Vituo vya mafuta Dar vyagoma!

Hapa cha muhimu ni kuwa nyuma ya serikali na Ewura tu, hawa wafanyabiashara wa mafuta naona wanataka kuwanyonya wananchi wee mpaka wabakie hawana kitu, sasa cha muhimu nikuwakomalia na hakuna kutetereka, nina hakika kabisa wananchi wote watakuwa nyuma ya serikali isitoshe wamiliki wengi wa vituo vya mafuta ni WATANZANIA WENYE ASILI YA KIASIA (KIESHIA) yes nimesema hivyo na nitasimama hapo niliposema, kama vp ondokeni tu wabakie wazalendo wenye kuwaonea huruma wazalendo wenzao ebooooooooooo!!!1
 
Wengi mnasahau kuwa wenye hisa kwenye hizi kampuni za mafuta ni hao hao waswahili wenzetu tuliowapa madaraka. Waasia kama ninavyowafahamu huwa hawana ubavu wa kutunisha misuli - ukiona wanafanya hivyo, hiyo jeuri yao inafadhiliwa. Kumbukeni michango yao mikubwa kwa CCM.
 

Kaka hivi kweli we unategemea kuwa hawa tuliowapa madaraka wanaweza wakawa wanawalinda wafanyabiashara wa mafuta?? kwani wao hawaogopi nchi itakapoingia kwenye migomo wao ndio wataonekana wabaya?? kwa hili mimi sikubaliani nalo kabsaaa ungenambia kuwa hawa tuliowapa madaraka wapo wanaofanya biashara hii ya mafuta ningekuelewa lakini si kwa hilo kaka
 
Hivi tz hatuna mtu kama tarek aziz! sadam alipowekewa vikwazo vya kiuchumi, wafanyabiashara wakapandisha bei ya vyakula, wakaombwa kushusha bei. waliokaidi tarek aliwakamata wote na kupingwa risasi hadharani.

Serikali ikague depot zote za mafuta, zitakazokutwa na mafuta wamiliki wakamatwe. Depot hizo zitaifishwe na kukabidhiwa TPDC. Vituo vyote vya mafuta vipigwe mnada maramoja. Jk asiogope hakuna kitakachoharibika, hivi huyu alienda vita vya kagera kweli? mbona haonyeshi haiba za kijeshi. Hivi hamwoni Hugo Shavez?

Kunahaja sasa serikali ichukue jukumu la kuagiza mafuta, ikumbukwe BP(T)ltd 50% share nizaserikali inaomtaji wakutosha na uwezo wa kumudu majukumu hayo. hivyo inaweza kuwa subcontracted kuagiza mafuta kwa niaba ya serikali.
 
Leo katika jiji la Dar es Salaam kulikuwa na kizaazaa cha upungufu wa Petrol katika vituo vingi vya mafuta. Wenye magari walionekana wakihaha kituo hadi kituo kutafuta mafuta. Ukosefu wa mafuta unaonekana ni hujuma kwa sababu vituo vingi vimekataa kuuza mafuta kwa sababu ya serikali (EWURA) kuanza kupanga bei ya mafuta. Je serikali itafanya nini kutunusuru sisi wenye magari ili kuepukana na adha ya ukosefu wa usafiri?
 
Mwanzoni walisema wanaomba kwanza stock yao iishe ndio washushe bei. Sasa wanadai hawana mafuta. Huu ni ubabe wa kijinga kabisa. Washughulikiwe.

Hivi Serikali ikiamua kutaifisha hivi vituo hawa jamaa si wanaweza kukimbilia mahakamani na kuibwaga serikali? Ni nini sasa kifanyike ili tuwabane kila kona na kuwaondoa kabisa kwenye hiyo biashara bila kuathiri utawala wa kisheria? Naombeni jibu!!
 

Sheria ya uhujumu uchumi ya 1984 ichukue mkondo wake hakuna jipya nchi yetu ni ya utawala wa sheria.
 
