Viwanja vya Pembamnazi-Kigamboni vimetelekezwa

Viwanja vya Pembamnazi-Kigamboni vimetelekezwa

Salama wakuu. Moja kwa moja niende kwenye mada.
Mnamo mwaka 2016 serikali iliamua kuuza viwanja Kigamboni eneo la Pembamnazi jijini Dsm. Mpaka Leo hii tarehe 2- 3- 2022 viwanja hivyo havijahudumiwa na serikali kwa kuwekewa miundombinu ikiwemo umeme, maji na kuchongwa barabara ili watu waweze kuvifikia viwanja vyao. Huu ni mwaka wa sita sasa pamebakia kuwa ni porini. Serikali kupitia wizara ya ardhi toeni tamko rasmi kuhusu eneo la Pembamnazi maana watu wakienda wizarani kuuliza kulikoni wanapewa majibu ya ovyo yanayokatisha tamaa.

Pia watu waliuziwa viwanja hivyo bila ya kuviona. Kwa vile muuzaji ni wizara ya ardhi wananchi wakaamini hawatotapeliwa. Kumbe eneo lenyewe ni pori kubwa lisilokuwa na miundombinu yeyote. Tunaomba waziri muhusika aende kutembelea Block 1 na Block 2 ili ajionee mwenyewe utapeli waliofanyiwa wananchi. Pelekeni miundombinu watu wajenge, mji ukue na serikali ipate mapato kupitia kodi.
2020 nlienda huko kucheki viwanja bado pori sehemu na sehemu,ila kuzuri sana
 
Salama wakuu. Moja kwa moja niende kwenye mada.
Mnamo mwaka 2016 serikali iliamua kuuza viwanja Kigamboni eneo la Pembamnazi jijini Dsm. Mpaka Leo hii tarehe 2- 3- 2022 viwanja hivyo havijahudumiwa na serikali kwa kuwekewa miundombinu ikiwemo umeme, maji na kuchongwa barabara ili watu waweze kuvifikia viwanja vyao. Huu ni mwaka wa sita sasa pamebakia kuwa ni porini. Serikali kupitia wizara ya ardhi toeni tamko rasmi kuhusu eneo la Pembamnazi maana watu wakienda wizarani kuuliza kulikoni wanapewa majibu ya ovyo yanayokatisha tamaa.

Pia watu waliuziwa viwanja hivyo bila ya kuviona. Kwa vile muuzaji ni wizara ya ardhi wananchi wakaamini hawatotapeliwa. Kumbe eneo lenyewe ni pori kubwa lisilokuwa na miundombinu yeyote. Tunaomba waziri muhusika aende kutembelea Block 1 na Block 2 ili ajionee mwenyewe utapeli waliofanyiwa wananchi. Pelekeni miundombinu watu wajenge, mji ukue na serikali ipate mapato kupitia kodi.
Picha tafadhali!
 
Nilikuwa huko juzi, kiwanja kidogo cha kutosha kujenga nyumba unapata kwa laki tatu, 300k.

Tena ukitaka unalipa kwa awamu mbili.
Ni maeneo gani mkuu? Naomba mfano uwe kuanzia pale kituo cha panton
 
Yes, ni ghali au kidogo?
Katikati,si ghali Ila si kidogo..kuna mtu alinishauri niende kisemvule akasema buyuni ni mbali sn,Ila Mimi najikuta napendelea zaidi upande wa kigamboni kuliko huko aliponishauri
 
Sisi tulikodi gari na hiyo kampuni ya kuuza viwanja, tuliondoka feri saa nne na dakika 17, tulifika kwenye viwanja saatano na 32. Amlmost lisaa zima na madakika kumi hivi
Hapo no traffic jam..safari ya zaidi ya saa moja Dar es salaam si mchezo,ni mbali sn
 
Sijakuelewa mkuu, kama umemaanisha umbali mi nimenunua tuu kwaajili ya badae. Nina program ya kununua viwanja vingi, baada ya miaka mitatu patakua bei sana
Nilimaanisha kuwa usijali umbali.
 
Nilikuwa huko juzi, kiwanja kidogo cha kutosha kujenga nyumba unapata kwa laki tatu, 300k.

Tena ukitaka unalipa kwa awamu mbili.
hivi ukosawa kweli ww!!
 
Sisi vyetu havina mgogoro, vimepimwa halafu wameshirikiana na serikali za kijiji, manispaa na kila eneo

Iwe kheri juu ya hilo,Mkuu kua makini tu sababu hizo serekali za vijiji hao ndo wanaouza hvyo viwanja. Kumekua na kesi juu ya hao wanunuzi walouziwa pamoja hizo serekali za vijiji kwasababu hao wadai wamesema hilo shamba ni la urithi ambalo lina warka wake.
 
Back
Top Bottom