Habari zenu!
Pamoja na kwamba sio rahisi na haiwezekani kuridhisha watu wote, pia kukosolewa pale mtu anapoenda kinyume ni sahihi au kukosolewa ili kujijenga zaidi, INARUHUSIWA.
Binafsi, mh rais mstaafu wa awamu ya nne naona amefanya vizuri.
Katika kipindi cha JK nimefanikiwa:
- Kusoma hadi elimi ya juu bila kupitia chuo cha UDSM ambacho kilikuwa ndio chuo kikuu kikubwa kabla ya JK kuingia madarakani, JK kaweka miundo mbinu iliyowezesha hili.
Nina ndugu, jamaa na marafiki ambao wamefanikiwa kupata elimu pia na kuweza kuitumia hiyo elimu ktk kujikwamua kimaisha. JK kaweka mazingira ya kuwezesha vyuo vikuu binafsi na vya serikali kuongezeka. Ni wewe tu!
-Nishati: Bibi yangu kijijini ana umeme siku hizi nyumbani kwake.
-Maji: kuna kisima cha maji mita kama hamsini toka anapoishi bibi yangu kijijini, hii imewezekana wakati wa uongozi wa JK.
-Kwenda kijijini, kutoka Dar likuwa inachukua masaa mengi zaidi ya 14, barabara haikuwa nzuri, sasa ni mkeka!
-JK katuwezesha kujielezea zaidi, freedom of expression imekuwa kubwa sana.
-nk
KWA UJUMLA, JK KAWEKA MIUNDO MBINU MIZURI AMBAYO KAMA ITAENDELEZWA NA KUTUMIWA BASI ANGALAU TUTASONGA MBELE.
JE KWAKO NI KIPI KITU CHANYA KINACHOWEZA KUKUFANYA UMKUMBUKE JK NA UONGOZI WAKE?
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki watanzania, Mungu wabariki marais wastaafu, na Mungu mbariki RAIS MPYA DR. John Pombe Magufuli.
Siasa tuweke kando, uchaguzi umeisha, tujenge nchi, na kama ni kukosoana eidha kwa sisi kwa sisi au kisiasa, basi tufanye iwe ktk CONSTRUCTIVE CRITICISM.