Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,103
- 128,723
Wanabodi
Kama kawaida yangu, mimi Mzee wa Masauti, The Voices From Within, nimeisikia sauti, imenieleza, japo hapo mwanzo, alitetea nguvu iliyotumika ni nguvu stahiki, kwa waandamaji wahuni na wahalifu waliokuwa wanataka kumpidua, lakini baada ya kubaini ukweli kuwa sio wote waliouliwa ni wahuni, waandamanaji wahalifu, kuna wengine waliuwawa kwa makosa kwa kupigwa risasi za moto, hawakuwa waandamanaji, wala hawakuuliwa kwenye maandamano, hivyo sasa hata yeye ni binadamu kama binadamu wengine, ana feelings, ana utu, ana moyo, kama nilivyomuelezea sifa zake HAPA
Na yeye sasa ameguswa, ameumia, amejutia na ameomba msamaha kiaina, not expressly kwa kusema samahani, but impliedly kwa kutumia maneno ya faraja ambayo ni apologetic ya neno "Tumeondokewa na wapendwa wetu", ambo hii inaonyesha ameguswa ameumia sasa waliokufa sio wote ni wahalifu bali ni wapendwa wetu.
Kwanza anzia hapa Live Rais Samia: Salaam za Mwaka Mpya
Kisha Mkuu Waufukwe Waufukweni anadadavua
Kiafrika, Baba ni kichwa cha nyumba, ni ishara ya strength kwenye familia, hata akifanya makosa ya wazi kwa mke, watoto au familia, hawezi kuimba msamaha wa wazi, kuomba msamaha kwa mwanaume ni dalili ya weakness, hivyo unakomaa.
Mfano mzuri ni lile kosa la kawaida la sisi wababa wa Kiafrika kupenda kula kula ovyo haswa vyakula vya hotelini, hata kama chakula cha nyumbani kipo!, mi mwenyewe enzi zangu za ujana, nakiri kupiga misosi sana, nilikuwa napenda sana kula kula vyakula mbalimbali Uliwahi kula vyakula gani kutoka sehemu mbalimbali Duniani ukafaidi?
Wale wababa wacheza mpira, badala ya kupiga mashuti golini, wao wanapenda kupiga mipira ya kona, na badala ya kufurahia mechi za uwanja wa nyumbani, wao wanapenda sana mechi za ugenini,
Kunapotokea magoli ya kucheza rafu au offside tricks, yamekataliwa, mababa huwa hawakubali kuwa wamecheza faulo, au rafu, wanakomaa, kamwe hawaombi msamaha, na kiukweli hawa wamama zetu wa kisasa, huwa wanakasirila sana, hivyo wanawabania, matokeo ni baba hataomba msamaha expressly kusema samahani, hawezi kuomba radhi bali utaona tuu baba amekuwa mdogo kama piriton, with apologetic actions!, kwanza atakuwa anarudi nyumbani mapema na vizawadi zawadi, mara kanga, mara kitenge, perfume, outing, shopping , malovidovi mengi, hivyo mama anabana anabana mwisho anaachia bila kuombwa msamaha rasmi, yanakwisha na maisha yanaendelea.
Sasa kwa kilichotokea ile October 29, kwanza waliotwa wahalifu wahuni, kisha wakashitakiwa kwa uhaini, kisha nguvu iliyotumika kuwadhibiti kwa kutumia risasi za moto, ikatetewa ni nguvu stahiki, lakini sasa imetolewa pole na waliokufa kuitwa wapendwa wetu.
Post ya mkuu wa nchi, ni post ya kiume, hata ikishikwa na mwanamke , mama akiwa ni mkuu wa nchi, anabadilika ana behave ki baba baba, hivyo na yeye hata ukifanya makosa, hawezi kuomba msamaha. Je Wajua Japo Baba ni Kichwa cha Nyumba, Mama Anaweza Kugeuka Kichwa Akawa Baba? Wajua Rais Samia ni Kichwa kama Baba?.
Hivyo hii the voices from within, imeniambia kuwa hata yeye ni binadamu mwenye moyo wa nyama, na utu, hivyo pia ameumizwa na vifo viliyotokea kimakosa ndio maana sasa anawaita wapendwa.
Sijui kwa wenzetu Waislamu, ila kwa sisi Wakrsto, kwenye sala zetu, zina sehemu 4, AUSO, Abudu, Ungama, Shukuru, Omba, Hivyo kwenye sala zetu lazima kwanza kuomba msamaha kwa makosa yetu, na kuwasamehe waliotukosea,
"Utusamehe dhambi zetu kama na sisi tunavyo wasamehe waliotukosea"
Usipo samehe sala zako ni bure
Asema Bwana kwenye Isaya 1:18-19
"Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi"
Na kwa Waislamu kuna samehe saba mara sabini.
Hakuna dhambi isiyo sameheka!.
Hivyo nawaomba Watanzania wenzangu,tumsamehe,yaliyopita sii ndwele, tugange yaliyopo na yajayo kama nilivyo shauri hapa Kwaheri 2025, Ulikuwa Mwaka wa Majanga!. Yaliyopita si Ndwele, Tugange Yajayo!. Karibu 2026, Uwe Mwaka wa Kheri!. Ni Mwaka wa Katiba Mpya!, Inakuja..!
