Vurugu Zanzibar, makanisa yachomwa moto!

Naogopa kusema kuwa kama hoja hii ina mashiko, basi hili ni janga la kitaifa ! Leo linatokea kule kwa mgongo wa kuukataa Muungano kwa kuwa una mapungufu mengi, Nani anajua kesho wenye mapesa watashinikiza nini ili hali ninyi ni watu wa kusema NDIO MZEE!!!!! Poleni sana wenzetu kwa kuwa maboya!
 
Usiogope kuitwa Kafir! Anayekuita hivyo ni mwanadamu wala si Mungu! Mungu aliyekuumba anajua kuwa wewe si Kafir! Achana na wasiojua wanachokifanya, wanaficha udini mgongoni mwa Muungano! Sijasikia dini ikiunganisha Taifa! Kama ingekuwa hivyo Somalia na nchi nyingine za Kiarabu wasingeendelea kuchinjana!

Well said!
 
Kwa mujibu wa Falsafa za Consequencialism Means justify the end.
Means (KITENDO CHA KUCHOMA MAKANISA) justifies the end (CHUKI NA HASIRA ZA KIDINI)
 
Shein anaweza kuogopa viongozi kadhaa wa SUK wanaounga mkono uhaini huu laki JMT inaweza kumwambia achague kuwa rais au kuungana na hawa wahuni. CCM imekosea mengi sana hawakupaswa kuwachagulia wazanzibari galasa lakini huyu ni zao la galasa lililokataliwa na mwl Nyerere-mkwe.re na wasipofanya marekebisho 2015 tutafikishwa na JWTZ
 
nimeona itv eti na leo walikuwa wanataka kuchoma kanisa katoliki...hawa jamaa wamekula tende sana sasa wanataka kuonja shubiri...!
 
Wakati virugu zikiendelea kujitokeza huko Zanzibar ni vizuri Watanzania kutambua na kukumbuka yafuatayo:- 1. Muungano kati ya Tanganyika na visiwa vya Unguja na Pemba ndio ulio pelekea kupatikana kwa nchi ya Tanzania. 2.Mafanikio yanayopatikana kutokana na muungano ni mengi kuliko matatizo. 3. Ni jukumu la kila mtanzania kupigania na kudumisha amani iliyopo. ANGALIZO- Tusiruhusu kikundi au baadhi ya watu kuvunja amani na muungano uliodumu kwa zaidi ya nusu karne.
 
Wakati virugu zikiendelea kujitokeza huko Zanzibar ni vizuri Watanzania kutambua na kukumbuka yafuatayo:- 1. Muungano kati ya Tanganyika na visiwa vya Unguja na Pemba ndio ulio pelekea kupatikana kwa nchi ya Tanzania. 2.Mafanikio yanayopatikana kutokana na muungano ni mengi kuliko matatizo. 3. Ni jukumu la kila mtanzania kupigania na kudumisha amani iliyopo. ANGALIZO- Tusiruhusu kikundi au baadhi ya watu kuvunja amani na muungano uliodumu kwa zaidi ya nusu karne.
nime-highlight kabisa kwa wino mwekundu kuonyesha uzito wa ujumbe.
 
Tuwape uhuru wao. Kwa nini tuwalazimishe kuwatawala? Suala wanadhamiwa na nani si muhimu, cha muhimu ni kuwapa mamlaka ya kujiamulia mambo yao wenyewe.
 
Hivi taarifa za kiintelegencia zinasemaje? Itakuwa ni CHADEMA hao ndiyo wanafanya fujo maana hichi ni chama cha fujo na kisichopenda Amani. Halafu huko zenji CUF na CCM siwameshika hatamu? Mbona hivyo? Au kwavile makanisa ndiyo yanachomwa na wao viongozi wao ni Waislamu? Inamaana wanafurahia haya matukio? Hebu great thinkers nifahamisheni
 
waavunje tu,me sioni faida ya muungano...Tanganyika bila zanzibar inawezekana...over
 
Ndoa isiyo na ridhaa ya wanandoa ni batili na inastahili kuvunjwa. Siyo utumie mabavu kwa kuwa unayo kuhalalisha ndoa ambayo mmoja wa wanandoa hana ridhaa nayo. Tutawaita wazanzibar majina mbali mbali; wahuni, magaidi nk. Lakini ukweli utabaki pale pale kwamba wana haki ya kuuhoji muungano maana unagusa maisha yao ya kila siku. Na siyo kuwashinikiza kwa kutumia polisi au majeshi.
 
Comrade umeongea mambo mazito sana utakuwa ni ujinga mweupe kabisa kama tutaendelea kuwatazama tu hao wachache wanaoitia kidole mboni ya jicho la Muungano,
Hakika tusikubali kakikundi hako katuvurugie amani yetu
 
No research NO right to write nonsense....Hakuna anaewadhamini wala nini Hizo nchi sijui mara OMAN,IRAN nk zina maslahi gani ZANZIBAR? Mbona km ni utajiri wa mafuta hizo inchi ndo zinaongoza...Chamsingi hapa huu muungano upitiwe upya na km ni vuguvugu la kujitenga lipo miaka yote tokea ata waasisi wapo NYERERE analifahamu mpaka KIKWETE analifahamu..Hakuna haja ya kusingizia nchi fulani eti ndio inafadhili itafikia wakati ata CHADEMA itasingiziwa eti kinafadhiliwa na chama fulani cha UINGEREZA....Tuache unafiki wetu wa bara kwani ata sisi tunamatatizo yetu mengi tu ya baadhi ya mikoa kutengwa kimaendeleo sasa wananchi wakiungana kupinga udhalimu utasema wanafadhiliwa na nani? Ndo maana CDM inapendekeza sera za majimbo....mficha maradhi kifo.......muungano usiwe biased km kweli ziliungana nchi mbili tusiwasemee wa Zanzibari wala kuwawakilisha kwenye international issue as if hawana Rais kila siku KJ ulaya hayo ndo yanawakasirisha...na km tukijitenga ZENJ itapiga hatua kubwa sana angalia visiwa vyote utagundua
 
ili kauli yako iheshimike.ni lazima tuadress mapungufu ya muungano.nionavyo muungano unahitaji mambo mawili ya kupigiwa kura ya maoni.serikali moja vs serikali tatu.
 
Back
Top Bottom