Vurugu Zanzibar, makanisa yachomwa moto!

Nadhani sasa wametupa ishara kwamba kinachotakiwa si kuvunja Muungano tu lakini pia wana mahitaji zaidi ya hilo la muungano. Kwahara haraka ni kwamba hata wakristo wahahitajiki Zanzibar na ndio maana makanisa yao yamechomwa moto. Makinisa ni majengo tu hivyo sidhani kama yenyewe tu bila wale wanao yatumia yanatatizo, tatizo ni watumiaji na ili message iwafikie wahusika basi ilibidi yachomwe moto. Hii inanikumbusha usemi aliowahi kusema baba wa taifa kuwa dhambi ya ubaguzi kwa kawaida haina mwisho. Leo wanasema sisi wanzanzibar wao wabara. Lakini kesho watenda kipengele kingine ambacho tayari wameshakionesha nacho ni wao wakristo sie waislam. Kesho kutwa watasema wao wa answar suna na sie wa shia. Mtondo watasema sie wa unguja wao wa pemba. Mtondogoo watasema sie ni wenye uwezo wao maskini na kuendelea na kuendelea kiasi kwamba utakuta si wamoja tena na nivurugu vurugu tupu. Si semi kuwa lazima waukubali Muungano ila sikuona mantiki ya kuunganisha kudai kukataa muungano na kuchoma makanisa ya wakristo. Wakristo ni wachache sana lakini nguvu yao ni kubwa mno waomaji wa biblia wanajua, ni vile tu ni wavumilivu na ni watu wa kusamehe na kusahau, lakini pia hufundishwa kuwapenda wale wanaowachukia. Kwa mantiki hiyo wasidharauliwe kwa uchache wao. Muungano = Uchomaji wa makanisa. Hili halitakaa likakubalika
 
Nakuunga mkono kaka, Kwa nini tuwapende watu wasiotupenda?. Wanatuita makafir, wanataka watanganyika waondoke kwao, wanachoma makanisa, magari na pia kuna ndugu yangu yupo kule anasema akienda dukani kitu anachohitaji anaambiwa hakuna wanamgundua kwa lafudhi yake ya bara, ila kuna rafiki zake pale akiwapa hela waeende kumnunulia chochote anachohitaji hapo dukani -Anauziwa. Mimi nimemshauri arudi Bara na nimeanza kuwachukia mno.

Usiogope kuitwa Kafir! Anayekuita hivyo ni mwanadamu wala si Mungu! Mungu aliyekuumba anajua kuwa wewe si Kafir! Achana na wasiojua wanachokifanya, wanaficha udini mgongoni mwa Muungano! Sijasikia dini ikiunganisha Taifa! Kama ingekuwa hivyo Somalia na nchi nyingine za Kiarabu wasingeendelea kuchinjana!
 
contradiction tupu!
makanisa yalikuwepo kabla ya muungano, vipi muungano ukivunjika makanisa yarudi bara? kwani yalitoka bara? na kama yalitoka bara kabla ya muungano, hayana uhusiano na muungano.
Mimi binafsi siutaki muungano na ninaishi bara, lakini siwezi kuchoma msikiti kwa sababu hiyo.
Isitoshe quran tukufu imesema wazi kuwa hao wanaoamini katika vitabu vingine (visivyo furkani) ni watu wa kitabu ndio maana muislamu anaweza kuwaoa; sasa ukichoma makanisa yao watakuwaje watu wa kitabu? (Samahani kama nitakuwa nimekosea baadhi ya spellings)

makanisa ninayozungumzia ni haya mapya ambayo kila kukicha bara yanaanzishwa na wanataka wawe na matawi zanzibar ... muungano ukivunjika watafunga virago vyao na makanisa yao kurudi bara...

watu wa kitabu wanaozungumziwa katika Qur'an ni wale wenye kuamini mungu ni mmoja hajazaa wala hajazaliwa.. usijipe moyo mkuu weye si mmoja wa watu wa kitabu...
 
Waliofanya ujinga huu leo wanadhani wameanzisha kitu chema sana, LAKINI NATAKA MJUE MUMEANZISHA KUCHIMBA KABURI LA KUIZIKA NCHI YENU MNAYODAI MNAIPENDA SANA! JIANDAENI KUZIKWA NAYO
 
Nimeshawishika kusema kweli Dr Shein hakupaswa kuwa rais wa Zanzibar na sababu moja hakuwa kiongozi wa maana (legacy) akiwa makamu wa rais JMT na pili hakuwa na agenda ya kumpeleka ikulu ukiacha debe la CCM kushawishi apewe. Sasa yanayotokea Znb ni aibu na kanyamaza kimya hajui afanye nini, hii ni utendaji mbovu usioweza kuona mawazo na matenda maovu yanayo hamasishwa na wanaharakati wa uamusho haramu
 
Ndio maana mi napata kaz kuamini kama uislamu ni din ambayo inayomuabudu MUNGU huyu wa huruma,mwenye kusamehe na sifa zingine nzuri alizonazo.Matendo yenu yanadhihilisha uwepo wa shetani mioyoni mwenu na ndiyo maana kila anayeelimika miongoni mwenu anakana kuwa mfuasi wa dini hii.UISLAMU NI DINI NZURI ILA MAZIMWI,MASHETAN NA KILA AINA YA MADUDU MABAYA NDO YANAUARIBU UISLAMU.
 
kweli Duniani kuna watu na viatu!. Muungano na kanisa wapi na wapi? Kama ni Muungano si wanaweza kudai kwa njiaa ya kawaida? Kuna bwana mmoja ametuma post yake na ameuliza KAMA WAZANZIBARI WOTE NI WAISLAM! Inashangaza sana kwa jambo hilo ambalo kwa vyovyote vile limefanywa na watu wasomi sana. Tutumie busara kudai haki zetu wapendwa. Mungu hapendi fujo, ni uamsho wa nini wa kushabikia fujo?
 



1) kuchoma hayo makanisa labda ni hatua ya mwisho walio chukua baada ya kuwapa onyo "hapa mtaani hatutaki makanisa ... mtatuharibia watoto wetu " nasikia kuna mengine yamejengwa kwa kibali cha kujenga hotel wewe ulitegemea wazanzibar wachukue hatua gani ...


2) wakristo wachache wa zanzibar lazima watakuwa kwa wingi ni dhehebu moja tu..! ambalo kanisa lao ni mkunazini hawa wengine wakuja "kutoka bara wafanya kazi wa serikali au wafanya biashara" watafute jinsi ya kujichanganya au wasali majumbani mwao...

nilitembelea china zhejiang provence kuna mji unaitwa hangzhou .. mji mzima una msikiti mmoja na makanisa mawili.. kanisa moja la wachina " wanajijua wenyewe ni dhehebu gani waliowengi"... jengine ni la foreigners ...! so hapo haijalishi we ni dhehebu gani huko ulipotoka .. hakuna ruhusu ya kuanzisha nyumba nyingine ya ibada . ule msikiti mmoja wa waislam haijalishi muislam wa dhehebu gani wote wana pray pamoja ... hutaki sali nyumbani


pombe ni chanzo cha maovu yote ... ubakaji etcl.... kuchomwa bar sawa tu sababu ni tofauti na mila na desturi za wa zanznibar ambao mila na desturi zao zimeegemea kwenye dini..!

kuchomwa nyumba za watanganyika sijasikia na siungi mkono...

Ikumbukwe kuwa kabla ya uisalamu kuingia Zanzibar kuliwa na dini za wenyeji. Fikiria kama wangekuwa na mentality kama hii unayoisema ya kuchoma nyumba za ibada husani misikiti ingekuwa sawa? kile unachosema kuharibu watoto, ni kuharibu au ni hiari ya mtu kuchagua? Hivi Mungu analazimisha watu kuchagua? Tunamtetea Mungu au Mungu anastahili kujijtetea? Katika dunia hii tunahitajiana na tunahitaji tolerance kwa wote.
 
Well said mdada! Huyu mzee toka awe Makamu hapa alikuwa boya boya tu! Siasa za Zanzibar hawezi kabisa asipoangalia watampindua
 
Najaribu kufikiria ,kutafiti chanzo cha wana-uamsho kudai Zanzibar huru, sijapata majibu. Kuna nini kinachowakera mpaka watake kujitenga. Hivi nini sababu ya msingi kabisa ya kilio chao.

BODACHOGO unapoteza muda wako kutafakari! huwezi kupata sababu yoyote zaidi ya ndoto za kudhani watafanikiwa sana bila muungano! Wanasahau kuwa siri ya mafanikio ni kazi kwa bidii sio misaada na bla bla!
 
anaogopa akikomaa na uamsho , suk itakwenda na maji maana ninavyoona mimi ndani ya suk kuna wawakilishi/mawaziri wanaounga mkono agenda za uamsho...!
 
Wadau, mnisamehe bure kwa hili.
Nashawishika kusema kuwa Ally Kombo ndiye Malaria Sugu!
 
Hii ni aibu kwa taifa linalofuata misingi ya sheria kuruhusu wahuni kutumia mwanya wa katiba kuhatarisha amani. Wazanzibari tunao huku Tanganyika wakifanya biashara na kutumia rasilimali zetu wala hatugombani. Tunayo haki ya kumtaka Shein achukue hatua au JMT kupitia JWTZ ichukue hatua maramoja kukomesha uhuni huu
 
Wazanzibari wanaoijua nchi yao walimtaka Bilal kama Rais wao na nyie watanganyika mkamtaka Shein kwani mlidhani ni mtu rahisi kufuata matakwa yenu na sasa mnavuna mlichopanda kwani laiti Bilal angekuwa Rais wa Zanzibar leo hao mamluki wa waarabu wanaotaka kutawala hapo visiwani kwa kupitia mlango wa nyuma wasingekuwa na nafasi!! Kazi mnayo na ndio hiyo vurugu zimeanza na Shein anawaangalia tu!!!
 
Kuhusu vurugu hizi wengi wanasingizia udini,hili ni moja tu yapo matatizo mengi zaidi ambayo hamyasemi mmekuwa wanasiasa sana tena wa upande mmoja.Hakuna mwenye ushahidi kila mtu anakurupuka na ukweli unafahamika.

Ukipenda nyama ya utumbo usiogope nzi! Kinachoonekena wazi ni kuchoma kanisa na halina uhusiano na muungano! Ningeelewa kama Bara ingekuwa ni nchi ya ukiristo na kwenu ni nchi ya kiislamu! Kuchoma kanisa katika mazingira kama hayo kungepeleka salamu nzuri Bara!
 
Shein anafaa sana ndio maana sasa hivi vurugu zimekwisha! Hangera Shein!
kuwa na utulivu wa muda siyo suluhisho lazima wahusika wapelekwe mahakamani wajibu mashitaka, baada ya siku chache wakiona kimya hiki cha rais watarudi na madhara makubwa. Hii siyo siasa ni uhaini
 
Back
Top Bottom