Vodacom leo mtamjua mteja mwenye hasira

Vodacom leo mtamjua mteja mwenye hasira

Mkuu jukwaa la Hoja na Habari Mchanganyiko nenda juu kabisa wana thread yao.
 
UPDATES
Mama tumewasiliana muda si mrefu anasema wamemtumia msg kuwa ameondolewa kwenye huduma fulani fulani ambazo hazijui na hakuwahi kuomba.
Hii ilikuwa ni baada ya mimi kumtumia msg ya kumwuliza kama hawa jamaa hawajawasiliana naye kuhusu kumaliza hili tatizo.
Lakini pia tumewasiliana vizuri na Vodacom Tanzania na nasubiri utekelezaji wao kwa sababu huu moto nilitaka niuwashe bila kumwambia mama kwa sababu ningemwambia, lazima angenizuia.
 
Tanesco ndo balaa, ukiweka hela pungufu ya wanayodai,(service charge) wanakata na hawarudushi! Mfano, kama hujalipia umeme kwa miezi miwili, ni lazima uweke kiasi kisichopungua 14,000, vinginevyo kitakatwa na hutapata kitu!
 
UPDATES
Mama tumewasiliana muda si mrefu anasema wamemtumia omsg kuwa ameondolewa kwenye huduma fulani fulani ambazo hazijui na hakuwahi kuomba.
Hii ilikuwa ni baada ya mimi kumtumia msg ya kumwuliza kama hawa jamaa hawajawasiliana naye kuhusu kumaliza hili tatizo.
Lakini pia tumewasiliana vizuri na Vodacom Tanzania na nasubiri utekelezaji wao kwa sababu huu moto nilitaka niuwashe bila kumwambia mama kwa sababu ningemwambia, lazima angenizuia.

Mkuu asante kwa mrejesho, m nimewapigia wameniambia nisubir mpaka masaa 3 nadhan n wakati muafaka wa kuondoa wizi,

Ngoja tusubr kwa wadau wengine
 
Me niliweka kwa mara ya kwanza vocha ya sh2000 sim ikazima hapo hapo... sijui haijazoea hiyo mizigo? Duh!
 
Tigo internet iko hovyooo...slow kama mwendo wa bi harusi...
Yani hamna cha afadhali...
Sasa huoni kwamba airtel ndio jibu.., ila tu usijiunge na ile switch on yao.., ni konokono kabisa.., jiunge na ile vocha ya 500 ya moja kwa moja..
 
Sasa huoni kwamba airtel ndio jibu.., ila tu usijiunge na ile switch on yao.., ni konokono kabisa.., jiunge na ile vocha ya 500 ya moja kwa moja..

Sawa nitahamia airtel...ila na huko wakizingua sijui ntaenda wapi?!!!
 
eli79, maelezo yako hayapishani na huh majibu niliyopata toka customer care ya Vodacom Tanzania. Lakini niliwauliza how come within 5minutes shilingi elfu tano ziishe zote na huku siko active kwenye data? Kimsingi majibu ya wahudumu wawili ambayo nimeya record yamepishana ndani ya nusu saa nilipokuwa nahoji upotevu wa pesa yangu. Huduma zao kwa sasa ni questionable!
Yeah, Mara nyingi tunapoteza pesa kwa kuwa active kwenye Data hata kama hamna bundle, tukiweka voucher tu zile underground programs ambazo hata hatuoni zikifanya kazi, mf. updates za programs, facebook inajirefresh n.k. Tena wanaotumia windows phones ndio usiseme.. Coz zile ni internet friendly kuliko hata androids.
..japo pia nadhani voda nao wanaiba kiaina. Kwenye Airtel sijawahi kuibiwa hata siku moja. Ndio maana nimekuwa nao kwa miaka bila kubadili line.
 
Last edited by a moderator:
Nishukuru tu kwangu hayo mashikolo mageni huwa hayanikuti.. Nina lain 2 za Vodacom Tanzania, moja inatumika kwenye modem na nyingine ni kwa ajili ya mawasoliano... Vocha inaweza kaa hata wiki 3 bila kupungua hata nukta!

Mara ya mwisho kujiunga na mahuduma yao ya miito na mengineyo ni mwaka 2008 enzi nikiwa o level.

Baada ya hapo sikuona umuhimu wa hizo huduma kwangu, salio nanunua kwa njia 2, kutoka m pesa ama vocha za kawaida!

Hizo shida za kukatwa katwa credit kwangu ziliisha miaka 6 iliyopita kipindi naongea bure saa sita usiku!

Over!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kama umeniona hivi.
Yaani sasa hivi nimekaa na chibuku hapa tena sasa hivi wameboresha ina nafaka nyingi kweli na inafoka povu balaa, hii haina haja ya kula manake ni lishe tosha.
Baada ya hapa, napiga ndoba kadhaa ili kusafisha mdomo halafu niwafate hawa wapuuzi mlimani city nikawaoneshe kazi.

Umetisha kamanda,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom