Waarusha na mila zao za kijinga!

ndyoko

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,971
1,650
Hiki kituko kimetokea juzi Kiteto.

Eti walimkamata mwenzao wakataka kwenda nae porini kumuadhibu, kisa kawatahiri watoto wake hospitali kwa kutumia ganzi, badala ya ile mila yao-ambayo ni kama ya wamasai-ya kuwatahiri watoto wao porini bila ganzi. Wananchi walipowakataza wasimuadhibu huyo muarusha mwenzao, wakagoma eti mila zao serikali haiwezi kuingilia maamuz yao yanayohusiana na mila zao. Polisi ilibidi waingilie kati na kumuokoa huyo muarusha na kuwakamata baadhi ya waarusha wengine na kuwaweka ndani.

Kasheshe ni pale waarusha wengine walipoamua kwenda kuvamia kituo cha polisi-idadi yao ilikuwa zaidi ya 200. Polisi walifanya kile ambacho wengi wetu tunakijua, na kupelekea waarusha 21 kuwekwa ndani hadi sasa. Jana walienda kuomba kuwawekea dhamana hao wenzao, polisi imechomoa na kuwaambia lazima wakae ndani walau kwa siku zisizopungua 21 ili watie adabu ya kufuta sheria za nchi.

Jamani, kumbe kuna makabila mengine hadi leo bado yanaishi maisha ya mwaka 47. Jamani waarusha mliosoma wabadilisheni akili wenzenu ambao shule imewapitia mbali. Kuna ubaya gani mtu akitahiriwa hospitali then aende huko porini mkale hizo nyama zenu zinazoambatana na sherehe?

Badilikeni bwana, acheni ujinga wa kizamani!
 
Wasumbufu sana hawa watu..
Miezi hii, tokea Januari ni miezi ya hizo tohara, kila ukipita mahali, iwe mjini au mitaani unakutana na makundi ya hawa jamaa wapatao 50 na kuendelea, wamevaa makaniki meusi na fimbo, wakiwa wanazunguka majumbani kuwasaka watu wa kabila lao ili wawaadhibu, andapo watakuwa hawajatahiriwa kwa rika lao!
Hakika wanaboa sana na mila yao ya kizamani....
Nashauri serikali wawatie adabu waporipori hawa, maana wanaondoa amani mitaani na fimbo na sime kila mahali!
 
Unaona ujinga kwa sababu umnepata aceess ya shule
Ni bora hao waarusha wanaosimamia kile wanachokiamini na walishofunzwa kukishika tangu utoto

hawa waliosoma na wanaacha taifa linaangamia tuwaelimisheje??

Madhara ya wakieteto ni jumuisho la uelewa wao. Sasa huoni ni jukumu la hawa walioelimika na wenye access ya kulata maendeleo kuwaelimisha wanakiteto na taifa zima??

Vipi kuhusu albino, kuua vikongwe??
System nzima ibadilike
 
Hiyo perception yenu inaitwa culture ethnocentrism, na nyie ndio wajinga na wapumbavu maana naningilia mila za watu yakwenu yamewasndia ndio maana mumeanza ushoga
 
si mila za kijinga ni mila zilizopitwa na wakati,ni kama kuwa na sh kumikumi hata zikifika milioni sokoni hununui kitu,huwezi kuziita hela za kijinga(ndyoko vipi?)
 
si mila za kijinga ni mila zilizopitwa na wakati,ni kama kuwa na sh kumikumi hata zikifika milioni sokoni hununui kitu,huwezi kuziita hela za kijinga(ndyoko vipi?)

Haya kaka nimekuelewa tena kwa sana mkuu!
 
Wacheni undezi nyie . Mngejua vijana wanavyofundishwa ujasiri msingeongea . Haiwahusu nyie kama inawauma fateni mila zenu za kule kwa malkia . Ingekuta ni kukeketwa hapo ningepinga , kwahili wacha vijana watolewe uwoga . Matumoki nanu .
 
Back
Top Bottom