Vodacom washusha bei kuongea sasa sh 1 kwa sekunde

Lukwangule

Senior Member
May 25, 2009
157
2
Vodacom Tanzania katika kushawishi matumizi zaidi ya simu za mkononi imeshusha bei ya upigaji simu ambapo sasa wateja wa Voda kwa Voda watapiga simu shilingi moja kwa sekunde.
Kwa hesabu za haraka haraka punguzo hilo ni zaidi ya asilimia 200 na wenyewe wanasema litatengeneza hasara lakini watafurahi kama watanzania wengi wataingia katika mtandao.
Akitangaza biashara hiyo mpya ambayo haihitaji kujisaili inayotarajia kuanza leo saa sita mchana, katika chumba cha habari cha magazeti ya serikali ya Daily News na HabariLeo,Ephraim mafuru ambaye ni Mkurugenzi wa Matangazo alisema ni lengo kufungua zaidi matumizi ya simu ambayo ni muhimu kwa maendeleo hasa vijijini.
Mafuru ambaye aliambatana katika safari ya kuzindua huduma hiyo na Mkurugenzi wa mahusiano ya jamii mwamvita makamba alisema hasara hiyo itafidiwa na hudjma nyingine za Vodacom ambazo zote zimelenga kuwa karibu na watanzania.
Huduma nyingine ni kama za fedha, intaneti na pia za ATM.
Ikiwa na wateja milioni saba na zaidi katika soko lenye jumla ya wateja milioni 13,Vodacom wanasema kwamba wanatoa nafasi zaidi kwa watu kuanza kutumia simu za mkononi kwa maendeleo yao.
Huduma hiyo itawezesha wateja zaidi ya milioni saba wa kampuni hiyo kunufaika na huduma hiyo ambayo itakuwa endelevu .
Mwamvita naye alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaongeza mabadiliko kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo imewekeza kwa miaka 10 nchini, hivyo kwa kipindi hiki ambacho ni cha Mapinduzi ni wakati muafaka kwa vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakulima, wanafunzi, wafanyakazi kuendelea kutumia mtandao huo na kufaidika na huduma zake.
Licha ya kuanza huduma hiyo kampuni hiyo itaendelea kutoa promosheni zake za “Cheka Time na Voda Jamaa”.
Kuhusu huduma za mkongo wa mawasiliano, alisema
 
Vodacom Tanzania katika kushawishi matumizi zaidi ya simu za mkononi imeshusha bei ya upigaji simu ambapo sasa wateja wa Voda kwa Voda watapiga simu shilingi moja kwa sekunde.
Kwa hesabu za haraka haraka punguzo hilo ni zaidi ya asilimia 200 na wenyewe wanasema litatengeneza hasara lakini watafurahi kama watanzania wengi wataingia katika mtandao.
Akitangaza biashara hiyo mpya ambayo haihitaji kujisaili inayotarajia kuanza leo saa sita mchana, katika chumba cha habari cha magazeti ya serikali ya Daily News na HabariLeo,Ephraim mafuru ambaye ni Mkurugenzi wa Matangazo alisema ni lengo kufungua zaidi matumizi ya simu ambayo ni muhimu kwa maendeleo hasa vijijini.
Mafuru ambaye aliambatana katika safari ya kuzindua huduma hiyo na Mkurugenzi wa mahusiano ya jamii mwamvita makamba alisema hasara hiyo itafidiwa na hudjma nyingine za Vodacom ambazo zote zimelenga kuwa karibu na watanzania.
Huduma nyingine ni kama za fedha, intaneti na pia za ATM.
Ikiwa na wateja milioni saba na zaidi katika soko lenye jumla ya wateja milioni 13,Vodacom wanasema kwamba wanatoa nafasi zaidi kwa watu kuanza kutumia simu za mkononi kwa maendeleo yao.
Huduma hiyo itawezesha wateja zaidi ya milioni saba wa kampuni hiyo kunufaika na huduma hiyo ambayo itakuwa endelevu .
Mwamvita naye alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaongeza mabadiliko kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo imewekeza kwa miaka 10 nchini, hivyo kwa kipindi hiki ambacho ni cha Mapinduzi ni wakati muafaka kwa vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakulima, wanafunzi, wafanyakazi kuendelea kutumia mtandao huo na kufaidika na huduma zake.
Licha ya kuanza huduma hiyo kampuni hiyo itaendelea kutoa promosheni zake za “Cheka Time na Voda Jamaa”.
Kuhusu huduma za mkongo wa mawasiliano, alisema
 