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali
Kama kawaida yangu, mimi Mzee wa Masauti, The Voices From Within, nimeisikia sauti, imenieleza, japo hapo mwanzo, alitetea nguvu iliyotumika ni nguvu stahiki, kwa waandamaji wahuni na wahalifu waliokuwa wanataka kumpidua, lakini baada ya kubaini ukweli kuwa sio wote waliouliwa ni wahuni, waandamanaji wahalifu, kuna wengine waliuwawa kwa makosa kwa kupigwa risasi za moto, hawakuwa waandamanaji, wala hawakuuliwa kwenye maandamano, hivyo sasa hata yeye ni binadamu kama binadamu wengine, ana feelings, ana utu, ana moyo, kama nilivyomuelezea sifa zake HAPA
Na yeye sasa ameguswa, ameumia, amejutia na ameomba msamaha kiaina, not expressly kwa kusema samahani, but impliedly kwa kutumia maneno ya faraja ambayo ni apologetic ya neno "Tumeondokewa na wapendwa wetu", ambo hii inaonyesha ameguswa ameumia sasa waliokufa sio wote ni wahalifu bali ni wapendwa wetu.
Kwanza anzia hapa Live Rais Samia: Salaam za Mwaka Mpya
Kisha Mkuu Waufukwe Waufukweni anadadavua
Kwenye kusoma maandishi kuna watu wanauwezo wa to read in between the lines, na Kwenye kusikiliza, to listen in between the words, ni wenye uwezo huu pekee ndio watakubaliana na mimi, huu ni msamaha, lakini walio wengi humu, ndio hivyo tena, hawawezi kunielewa.Samia Suluhu Hassan, katika salamu za mwaka mpya 2026 amesema "Tumeondokewa na wapendwa wetu, tuendelee kuwaombea"
Kiafrika, Baba ni kichwa cha nyumba, ni ishara ya strength kwenye familia, hata akifanya makosa ya wazi kwa mke, watoto au familia, hawezi kuimba msamaha wa wazi, kuomba msamaha kwa mwanaume ni dalili ya weakness, hivyo unakomaa.
Mfano mzuri ni lile kosa la kawaida la sisi wababa wa Kiafrika kupenda kula kula ovyo haswa vyakula vya hotelini, hata kama chakula cha nyumbani kipo!, mi mwenyewe enzi zangu za ujana, nakiri kupiga misosi sana, nilikuwa napenda sana kula kula vyakula mbalimbali Uliwahi kula vyakula gani kutoka sehemu mbalimbali Duniani ukafaidi?
Wale wababa wacheza mpira, badala ya kupiga mashuti golini, wao wanapenda kupiga mipira ya kona, na badala ya kufurahia mechi za uwanja wa nyumbani, wao wanapenda sana mechi za ugenini,
Kunapotokea magoli ya kucheza rafu au offside tricks, yamekataliwa, mababa huwa hawakubali kuwa wamecheza faulo, au rafu, wanakomaa, kamwe hawaombi msamaha, na kiukweli hawa wamama zetu wa kisasa, huwa wanakasirila sana, hivyo wanawabania, matokeo ni baba hataomba msamaha expressly kusema samahani, hawezi kuomba radhi bali utaona tuu baba amekuwa mdogo kama piriton, with apologetic actions!, kwanza atakuwa anarudi nyumbani mapema na vizawadi zawadi, mara kanga, mara kitenge, perfume, outing, shopping , malovidovi mengi, hivyo mama anabana anabana mwisho anaachia bila kuombwa msamaha rasmi, yanakwisha na maisha yanaendelea.
Sasa kwa kilichotokea ile October 29, kwanza waliotwa wahalifu wahuni, kisha wakashitakiwa kwa uhaini, kisha nguvu iliyotumika kuwadhibiti kwa kutumia risasi za moto, ikatetewa ni nguvu stahiki, lakini sasa imetolewa pole na waliokufa kuitwa wapendwa wetu.
Post ya mkuu wa nchi, ni post ya kiume, hata ikishikwa na mwanamke , mama akiwa ni mkuu wa nchi, anabadilika ana behave ki baba baba, hivyo na yeye hata ukifanya makosa, hawezi kuomba msamaha. Je Wajua Japo Baba ni Kichwa cha Nyumba, Mama Anaweza Kugeuka Kichwa Akawa Baba? Wajua Rais Samia ni Kichwa kama Baba?.
Hivyo hii the voices from within, imeniambia kuwa hata yeye ni binadamu mwenye moyo wa nyama, na utu, hivyo pia ameumizwa na vifo viliyotokea kimakosa ndio maana sasa anawaita wapendwa.
Sijui kwa wenzetu Waislamu, ila kwa sisi Wakrsto, kwenye sala zetu, zina sehemu 4, AUSO, Abudu, Ungama, Shukuru, Omba, Hivyo kwenye sala zetu lazima kwanza kuomba msamaha kwa makosa yetu, na kuwasamehe waliotukosea,
"Utusamehe dhambi zetu kama na sisi tunavyo wasamehe waliotukosea"
Usipo samehe sala zako ni bure
Asema Bwana kwenye Isaya 1:18-19
"Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi"
Na kwa Waislamu kuna samehe saba mara sabini.
Hakuna dhambi isiyo sameheka!.
Hivyo nawaomba Watanzania wenzangu,tumsamehe,yaliyopita sii ndwele, tugange yaliyopo na yajayo kama nilivyo shauri hapa Kwaheri 2025, Ulikuwa Mwaka wa Majanga!. Yaliyopita si Ndwele, Tugange Yajayo!. Karibu 2026, Uwe Mwaka wa Kheri!. Ni Mwaka wa Katiba Mpya!, Inakuja..!
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali