Wababa wangapi wanawaogesha watoto wao?

Wababa wangapi wanawaogesha watoto wao?

kwamtoro

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2010
Posts
4,922
Reaction score
3,244
Mke wa rafiki yangu amejifungua wiki kadhaa zimepita, rafiki yangu siku zote alipenda kuwa part of everything going on with his son ikiwa ni pamoja na kumuogesha kichanga. Alimuomba mama mkwe wake ambaye alikuja kumwangalia mtoto wake kabla na wakati amejifungua kumfundisha jinsi ya kumuogesha mtoto. Mama mkwe wake alimfundisha na toka mama mkwe wake ameondoka amekuwa akisaidiana mke wake kumuogesha mtoto. Ana sema ana enjoy sana

Je ni wababa wangapi, tunafanya haya, naomba michango zaidi kwa wababa nini wafanyacho katika kipindi ambacho mke wako amejifungua.
 
Aisee! Nice baba! Ila cdhani kama ataendelea na kwa mtoto atayefuata inawezekana ndo mtoto wake wa kwanza! So full attention! Guud baba!loh! Heee ! Hivi kumbe ni akina baba loh! Nilikuwa sijaonaa!!!
 
mim sijaona hiyo kitu,ata mtoto akikojoa utasikia we mama fulani mtoto amekojoa acha kupika uje umbadilishie nguo,mim sijawai valishwa ata nguo,viatu au kofia na baba.
 
kuvua boxer tu shughuli sembuse kuogesha mtoto? haya tusubiri wakuje watuambie.
 
Inawezekana ni mtoto wa kwanza wa huyu jamaa n'a ni kumuogesha tu anachukulia ujiko ila yakija yale mengine utasikia habari zake n'a wakishakuwa wengi hutasikia tena hizi mambo
 
Mkurugenzi si unajua tena kumuogesha mtoto ni wajibu wa ke!
Kama hayupo sawa!
But akiwepo inakua ngumu sana kwa me kujivika hii duty!!!
Mm nawezamsaidia kupika lakini SI kumsafisha mtoto! Teh teh teh!

hahahahaa sie kwetu utasikia we mama nanihii mwanao amejisaidia njoo umchukue
 
mwanaume anayejitambua lazma awajibike kwa mke na familia yake,mm ni mfano wa baba bora tangu mke wangu ni mjamzito akiwa na miez 4 ya ujauzto alipewa bed rest hvyo ikanilazimu kubeba majukumu yote ikiwa ni kufua,kupka,usafi wa nyumba na mengneyo,hata alipojifungua nimekua nikifanya hvyo hasa pale anapozdiwa na kaz hapa nyumban,mwanangu akiendaa choo au haja ndogo kama nipo namsafisha ikibid hata kumwogesha nafanya hvyo,wanaume achen mfumo dume kuwen postively kwa familia zenu.
 
hahahahaa sie kwetu utasikia we mama nanihii mwanao amejisaidia njoo umchukue

Akisha valishwa vizuri utasikia akiwambia marafiki zake, check chata langu ilo.
 
Nice
Babies that age are very delicate, handle with care. Even some mothers fear to bath some very young babies.
Tell your friend to keep it up!
 
Ni baba mzuri japo hawapo wengi wa aina hiyo.

.............hata hivyo siyo wakuwaamini kihiivyo nao wana madhaifu yao fulani fulani.
 
hakuna baya kwenye kultekeleza hli ila ni kama tu utaweza kufumba macho na maskio
 
hakuna baya kwenye kultekeleza hli ila ni kama tu utaweza kufumba macho na maskio

Wanaume wanaweza sana tu, ila ili neno (LIBWATA) linatugharimu sana. Hasa kama unaishi uswazi.
 
kuvua boxer tu shughuli sembuse kuogesha mtoto? haya tusubiri wakuje watuambie.

Una maanisha wanaume wengi wanasaidiwa kuvua boxer na wake zao au umeamua ku nogesha tu story?. hata kama una ushahidi ujue wanaume kama hao ni ma ubwabwa
 
Mimi nilikuwa na kawaida ya kumuogesha 1st born wangu three years ago, na bado ninafanya hivyo hata sasa wako wawili. lakini si mara zote, ni pale ninapopata fursa. Hata hivyo, mkubwa anasema anafurahi sana nikimuogesha. Ni sehemu ya maisha ambayo inatuweka karibu sana na watoto.
 
hahahhaaa tuko wengi sana bhana, mie ni mmojawapo na hata jana nilishinda nae kutwa nzima wakati Mama yake ameenda msibani Chalinze. Nilimuogesha, nikamlisha, nikambadilisha, mchana wa saa nane nikalala nae hadi saa kumi na moja, tukaamka, nikampa chakula tena tukaendelea kucheza wote, ila Mama yake alipokuja tu urafiki wote ukaisha!!! ana mwaka mmoja na miezi sita tu.
Ni baba mzuri japo hawapo wengi wa aina hiyo.

.............hata hivyo siyo wakuwaamini kihiivyo nao wana madhaifu yao fulani fulani.
 
Back
Top Bottom