vodacom tanzania katika kushawishi matumizi zaidi ya simu za mkononi imeshusha bei ya upigaji simu ambapo sasa wateja wa voda kwa voda watapiga simu shilingi moja kwa sekunde.
kwa hesabu za haraka haraka punguzo hilo ni zaidi ya asilimia 200 na wenyewe wanasema litatengeneza hasara lakini watafurahi kama watanzania wengi wataingia katika mtandao.
akitangaza biashara hiyo mpya ambayo haihitaji kujisaili inayotarajia kuanza leo saa sita mchana, katika chumba cha habari cha magazeti ya serikali ya daily news na habarileo,ephraim mafuru ambaye ni mkurugenzi wa matangazo alisema ni lengo kufungua zaidi matumizi ya simu ambayo ni muhimu kwa maendeleo hasa vijijini.
Mafuru ambaye aliambatana katika safari ya kuzindua huduma hiyo na mkurugenzi wa mahusiano ya jamii mwamvita makamba alisema hasara hiyo itafidiwa na hudjma nyingine za vodacom ambazo zote zimelenga kuwa karibu na watanzania.
Huduma nyingine ni kama za fedha, intaneti na pia za atm.
Ikiwa na wateja milioni saba na zaidi katika soko lenye jumla ya wateja milioni 13,vodacom wanasema kwamba wanatoa nafasi zaidi kwa watu kuanza kutumia simu za mkononi kwa maendeleo yao.
Huduma hiyo itawezesha wateja zaidi ya milioni saba wa kampuni hiyo kunufaika na huduma hiyo ambayo itakuwa endelevu .
Mwamvita naye alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaongeza mabadiliko kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo imewekeza kwa miaka 10 nchini, hivyo kwa kipindi hiki ambacho ni cha mapinduzi ni wakati muafaka kwa vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakulima, wanafunzi, wafanyakazi kuendelea kutumia mtandao huo na kufaidika na huduma zake.
Licha ya kuanza huduma hiyo kampuni hiyo itaendelea kutoa promosheni zake za “cheka time na voda jamaa”.
Kuhusu huduma za mkongo wa mawasiliano, alisema


hivi kweli rostam anawapenda sana wa tz kiasi cha kukubali hasara ili wabongo wafaidi mawasiliano ya bei nafuu??
 
Yesu ni Bwana!..HALELUYA!
Bwana ameona unyonge wa mjakazi wake!
Asante TIGO kwa kuonyesha njia ya ukombozi!...
 
duuu 200%.....balaaa ila itasaidiaa kuleta maendeleeooo.....hasa vijijiniii
 
Mi Voda nilisha sahau hawa wezi sana wanawanyonya sana wabishi wasio elimika.
 
Ndo fanida ya soko huria kama ni kweli, Vodacom walikuwa hawana ujanja zaidi ya ku lower tarrif zao. Asilimia kubwa ya watumiaji wa simu mijini walishaikimbia Voda ukiacha corporate customers.

Thanks to tiGO and Zantel kwa ku lead market kwa lower tarrifs!!

Na bado..........naamini tiGO watakuja na tarrif ya centi 30 kwa sekunde, ndopo hapo makaburu wa Vodacom na Zain watakapo restructure kampuni zao na kuwa force kuwa price competitive kama wenzao wa tiGO na Zantel!!
 
hivi kweli rostam anawapenda sana wa tz kiasi cha kukubali hasara ili wabongo wafaidi mawasiliano ya bei nafuu??

Mkuu akukumbuke we nani??? Vodacom wamelazimika ku lower tarrif kutokana na mapato yao kuanza kudorora!

Mpaka mafisadi wanatumia tiGo na Zantel siku hizi!!

Mkuu ila RA alishauza share zake pale Vodacom......baada ya wadau kuanza 'majungu'!!
 
Mkuu akukumbuke we nani??? Vodacom wamelazimika ku lower tarrif kutokana na mapato yao kuanza kudorora!

Mpaka mafisadi wanatumia tiGo na Zantel siku hizi!!

Mkuu ila RA alishauza share zake pale Vodacom......baada ya wadau kuanza 'majungu'!!

Kimsingi Voda walikuwa hawana ujanja wa kuendelea kung'ang'ania kutoza wateja wao gharama za juu ilhali wateja wanaukimbia mtandao wao. Wateja sasa wanajaa Tigo na Zantel. Zamani Voda na Zain ndio waliokuwa na coverage kubwa mikoani, lakini kwa sasa hata makampuni mengine nayo yamejitanua sana mpaka vijijini. Ndo hapa kichwa kilipowauma watu wa Voda.
 
Watupe basi na kale Ka- Tuzo millionea .................Mbona hakatulengi sisi.................
 
Kwa mwendo huu kuna baadhi ya kampuni zitakufa. Fair competition commission inabidi wakae chonjo!
 
Waache kujishaua hapa. Eti watapata hasara!

Does it mean Tigo were running at loss with their 1 sh per sec service that started long tym ago?

To hell with their profit or whatever they say.

