Vyuo Vikuu visivyo na sifa kufutwa!

Vyuo Vikuu visivyo na sifa kufutwa!

Na kama nchini serikali inajua kabisa ya kuwa kuna makampuni tena yanajitangazia kuwaandikia watu Research proposal, thesis na mpaka data unapewa halafu serikali haifanyi chochote ujue hiyo nchi elimu yako iko kwenye rehani.
Na kitu chengine thesis moja inaweza kutumiwa na watu tofauti bila ya wasi wasi wowote na ukija suala la plagiarism huku ni balaa kabisa kwani naweza kusema more than 80% ya thesis zinazoandikwa na vyuo vya tz basi ziko hivyo
mkuu post yako imenitisha kidogo. unaushahidi kweli na ulichokiandika? au ni majungu tu. siku hizi kuna software za kuditect plagiarism. waambieni hao maporofeseri wa vyuo vyetu wazitafute.
 
mkuu post yako imenitisha kidogo. unaushahidi kweli na ulichokiandika? au ni majungu tu. siku hizi kuna software za kuditect plagiarism. waambieni hao maporofeseri wa vyuo vyetu wazitafute.
Nilichoandika hapo nina ushahidi nacho na wanafunzi wa mzumbe wanaongoza na kwa wanaosoma masomo ya biashaara ni kitu cha kawaida.
 
Chama kitaingilia kati kunusuru wananchi wake.
Hata chama kisipoingilia kati, yeye mwenyewe hawezi kuwa na huo ubavu wa kufuta vyuo vyote! Manake sidhani kama kuna chuo chenye at least 50% PhD Lecturers ukiondoa UDSM na SUA...
 
Nilichoandika hapo nina ushahidi nacho na wanafunzi wa mzumbe wanaongoza na kwa wanaosoma masomo ya biashaara ni kitu cha kawaida.


Ni kweli mkuu kwa hiyo Mzumbe hasa tawi la DSM ni shida. Kuna siku nilienda pale ukiwaangalia tu kwanza hao wanafunzi walivyo unaona kabisa hawa watu hawawezi andika hizo dessertations
 
Tatizo kubwa katika elimu ya vyuo vikuu ni kudumaa kwa mitaala dunia ya sasa inahitaji specialization haswa na siyo just general understanding. Course kama agriculture general inatakiwa ivunjwe vunjwe into specific crops I.e. Tomato production, onion, watermelon etc etc

Animal science break into poultry production, dairy, beef, pig depending on market and economic drivers. Lengo langu ni kwamba mtu hawezi competent kwenye vyote na hawezi kutumia ujuzi wote lakini akifundishwa kuku tu alafu ikiwa more practical zaidi it's easy for a graduate to become a successful entrepreneur
 
Ni kweli mkuu kwa hiyo Mzumbe hasa tawi la DSM ni shida. Kuna siku nilienda pale ukiwaangalia tu kwanza hao wanafunzi walivyo unaona kabisa hawa watu hawawezi andika hizo dessertations
Na kuna chuo kimoja kinaitwa ZANZIBAR UNIVERSITY kinatoa degree ya nursing ni aibu tupu
 
Aanze na T.I.A dar hiki kitaasisi ni Jipu kubwa mno kuliko vyuo vyote TZ
 
Serikali ina mpango wa kukagua vyuo vikuu vyote nchini na vile ambavyo vitakuwa havina sifa itavifunga bila kusita kwani haitaki watanzania wafanyiwe majaribio katika elimu.

Taarifa hiyo imetolewa na waziri wa Elimu,Prof. Ndalichako ambaye amesema vyuo vingi havina sifa licha ya vyuo hivyo kupewa ithibati.

Prof. Ndalichako amesema inatakiwa angalau asilimia 50 ya walimu katika kila chuko kikuu kimoja wawe na shahada ya uzamivu(Ph.D) na kwamba haitakiwi mwalimu mwenye shahada ya kwanza kufundisha wanafunzi wa shahada ya kwanza.

Prof. ameongeza kuwa uwepo wa vyuo vingi visivyo na sifa kunapelekea uwepo wa vijana wengi wasio na ajira mitaani na hivyo kuongeza hasira.

Chanzo: Nipashe

Prof. Kaeleza mengi ambayo ninahakika yakifanyiwa kazi,vyuo vingi vitafungwa na itakuwa majanga makubwa.


Dr. Ndalichako mimi nadhani kwa kuisadia sekta ya Elimu kwa nchi hii basi ni bora tuka base kwenye Elimu Bora na sio Bora Elimu. Chuo, kwa mfano UDSM ni chuo cha zamani na kinaweza kawa na hao 50% ya PHd holders unaosema lakini tuangalie quality ya hao Lecturers na Graduates wake . Wengi wa hao malecturers wenyewe ndio wanashia kuwa Mafisadi jee si watakuwa pengine hata wanawapa wanafunzi mitihanii majumbani? Angalia mfano wa Pro. Tibaijuka katoka hapo UDSM (escrow). Muangalie Chenge ni Product ya Havard lakini ni fisadi nyangumi. hali kadhalika Pro. Muhongo. Mimi nadhani kwa huku tulikofika nadhani suala la Educational Ethics likawa ni lazima.
 
Pia chanzo ni kuwapa mikopo wanafunzi wanaojiunga vyuo binafsi. Wanahongo huko TCU kusajili chuo then wao wanapiga hela kwa wanafunzi
 
Huyu sasa anaanza kuboronga..mtu makini huwezi kutoa kauli ambayo unajua haitekelezeki. Hilo la kufunga vyuo ambavyo havina asilimia 50 ya wahadhiri wenye phd atachemka tu???
 
Pia chanzo ni kuwapa mikopo wanafunzi wanaojiunga vyuo binafsi. Wanahongo huko TCU kusajili chuo then wao wanapiga hela kwa wanafunzi
Kweli kabisa, tisiyuu ni Jipu.
Nadhani ni bora TCU isiwepo maana ndio chanzo cha elimu kudorora..
Mheshimiwa prof aanze na TCU!
 
Wenye PhD na maprofesa wote wamekimbilia siasa, angalia baraza la mawaziri. Inabidi tujue namna yakuwatumia wasomi wetu.
 
Kwa vigezo hivyo vitafungwa vyuo vingi sana. Pale MUHAS mwalimu ana master ana msupervise master student.. only in Tz
Kwa medical school aliye kutangulia kusoma ndie mkubwa bro, Mwanafunzi wa masters(resident) husimamiwa na specialist au expert katika field husika na pia huyo resident anasifa za kuwasimamia MD students na Intern doctors. Mkuu utaalam wa maswala ya tiba ni exposure ktk cases mbalimbali na si vinginevyo.
 
Kwa vigezo hivyo vitafungwa vyuo vingi sana. Pale MUHAS mwalimu ana master ana msupervise master student.. only in Tz
Nenda pia UDOM ukaone maajabu hayo kwenye baadhi ya Faculties.
 
Chuo cha kwanza kufutwa lazima kitakuwa kilichomtunuku Profesa maji marefu kada wa chama cha mapinduzi
 
Back
Top Bottom