ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Hiki kituko kimetokea juzi Kiteto.
Eti walimkamata mwenzao wakataka kwenda nae porini kumuadhibu, kisa kawatahiri watoto wake hospitali kwa kutumia ganzi, badala ya ile mila yao-ambayo ni kama ya wamasai-ya kuwatahiri watoto wao porini bila ganzi. Wananchi walipowakataza wasimuadhibu huyo muarusha mwenzao, wakagoma eti mila zao serikali haiwezi kuingilia maamuz yao yanayohusiana na mila zao. Polisi ilibidi waingilie kati na kumuokoa huyo muarusha na kuwakamata baadhi ya waarusha wengine na kuwaweka ndani.
Kasheshe ni pale waarusha wengine walipoamua kwenda kuvamia kituo cha polisi-idadi yao ilikuwa zaidi ya 200. Polisi walifanya kile ambacho wengi wetu tunakijua, na kupelekea waarusha 21 kuwekwa ndani hadi sasa. Jana walienda kuomba kuwawekea dhamana hao wenzao, polisi imechomoa na kuwaambia lazima wakae ndani walau kwa siku zisizopungua 21 ili watie adabu ya kufuta sheria za nchi.
Jamani, kumbe kuna makabila mengine hadi leo bado yanaishi maisha ya mwaka 47. Jamani waarusha mliosoma wabadilisheni akili wenzenu ambao shule imewapitia mbali. Kuna ubaya gani mtu akitahiriwa hospitali then aende huko porini mkale hizo nyama zenu zinazoambatana na sherehe?
Badilikeni bwana, acheni ujinga wa kizamani!
Eti walimkamata mwenzao wakataka kwenda nae porini kumuadhibu, kisa kawatahiri watoto wake hospitali kwa kutumia ganzi, badala ya ile mila yao-ambayo ni kama ya wamasai-ya kuwatahiri watoto wao porini bila ganzi. Wananchi walipowakataza wasimuadhibu huyo muarusha mwenzao, wakagoma eti mila zao serikali haiwezi kuingilia maamuz yao yanayohusiana na mila zao. Polisi ilibidi waingilie kati na kumuokoa huyo muarusha na kuwakamata baadhi ya waarusha wengine na kuwaweka ndani.
Kasheshe ni pale waarusha wengine walipoamua kwenda kuvamia kituo cha polisi-idadi yao ilikuwa zaidi ya 200. Polisi walifanya kile ambacho wengi wetu tunakijua, na kupelekea waarusha 21 kuwekwa ndani hadi sasa. Jana walienda kuomba kuwawekea dhamana hao wenzao, polisi imechomoa na kuwaambia lazima wakae ndani walau kwa siku zisizopungua 21 ili watie adabu ya kufuta sheria za nchi.
Jamani, kumbe kuna makabila mengine hadi leo bado yanaishi maisha ya mwaka 47. Jamani waarusha mliosoma wabadilisheni akili wenzenu ambao shule imewapitia mbali. Kuna ubaya gani mtu akitahiriwa hospitali then aende huko porini mkale hizo nyama zenu zinazoambatana na sherehe?
Badilikeni bwana, acheni ujinga wa kizamani!