Kampuni za simu wanatunyonya sana. Si tu watumiaji hata workers wana-deserve to be payed better if u look at what they (companies) earn.

Shame on them makaburu!
 
Kwa mwendo huu kuna baadhi ya kampuni zitakufa. Fair competition commission inabidi wakae chonjo!

Ni kweli.....Voda na Zain zinaweza kufa kwa Tanzania kwa sababu kwa zaidi ya miaka 10 wamekuwa wakipata faida kwa kucharge bei kubwa huduma zao na sio kujifunza ku manage running costs.

Muda mfupi ujao tutaanza kusikia rightsizing (kupunguza wafanyakazi) inafanyika katika makampuni haya. Ndugu zetu mlio huko mkae mkao wa maumivu anytime kuanzia sasa! Kupunguza bei kwa 200% sio mchezo..........

Ingawa wameweka mkakati wa kuwakamua watanzania kwenye huduma zao zingine ili kufidia hasara itakayotokea. Mimi hili haliniumizi sana kwa sababu walalahoi wengi hawatumii hizi additional product zao, kazi kwa middle class and above especially corporate customers!!
 
Ni kweli.....Voda na Zain zinaweza kufa kwa Tanzania kwa sababu kwa zaidi ya miaka 10 wamekuwa wakipata faida kwa kucharge bei kubwa huduma zao na sio kujifunza ku manage running costs.

Hizi kampuni kubwa tayari kwa sehemu kubwa wamesha invest vya kutosha. Hizi ndogo/mpya the likes of sasatel, hits etc ni vigumu sana kustawi kwenye environment yenye vita ya bei (price wars) au kama baadhi ya hizi kampuni kubwa/kongwe zitaamua/zimeamua kushirikiana (illegally) kupanga bei.
 
Kwa mwendo huu kuna baadhi ya kampuni zitakufa. Fair competition commission inabidi wakae chonjo!

FCC kazi yao ni kusimamia kuhakikisha kunakuwa na ushindani wa haki na si kuzuia ushindani. Shida inakuwa, iwapo makampuni ya simu yatakaa na kupanga bei za huduma zao ili kuwaumiza wateja, hapo ndipo FCC wanatakiwa kuingilia kati na kuwaadhibu. Upangaji wa bei (price fixing) kwa washindani ili kuumiza walaji ni makosa.


Ni kweli.....Voda na Zain zinaweza kufa kwa Tanzania kwa sababu kwa zaidi ya miaka 10 wamekuwa wakipata faida kwa kucharge bei kubwa huduma zao na sio kujifunza ku manage running costs.

Muda mfupi ujao tutaanza kusikia rightsizing (kupunguza wafanyakazi) inafanyika katika makampuni haya. Ndugu zetu mlio huko mkae mkao wa maumivu anytime kuanzia sasa! Kupunguza bei kwa 200% sio mchezo..........

Ingawa wameweka mkakati wa kuwakamua watanzania kwenye huduma zao zingine ili kufidia hasara itakayotokea. Mimi hili haliniumizi sana kwa sababu walalahoi wengi hawatumii hizi additional product zao, kazi kwa middle class and above especially corporate customers!!

Umegusa pabaya.
Voda na zain hawajui kutumia kidogo walichonacho kwa umakini. Njia mojawapo ya kupunguza matumizi ni kupunguza idadi ya magari yao, wana magari mengi mno pasipo sababu za msingi. Gharama za kuyahudumia magari haya hulipwa na wateja kwa kuwakamua zaidi, hivyo kuwaongezea mzigo.


Hizi kampuni kubwa tayari kwa sehemu kubwa wamesha invest vya kutosha. Hizi ndogo/mpya the likes of sasatel, hits etc ni vigumu sana kustawi kwenye environment yenye vita ya bei (price wars) au kama baadhi ya hizi kampuni kubwa/kongwe zitaamua/zimeamua kushirikiana (illegally) kupanga bei.

Kwa jinsi kampuni kubwa kubwa za simu zilivyojiimarisha kimiundombinu na kibiashara, usimamaji wa uhakika kwa Sasatel na kampuni nyingine changa ni kazi sana.
 
Ha ha ha !!! Customers wengi walishasepa kiaina na kuingilia tiGo!!! Afadhali wameshtuka mapema!!
 
Ushauri wangu wa bure jamani

wale washikaji zetu ambao wameajiriwa na hawa makaburu waanze kurusha CV haraka iwezekanavyo, kuweni karibu na magazeti hasa ze gadian la ijumaa pamoja na mitandao ya ajira manake kinachofwata hapo ni dizasta....yani hao wawekezaji hawajaja kuuza sura bongo they are here to make chapaa...

huo ndo ushauri wangu wa bure jamani,

wenu katika bwana

zionTZ
 
Back
Top Bottom