Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,420
Bwana Said Mtanda , ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mara ametangaza hadharani na kumuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuanza kuwalipa posho ya sh 120, 000 , waandishi wa habari wanaoambatana nao kwenye shughuli zao
Akizungumza kwa style ya Majivuno na kujigamba , Bwana Mtanda amedai kwamba Mkuu wa Mkoa ni mtu mkubwa , haiwezekani wanaoambata naye walipwe hela ndogo kama elfu 30 , na kwamba kuanzia leo waanze kulipwa kitita kipya , Hata hivyo Mtanda amekiri kwamba jambo hilo analolifanya halipo kwenye kanuni , ila amedai kutoka na ukubwa wake kama Mkuu wa Mkoa ni lazima lifanyike .
Bali hoja yetu ni hii , Waandishi wa Habari ni waajiriwa wa vyombo vyao vya habari , kwanini walipwe na RC wanapokuwa kwenye majukumu yao , Je hii ni Rushwa ili kuficha uchafu wa Mtanda , ambaye anatajwa mara kadhaa kutoroka Majukumu ya kiofisi ili kwenda kuangalia mechi za Yanga ? Je ni Mikoa mingapi inayomwaga Bahasha za Khaki kama anavyofanya Mtanda , na zinatoka kwenye mfuko gani wa serikali ?
Akizungumza kwa style ya Majivuno na kujigamba , Bwana Mtanda amedai kwamba Mkuu wa Mkoa ni mtu mkubwa , haiwezekani wanaoambata naye walipwe hela ndogo kama elfu 30 , na kwamba kuanzia leo waanze kulipwa kitita kipya , Hata hivyo Mtanda amekiri kwamba jambo hilo analolifanya halipo kwenye kanuni , ila amedai kutoka na ukubwa wake kama Mkuu wa Mkoa ni lazima lifanyike .
Bali hoja yetu ni hii , Waandishi wa Habari ni waajiriwa wa vyombo vyao vya habari , kwanini walipwe na RC wanapokuwa kwenye majukumu yao , Je hii ni Rushwa ili kuficha uchafu wa Mtanda , ambaye anatajwa mara kadhaa kutoroka Majukumu ya kiofisi ili kwenda kuangalia mechi za Yanga ? Je ni Mikoa mingapi inayomwaga Bahasha za Khaki kama anavyofanya Mtanda , na zinatoka kwenye mfuko gani wa serikali ?