Vyuo Vikuu visivyo na sifa kufutwa!

Vyuo Vikuu visivyo na sifa kufutwa!

Prof. Ndalichako naomba atazame pia kwenye suala kudahili yaani unakuta mtu kapata E E S alafu yupo chuo kikuu anachukua Education na anapata mkopo kama kawaida. Kiukweli hivi vyuo vikuu uchwara vimekuwa kimbilio la watu wenye ufahulu hafifu na kibaya zaidi wanakimbilia kwenye kozi za education ili wapate mikopo.
umezingatia viwango vinavyoruhusiwa kuchukua degree au umeongea tu kwa hisia zako
 
Serikali ina mpango wa kukagua vyuo vikuu vyote nchini na vile ambavyo vitakuwa havina sifa itavifunga bila kusita kwani haitaki watanzania wafanyiwe majaribio katika elimu.

Taarifa hiyo imetolewa na waziri wa Elimu,Prof. Ndalichako ambaye amesema vyuo vingi havina sifa licha ya vyuo hivyo kupewa ithibati.

Prof. Ndalichako amesema inatakiwa angalau asilimia 50 ya walimu katika kila chuko kikuu kimoja wawe na shahada ya uzamivu(Ph.D) na kwamba haitakiwi mwalimu mwenye shahada ya kwanza kufundisha wanafunzi wa shahada ya kwanza.

Prof. ameongeza kuwa uwepo wa vyuo vingi visivyo na sifa kunapelekea uwepo wa vijana wengi wasio na ajira mitaani na hivyo kuongeza hasira.


Chanzo: Nipashe

Prof. Kaeleza mengi ambayo ninahakika yakifanyiwa kazi,vyuo vingi vitafungwa na itakuwa majanga makubwa.

Hasira za nini?! Na hasira za kina nani?! Na juu ya nani??!
 
Kutokuwepo kwa ajira kunasababishwa zaid na kutokuwepo uwekezaji wa kutosha ktk sekta zinazozalisha ajira kwa wingi mfano viwanda vya usindikaj mazao ya kilimo, samaki, na mazao ya biashara, sidhan kama inasababishwa na ukosefu wa walimu wenye sifa ktka vyuo, unless kuna study imefanyika kuprove hiyo, nakubali vyuo vimekuwa vingi na ubora wake ni wa mashaka mfano vyuo vingi sana viko kariakoo havieleweki vizur, wakati tukifuta vyuo visivyo na sifa tuangalie pia je wahitaji walikuwa na sifa za kuingilia vyuon? kama wanazo na wamekosa vyuo linaweza kuwa tatizo jingine, ambalo linatukabili saiv, kuwa na wanafunz wenye sifa za kwenda chuo, pengine wengine wanaweza kujilipia lkn kwa ile kasumba ya kubalance supply ya wanaomaliza vyuo na nafasi za kaz ikasababisha kuwa na wataalam wachache mfano kwene fan ya udaktari.

Umenena vyema comrade!! Na sidhani kufuta vyuo hivyo kutasaidia kupunguza IDADI YA VIJANA WASIO NA AJIRA MTAANI, kama chanzo kinavyoripoti....
Binafsi nadhani ni busara sasa shule na vyuo vya ufundi viboreshwe ili kuwajengea vijana elimu ya ujasiliamali na ubunifu. Vyuo vingi vinaandaa waajiriwa, ila ajira rasmi ni chache mno tanzania, kuna article moja nilisoma siku chache nyuma, ratio ya ajira na wafanyakazi (wanaotafuta) ni 1:101......now this is bad.
 
.......na hili suala la wenyeviti wa vyama vya siasa kuwa na elimu ya form six failure inabidi litizamwe upya na msajiri wa vyama.

Hili ni JIPU na lishaiva tayari na sasa litumbuliwe tu.
Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
 
Back
Top Bottom