Kama serikali ilitumia sheria hii katika korosho kwa nini isitumie katika mafuta?,

 
Last edited:
Fuel shortage in Dar to end soon
CHARLES KIZIGHA
Daily News; Monday,January 12, 2009 @20:50​

FUEL shortage at various pump stations in the country might end soon, following arrival of tankers at the Dar es Salaam port. Four oil tankers are at the Dar es Salaam harbour loaded with about 80,000 tonnes of petroleum products that are expected to meet the nation’s demand for about a month.

BP and GAPCO have reportedly informed the Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) that petrol stocks were running out. Engen pump stations run out of fuel over the weekend. Several petrol filling stations in Dar es Salaam witnessed long queues of motorists over the weekend, raising fears of imminent transport crisis.

The GAPCO Chief Operating Officer, Mr Krishna Pradrai, confirmed that the company had run out of petrol stocks since last weekend and was expecting to receive new stocks later this week. He said that a vessel MT Wawasan was at the outer anchorage carrying some 10,000 tonnes of petrol which would be shared by some four or five companies.

“It is unfortunate that the tanker will get into the port by January 16 (on Friday) to discharge the products. January 16 is just an indication date. I am not sure when the vessel will berth,” he said. This means dealers of GAPCO will not get petrol until the vessel discharges fuel.

The BP Managing Director, Mr Engenlhard Kongoro, said that he was not aware of any shortage of fuel at his depot or pump stations supplied by his company, but said he would check on that.

The Managing Director of Engen, Mr Seelan Naidoo, whose pump stations in Mbezi and Mikocheni had run out of fuel, said the stocks supplied last Friday were exhausted because there was a rush at those points. “We have opened the depot this afternoon (yesterday) for trucks to draw fuel. We will make arrangements for other companies which have no stocks to get them from us,” he said.

One of the four tankers christened MT Atlantic carrying about 30,000 tonnes made up of 16,987 tonnes of diesel, 4,000 tonnes of petrol and 4,807 of jet fuel, is discharging at the Kurasini Oil Jetty (KOJ), but is said to be slow in pumping out the products. It could not be established when MT Atlantic would complete discharging, an exercise that started over the weekend.

One port official said some tankers take up to three days to discharge such cargo, because it depends on the pumping rate. Three more tankers loaded with over 50,000 tonnes of petroleum products are at the outer anchorage, waiting for their turn to berth at the KOJ.

The Director of Petroleum with Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA), Mr Sirili Massay, told the 'Daily News' that the products carried in the four tankers, about 80,000, could meet the nation’s demand for a month. EWURA’s petrol indicative prices for Dar es Salaam starting today increased from 1,147/- last week to 1,171/- while the cap one moved from 1,233/- to 1,259/- per litre.

Wholesale indicative price for petrol in Dar es Salaam last week was 1,084/- and that of diesel 1,207/- and the cap price for both was 1,165/- and 1,297/- respectively and will remain the same this week. The indicative price for diesel last week in Dar es Salaam was 1,270/-, this week it will be 1,301/- per litre and the cap price was 1,365/- and now 1,399/- for the same measure.
 
Fuel shortage in Dar to end soon
CHARLES KIZIGHA
Daily News; Monday,January 12, 2009 @20:50

FUEL shortage at various pump stations in the country might end soon, following arrival of tankers at the Dar es Salaam port. Four oil tankers are at the Dar es Salaam harbour loaded with about 80,000 tonnes of petroleum products that are expected to meet the nation's demand for about a month.

BP and GAPCO have reportedly informed the Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) that petrol stocks were running out. Engen pump stations run out of fuel over the weekend. Several petrol filling stations in Dar es Salaam witnessed long queues of motorists over the weekend, raising fears of imminent transport crisis.

