Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wakati vumbi la hoja kuhusu posho zaidi ya moja kwa kazi ile ile halijatua, niliangalia Star TV ambapo kulikuwa na mjadala kuhusu waandishi wa habari kulipwa posho hizo! Kwa haraka haraka nilipata mambo mawili makuu kwenye mjadala huo: 1. Je, mwandishi wa habari akilipwa posho na yule ambaye amemwalika kwa ajili ya kuandika habari kwa ajili ya tukio fulani (km kampeni za uchaguzi) ataandika kweli hata mabaya ya mlipa posho kama yapo? Kama sivyo, weledi (professionalism) uko wapi hapa? 2. Baadhi ya waandishi wa habari wanalipwa mishahara midogo na wengine hawalipwi (wanaishi kwa posho), je, wakiacha kupokea posho watajikimu namna gani? Naleta mjadala huu kwenu wadau kwa ajili ya brainstorming, nini kifanyike ili kuwanusuru waandishi wa habari na utumwa kwa wenye fedha?