Lukwangule
Senior Member
- May 25, 2009
- 157
- 2
Vodacom Tanzania katika kushawishi matumizi zaidi ya simu za mkononi imeshusha bei ya upigaji simu ambapo sasa wateja wa Voda kwa Voda watapiga simu shilingi moja kwa sekunde.
Kwa hesabu za haraka haraka punguzo hilo ni zaidi ya asilimia 200 na wenyewe wanasema litatengeneza hasara lakini watafurahi kama watanzania wengi wataingia katika mtandao.
Akitangaza biashara hiyo mpya ambayo haihitaji kujisaili inayotarajia kuanza leo saa sita mchana, katika chumba cha habari cha magazeti ya serikali ya Daily News na HabariLeo,Ephraim mafuru ambaye ni Mkurugenzi wa Matangazo alisema ni lengo kufungua zaidi matumizi ya simu ambayo ni muhimu kwa maendeleo hasa vijijini.
Mafuru ambaye aliambatana katika safari ya kuzindua huduma hiyo na Mkurugenzi wa mahusiano ya jamii mwamvita makamba alisema hasara hiyo itafidiwa na hudjma nyingine za Vodacom ambazo zote zimelenga kuwa karibu na watanzania.
Huduma nyingine ni kama za fedha, intaneti na pia za ATM.
Ikiwa na wateja milioni saba na zaidi katika soko lenye jumla ya wateja milioni 13,Vodacom wanasema kwamba wanatoa nafasi zaidi kwa watu kuanza kutumia simu za mkononi kwa maendeleo yao.
Huduma hiyo itawezesha wateja zaidi ya milioni saba wa kampuni hiyo kunufaika na huduma hiyo ambayo itakuwa endelevu .
Mwamvita naye alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaongeza mabadiliko kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo imewekeza kwa miaka 10 nchini, hivyo kwa kipindi hiki ambacho ni cha Mapinduzi ni wakati muafaka kwa vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakulima, wanafunzi, wafanyakazi kuendelea kutumia mtandao huo na kufaidika na huduma zake.
Licha ya kuanza huduma hiyo kampuni hiyo itaendelea kutoa promosheni zake za Cheka Time na Voda Jamaa.
Kuhusu huduma za mkongo wa mawasiliano, alisema
Kwa hesabu za haraka haraka punguzo hilo ni zaidi ya asilimia 200 na wenyewe wanasema litatengeneza hasara lakini watafurahi kama watanzania wengi wataingia katika mtandao.
Akitangaza biashara hiyo mpya ambayo haihitaji kujisaili inayotarajia kuanza leo saa sita mchana, katika chumba cha habari cha magazeti ya serikali ya Daily News na HabariLeo,Ephraim mafuru ambaye ni Mkurugenzi wa Matangazo alisema ni lengo kufungua zaidi matumizi ya simu ambayo ni muhimu kwa maendeleo hasa vijijini.
Mafuru ambaye aliambatana katika safari ya kuzindua huduma hiyo na Mkurugenzi wa mahusiano ya jamii mwamvita makamba alisema hasara hiyo itafidiwa na hudjma nyingine za Vodacom ambazo zote zimelenga kuwa karibu na watanzania.
Huduma nyingine ni kama za fedha, intaneti na pia za ATM.
Ikiwa na wateja milioni saba na zaidi katika soko lenye jumla ya wateja milioni 13,Vodacom wanasema kwamba wanatoa nafasi zaidi kwa watu kuanza kutumia simu za mkononi kwa maendeleo yao.
Huduma hiyo itawezesha wateja zaidi ya milioni saba wa kampuni hiyo kunufaika na huduma hiyo ambayo itakuwa endelevu .
Mwamvita naye alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaongeza mabadiliko kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo imewekeza kwa miaka 10 nchini, hivyo kwa kipindi hiki ambacho ni cha Mapinduzi ni wakati muafaka kwa vikundi mbalimbali vya uzalishaji mali, wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakulima, wanafunzi, wafanyakazi kuendelea kutumia mtandao huo na kufaidika na huduma zake.
Licha ya kuanza huduma hiyo kampuni hiyo itaendelea kutoa promosheni zake za Cheka Time na Voda Jamaa.
Kuhusu huduma za mkongo wa mawasiliano, alisema