vamda
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 919
- 599
Salama wakuu.
Moja kwa moja niende kwenye mada.
Mnamo mwaka 2016 serikali iliamua kuuza viwanja Kigamboni eneo la Pembamnazi jijini Dsm. Mpaka Leo hii tarehe 2- 3- 2022 viwanja hivyo havijahudumiwa na serikali kwa kuwekewa miundombinu ikiwemo umeme, maji na kuchongwa barabara ili watu waweze kuvifikia viwanja vyao.
Huu ni mwaka wa sita sasa pamebakia kuwa ni porini. Serikali kupitia wizara ya ardhi toeni tamko rasmi kuhusu eneo la Pembamnazi maana watu wakienda wizarani kuuliza kulikoni wanapewa majibu ya ovyo yanayokatisha tamaa.
Pia watu waliuziwa viwanja hivyo bila ya kuviona. Kwa vile muuzaji ni wizara ya ardhi wananchi wakaamini hawatotapeliwa. Kumbe eneo lenyewe ni pori kubwa lisilokuwa na miundombinu yeyote.
Tunaomba waziri muhusika aende kutembelea Block 1 na Block 2 ili ajionee mwenyewe utapeli waliofanyiwa wananchi.
Pelekeni miundombinu watu wajenge, mji ukue na serikali ipate mapato kupitia kodi.
Moja kwa moja niende kwenye mada.
Mnamo mwaka 2016 serikali iliamua kuuza viwanja Kigamboni eneo la Pembamnazi jijini Dsm. Mpaka Leo hii tarehe 2- 3- 2022 viwanja hivyo havijahudumiwa na serikali kwa kuwekewa miundombinu ikiwemo umeme, maji na kuchongwa barabara ili watu waweze kuvifikia viwanja vyao.
Huu ni mwaka wa sita sasa pamebakia kuwa ni porini. Serikali kupitia wizara ya ardhi toeni tamko rasmi kuhusu eneo la Pembamnazi maana watu wakienda wizarani kuuliza kulikoni wanapewa majibu ya ovyo yanayokatisha tamaa.
Pia watu waliuziwa viwanja hivyo bila ya kuviona. Kwa vile muuzaji ni wizara ya ardhi wananchi wakaamini hawatotapeliwa. Kumbe eneo lenyewe ni pori kubwa lisilokuwa na miundombinu yeyote.
Tunaomba waziri muhusika aende kutembelea Block 1 na Block 2 ili ajionee mwenyewe utapeli waliofanyiwa wananchi.
Pelekeni miundombinu watu wajenge, mji ukue na serikali ipate mapato kupitia kodi.