Vodacom kuweni makini na mitandao yenu

Koryo2

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
2,056
2,515
Asubuhi ya leo tarehe 29.1.2020 nilienda kutoa fedha kwenye kibanda cha M-Pesa. Nilifuata taratibu zote na nikaelezwa kuwa taratibu zimekamilika. Nilisubiri ili nipate ujumbe wa kutoa fedha bila mafanikio. Nilikaa pale kwa muda wa saa moja bila mafanikio na hivyo ikabidi niondoke.

Usiku huu saa 4.15 usiku tarehe 29.1.2020 ndipo nimepata ujumbe unaothibitishwa kuwa nipewe fedha nilizofanyia muamala asubuhi ya tarehe 29.1.2020. Bahati nzuri pale nilipofanyia taratibu za kutolea fedha wananifahamu.

Swali la kujiuliza, kama ningekuwa safarini mfano Sikonge halafu ninaenda Mbeya hizi fedha zangu ningezipataje?. Ninafikiria kwenda Mahakamani ili nidai haki zangu kwa kitendo mlichonifanyia leo.

Badilikeni.
 
voda ni mabwege sana, nimeweka vocha wakasema kuna tatizo la mtandao.kurudia kuweka wanasema imetumika (kwenye namba yangu) kujiunga wananambia sina salio, kuchek salio nna 0.00 vocha nimesha tupa

namba 100 huduma kwa wateja inaishia andika ending call

acheni upumbavu voda
 
Kuna customer services na customer support ulipaswa kuwapigia pale pale kabla hujaondoka... Unajua hivi vitu vinafanywa na mitambo so sometimes faults ndogo ndogo hazikosekani

Jr
 
Shida ipo maana hata Mimi hunitokea mara nyingi hasa mwezi huu. Ukicheck balance wanakata sh. 60. Nadhani wanafanya makusudi ili wafanye makato unapokuwa unataka kujua kiasi kilichomo pindi ujumbe ukichelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna customer services na customer support ulipaswa kuwapigia pale pale kabla hujaondoka... Unajua hivi vitu vinafanywa na mitambo so sometimes faults ndogo ndogo hazikosekani
Ni kweli kabisa, na hii inatokea sana kwa wenye vibanda vya kutolea pesa,
unakuta hana Flot na kazi kaipenda, atakuweka pending mpaka wamjazie pesa ktk Flot yake ndipo akutumie
na kwa vile walikuwa wanamfahamu walimsubirisha
Kilichopo ni kuwapigia Voda wenyewe kitengo cha M Pesa, au (# 7) akaunti yangu halafu M pesa, halafi (#3) Taarifa fupi, Mm yalinikuta nimetweka M Pesa nafika Mkoa mwingine natoa hakuna kitu nikamtuma jirani aende kwenye kibanda kumuuliza mhudumu akajibiwa wakati ule hakuwa na Flot
 
voda ni mabwege sana, nimeweka vocha wakasema kuna tatizo la mtandao.kurudia kuweka wanasema imetumika (kwenye namba yangu) kujiunga wananambia sina salio, kuchek salio nna 0.00 vocha nimesha tupa

namba 100 huduma kwa wateja inaishia andika ending call

acheni upumbavu voda
Kuna rafiki yangu jana kimemtokea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom