Vyama vya wafanyakazi Tanzania vinakwama wapi?

Mwesige

Member
Oct 21, 2010
45
12
Kwanza nitangaze wazi kwamba Mimi ni Kiongizi Mwandamizi wa Chama cha wafanyakazi sekta ya Nishati na Madini (Sekta ya Uziduaji) Tanzania, kinaitwa kwa ufupi NUMET.

Pamoja na kwamba hatuhusiki sana na wafanyakazi wa sekta ya umma ambayo inalalamika sana kwasababu za kutoongezwa mishahara, na masilahi mengine, na sisi pia kwenye sekta binafsi wanachama wetu hawako na furaha kama tulivyotarajia au kama walivyotarajia.

Kuna mambo mengi tunafanya, Lakini kwasababu mbalimbali kuna mambo mengi hatujafanya. Lakini angalau kuna juhudi zinafanyika na baadhi ya wanachama wetu wanashiriki moja kwa moja.

Lakini, ukitafuta kiwango cha wafanyakazi nchini kuridhishwa na huduma zitolewazona vyama vya wafanyakazi nchini kwa ujumla wake, ni kidogo sana.

Jukwaa hili lina watu wenye uelewa wa mambo mengi sana. Mnafikiri vyama hivi vinakwama wapi? Maana kuendelea kulalamika tu bila kutoa suluhu inaweza isisaidie sana kujikwamua kwenye mkwamo huu.

Karibuni tujadili.

Nicomedes M Kajungu
Katibu Mkuu
NUMET
MWANZA HQ
T
 
Kwanza nitangaze wazi kwamba Mimi ni Kiongizi Mwandamizi wa Chama cha wafanyakazi sekta ya Nishati na Madini (Sekta ya Uziduaji) Tanzania, kinaitwa kwa ufupi NUMET.

Pamoja na kwamba hatuhusiki sana na wafanyakazi wa sekta ya umma ambayo inalalamika sana kwasababu za kutoongezwa mishahara, na masilahi mengine, na sisi pia kwenye sekta binafsi wanachama wetu hawako na furaha kama tulivyotarajia au kama walivyotarajia.

Kuna mambo mengi tunafanya, Lakini kwasababu mbalimbali kuna mambo mengi hatujafanya. Lakini angalau kuna juhudi zinafanyika na baadhi ya wanachama wetu wanashiriki moja kwa moja.

Lakini, ukitafuta kiwango cha wafanyakazi nchini kuridhishwa na huduma zitolewazona vyama vya wafanyakazi nchini kwa ujumla wake, ni kidogo sana.

Jukwaa hili lina watu wenye uelewa wa mambo mengi sana. Mnafikiri vyama hivi vinakwama wapi? Maana kuendelea kulalamika tu bila kutoa suluhu inaweza isisaidie sana kujikwamua kwenye mkwamo huu.

Karibuni tujadili.

Nicomedes M Kajungu
Katibu Mkuu
NUMET
MWANZA HQ
T
Soma sheria iitwayo "Master Servant Act" ya 1823. Ndiyo inayohusika bongoland.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Juzi nilibandika uzi humu nikapendekeza ikiwezekana hivi vyama kama vitashindwa mwaka huu 2020 kutetea maslahi ya watumishi vifutwe maana havina msaada kwa watumishi kazi zake ni kukata pesa za watumishi tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vyama vya wafanyakazi ni mzigo mwingine kwa wafanyakazi, yaani ukiweka PAYE, mishahara duni, poor working conditions, unyanyasaji na vyama vya wafanyakazi, hao ndio maadui wa ustawi wa wafanyakazi Tanzania.
Suluhisho ni kwa
Vyama vya wafanyakazi kujitoa kwenye kwapa za CCM (Siasa) au wafanyakazi wajitoe kwenye vyama hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni ujinga kuendelea kuwaamini viongozi wanao negotiate na employers 5* hotels.
Hii ni mbinu ya kuwalemaza wasifanye kazi yao.
Jitoeni maana thamani yao ni ninyi, ninyi msipokuwepo hawana thamani waliyonayo kwa muajiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wanajukwaa!

Nimekuwa nikitafakari kwa kina juu ya kazi za vyama vya wafanyakazi na mchango Wa vyama hivyo kwa wanachama wake yaani watumishi Wa Umma.

kwa upande wangu sijaona kama vina msaada kwasababu watumishi hawapandi vyeo wala kupata ongezeko la kila mwaka yaani annual increment, cha ajabu watumishi bado wanaendelea kuwa wanachama.

Vyama hivi kazi yake kubwa ni kuwanyonya wanachama wake badala ya kuwasaidia kupata stahiki zao, kwa jicho la tatu nahisi vyama hivi ni vibaraka vya serikali kuu na huenda wanakula pamoja. Huenda kuna wanachama wanaofaidika, naomba watupatie ushuhuda ili tusiendelee kuwa na fikra potofu.

Naomba kuwasilisha.
 
Mimi niliwatimua walipokuja kutaka kuanza kunikata nikawaambia wasithubutu kunikata maana hawana msaada kwangu
Habari wanajukwaa! Nimekuwa nikitafakari kwa kina juu ya kazi za vyama vya wafanyakazi na mchango Wa vyama hivyo kwa wanachama wake yaani watumishi Wa Umma, kwa upande wangu sijaona kama vina msaada kwasababu watumishi hawapandi vyeo wala kupata ongezeko la kila mwaka yaani annual increment, cha ajabu watumishi bado wanaendelea kuwa wanachama. Vyama hivi kazi yake kubwa ni kuwanyonya wanachama wake badala ya kuwasaidia kupata stahiki zao, kwa jicho la tatu nahisi vyama hivi ni vibaraka vya serikali kuu na huenda wanakula pamoja. Huenda kuna wanachama wanaofaidika, naomba watupatie ushuhuda ili tusiendelee kuwa na fikra potofu. Naomba kuwasilisha.

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Mtumishi!
joysafaribay_B7wLTIgiiGw.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom