
Back
Top Bottom