eti kwa 250 utaweza kudownload miziki,updates,habari za michezo mbalimbali kifurushi chenyewe unapewa Mb5.wakati unakuta nyimbo moja ina mb10. Wadau hii imekaaje?
Hizo 5mb hata kama simu ni ya tochi bado wanachekesha. Nikifungua Jf Photo kurasa kadhaa si kwishilia huko, ebo!
Kama unatumia opera mini unajidanganya si kweli inaisha haraka homepage facebook ni kb 22 kwangu na opera mini na kila picha kb 11. So ina maana uload picha 400 (bila kudownload) ndo itaisha
Let's just say, hainifai, na baadhi ya geeks humu!
Ninapobrowse JF mfululizo data usage naona Opera Mini original size na received size, mb kadhaa zinatoka, hapo bado blogs, na kadha wa kadha.
Mb 5 zinaishia kwenye kufungua homepage ya jf yani huu wizi tu mchana mchana..tigo walikua wanatoa Mb 25 kwa simu ila zilikua zinakata bila kudownload music sasa hivi viMb vitano si bure kabisaa..biashara bana
Hapa ishu ni kwamba, wanalipa kikubwa kuliko wanachopewa.
Naskia watu wengi wanalalamika tunauziwa bundle bei ghali ila tanzania were lucky bundle zetu ni rahisi sanaa 250 kwa 5 mb ina maana mb1 ni sh 50. Hapo ghali?
Sisi tunazidiwa speed na sio bei ya bundles hebu pitia website ya safaricom cheki bei ya bundles at&t marekani ni dola 54 unlimited kwa mwezi wakati tz ni elf 30