Vodacom leo mtamjua mteja mwenye hasira

Vodacom leo mtamjua mteja mwenye hasira

Shin Lim

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
8,327
Reaction score
15,339
Yaani siku hizi kila nikiweka hela lazima mnikate bila sababu wakati sijajiunga na huduma zenu uchuro za kutuibia pesa, hiyo haijaniuma sana.

Kilichoniuma zaidi, mmeanza kumkata mama yangu mzazi wakati hizo huduma hawezi kuzitumia kabisa, yeye ni kupiga kupokea na kutuma msg tu.
Cha ajabu sasa hivi akiweka jero tu, mnalitafuna lote hali inayomfanya akiweka aunge kifurushi cha hela yote wakati huo huo utafikiri hiyo vocha ameiiba.

Sasa nawaambia hivi, kutokana na ugumu ninaopata katika kupata hizo pesa, nawapa masaa 8 kutoka sasa muwe mmeshamaliza hilo tatizo ikiwa ni pamoja kurudisha hela mlioiba bila taarifa.
Namba yake ipo PM kwako.
Tutaheshimiana tu.
Vodacom Tanzania
 
Last edited by a moderator:
hii thread inachekesha lakn pia unahuzunisha,,,! voda wamekuwa wezi kweli. siyo wewe tu, hata mimi
 
Loh..mwenyewe nimeweka kajero, sijakaa vizuri imekatwa imebaki 471...nikaweka jero lingine nikajiunga kifurushi cha jero...baadae naangalia wamekula hadi zile chenji zangu, yani wamekomba zoote wameniachia 0..
 
mara mabreaking news mara mavichekesho nimewaomba mimi?napiga linamba lenu halieleweki maelezo Vodacom Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Ni sheeeda cheap is expensive,wanarudisha hela zao pale ulipopewa huduma bure.
 
Yaani siku hizi kila nikiweka hela lazima mnikate bila sababu wakati sijajiunga na huduma zenu uchuro za kutuibia pesa, hiyo haijaniuma sana.

Kilichoniuma zaidi, mmeanza kumkata mama yangu mzazi wakati hizo huduma hawezi kuzitumia kabisa, yeye ni kupiga kupokea na kutuma msg tu.
Cha ajabu sasa hivi akiweka jero tu, mnalitafuna lote hali inayomfanya akiweka aunge kifurushi cha hela yote wakati huo huo utafikiri hiyo vocha ameiiba.

Sasa nawaambia hivi, kutokana na ugumu ninaopata katika kupata hizo pesa, nawapa masaa 8 kutoka sasa muwe mmeshamaliza hilo tatizo ikiwa ni pamoja kurudisha hela mlioiba bila taarifa.
Namba yake ipo PM kwako.
Tutaheshimiana tu.
Vodacom Tanzania

pole sana mkuu,wamempiga maza window shopping?hawa jamaa hawana huruma hata chembe
 
Loh..mwenyewe nimeweka kajero, sijakaa vizuri imekatwa imebaki 471...nikaweka jero lingine nikajiunga kifurushi cha jero...baadae naangalia wamekula hadi zile chenji zangu, yani wamekomba zoote wameniachia 0..
Vodacom hili tatizo mnalifahanu mnafanya wizi was mchana sasa tunatangaza kuwahama rasmi coda siyo baba wala mama,tuwahame kwa bidii zote
 
Mimi hizi Hbari za Nipashe ndo zinanikela hata sijajiunga wananitumia tu
 
vihudama vya ajibu Vodacom toeni especially mnasema mteja sokoni ukiweka tu voucher ukichelewa kujiunga na kifurush within 5 minutes mmesha fyeka amount

Cc Vodacom Tanzania
 
Last edited by a moderator:
Vodacom hili tatizo mnalifahanu mnafanya wizi was mchana sasa tunatangaza kuwahama rasmi coda siyo baba wala mama,tuwahame kwa bidii zote

Hamna kwa kukimbilia...kote hovyo...labda tumbembeleze Bakhressa aanzishe mtandao wa simu...walau yule anaweza kuleta fair competition...
Wawaulize startimes na Dstv...
 
Ukija upande wa tigo nao ni wale wale tu aisee, hawa jamaa ni wehu sana
Ni tatizo. Nimesafiri kwenda mahali nikawa nimeweka kakifurushi ka-Airtel OMG mwezi mzima. Nimefika huko Airtel iko slow mbaya. Sina la kufanya imebidi niendelee na Vodacom. Ushindani kwenye hili soko si perfect.
 
Ni tatizo. Nimesafiri kwenda mahali nikawa nimeweka kakifurushi ka-Airtel OMG mwezi mzima. Nimefika huko Airtel iko slow mbaya. Sina la kufanya imebidi niendelee na Vodacom. Ushindani kwenye hili soko si perfect.

Usije ukarogwa ukanunua modem ya Zantel yaani sikuamini yaliyonikuta mkoani, wote ni hovyo kabisaaaa nilikua na reports muhimu za kutuma Ile nimefika tu nikakaa nikaanza mishe ya kukonekti, nyooooo upuuzi mtupu
 
Kuna mda unaweka vocha ili kujiunga na kifurushi lakini unashindwa, sijui ndio system inakuwa down ama vipi au ndio kakati wao wa siri?.
Mfano juzi usiku hili linikuta.niliweka vocha ya 1000 lakini kila nikitaka kujiunga na kifufushi inashindikana. Sasa kuja kuamka asubuhi salio limeshakatwa na kifurushi sijaunganishwa.
Imefikia hatua sasa hivi kila nikiweka vocha inanibidi nijiunge mda huohuo kuhofia kuibiwa na hawa wezi.
 
Voda wana mikataba mingi na kampuni ambazo wateja wake hawazijui.Mfano meseji za breking news,burudani,sokon,nk zinatolewa na kampuni hizo kupitia voda.Hivyo hata ukifungua nashtaka voda hawahusiki!Kujiunga na hizo huduma ni rahis sana kazi ipo ktk kujitoa...
 
Loh..mwenyewe nimeweka kajero, sijakaa vizuri imekatwa imebaki 471...nikaweka jero lingine nikajiunga kifurushi cha jero...baadae naangalia wamekula hadi zile chenji zangu, yani wamekomba zoote wameniachia 0..

Inawezekana hukuwa na credit, wakati huo huo data package ilikuwa active kwa hiyo ulivyoweka Tu kabla hata ya kujiunga data ikala 29sh za chap chap..yaweza kuwa sio VODA ni uelewa wako tu.
 
Walisha sema Vodacom Kazi ni kwako so hayo yoote ndio kazi mlio ambiwa...................
 
Wanakuunganisha kwenye huduma ambayo ujataka kujiunga kama nipashe habari mimi nimeiweka kapuni line yao voda jirekebisheni

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom