Umeniwahi kuleta hii mada, nilienda vunja bei sinza. Haya ndio niliyaona;
- Nilichat na hao vunja bei whatsapp, nikawauliza nikichukua kuanzia piece 10 mtaniuziaje, wakasema 18000, nilivyoenda dukani kwao sinza wakakaza kuwa watauza bei ya mwisho 22000, nilishangaa sana.
- Jamaa anayekaa counter(anayepokea pesa) hana customer care nzuri, ipo hivii hata kama mteja anauliza swali mara mbili mbili unachopaswa ni kumjibu tu na sio kuonyesha umemdharau.
- wameanza tabia ya ukiwa hujulikani(sio star) wewe tegemea kupuuziwapuuziwa tu, ila akija mbongo fleva utaona hizo shobo za kufa na mtu
Niwakumbushe, hao wabongo fleva wapo wachache hawawezi kununua nguo duka zima, ila sisi ambao hatujulikani sio ma-star ndio tupo wengi na tunaoweza kununua nguo kwa wingi. Mastar wanatumika kutuleta sisi hapo, yaani nikiona diamond katupia jeans au tshirt na kasema kanunua vunja bei basi ndio anatuvuta sisi followers wake wengi tuje hapo, so tubahitaj pia kuwa respected.
JIREKEBISHENI HAPO