The GAPCO Chief Operating Officer, Mr Krishna Pradrai, confirmed that the company had run out of petrol stocks since last weekend and was expecting to receive new stocks later this week. He said that a vessel MT Wawasan was at the outer anchorage carrying some 10,000 tonnes of petrol which would be shared by some four or five companies.

"It is unfortunate that the tanker will get into the port by January 16 (on Friday) to discharge the products. January 16 is just an indication date. I am not sure when the vessel will berth," he said. This means dealers of GAPCO will not get petrol until the vessel discharges fuel.

The BP Managing Director, Mr Engenlhard Kongoro, said that he was not aware of any shortage of fuel at his depot or pump stations supplied by his company, but said he would check on that.

The Managing Director of Engen, Mr Seelan Naidoo, whose pump stations in Mbezi and Mikocheni had run out of fuel, said the stocks supplied last Friday were exhausted because there was a rush at those points. "We have opened the depot this afternoon (yesterday) for trucks to draw fuel. We will make arrangements for other companies which have no stocks to get them from us," he said.

One of the four tankers christened MT Atlantic carrying about 30,000 tonnes made up of 16,987 tonnes of diesel, 4,000 tonnes of petrol and 4,807 of jet fuel, is discharging at the Kurasini Oil Jetty (KOJ), but is said to be slow in pumping out the products. It could not be established when MT Atlantic would complete discharging, an exercise that started over the weekend.

One port official said some tankers take up to three days to discharge such cargo, because it depends on the pumping rate. Three more tankers loaded with over 50,000 tonnes of petroleum products are at the outer anchorage, waiting for their turn to berth at the KOJ.

The Director of Petroleum with Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA), Mr Sirili Massay, told the 'Daily News' that the products carried in the four tankers, about 80,000, could meet the nation's demand for a month. EWURA's petrol indicative prices for Dar es Salaam starting today increased from 1,147/- last week to 1,171/- while the cap one moved from 1,233/- to 1,259/- per litre.

Wholesale indicative price for petrol in Dar es Salaam last week was 1,084/- and that of diesel 1,207/- and the cap price for both was 1,165/- and 1,297/- respectively and will remain the same this week. The indicative price for diesel last week in Dar es Salaam was 1,270/-, this week it will be 1,301/- per litre and the cap price was 1,365/- and now 1,399/- for the same measure.
 
...mimi ningekuwa jakaya ..ningewashika waagizaji walioandaa huu mgomo ambao hawazidi kumi na kuwaweka underground.....kwanza wapate psychological torture....alafu ikifika asubuhi ..naagiza wapewe chai waletwe ofisini kwangu ..na kuwauliza swali moja tu......MMEAMUAJE ?.....

....kuachiwa kwao kutategemea na jibu watakalotoa .....mara nyingine inabidi kuwa dikteta ili usichezewe mdebwedo... nitashangaa sana kama itafika asubuhi huu mgomo ukiwa bado unaendelea ...hapo nitajua tuna serikali au hatuna ..tujuwe moja!!!

lakini pia in another angle tutaona faida ya serikali kuagiiza akiba ya mafuta kupitia TPDC... STRATEGIC OIL RESERVE....

TATU inabidi waziri wa nishati na naibu wake wajiuzulu kwa kulidanganya taifa kuwa kuna akiba kwa ujumla ya kutosha miezi mitatu ...pale walipokuwa waki justify wauza mafuta kuuza hadi stock yao iishe... sasa stock ya miezi mitatu imeishaje kwa wiki moja????... hata hilo linashindikana kuhoji... na kuchukua hatua??
 
Mungu aiepushiye mbali!!Mkuu wangu hiyo sheria/wazo lako la 'Jicho kwa jicho',Taifa zima litabaki na Vipofu watupu!Yatakwisha tu haya,kumbuka Dar ni sehemu tu ya Tanzania.
 
Sheria ya uhujumu uchumi ya 1984 ichukue mkondo wake hakuna jipya nchi yetu ni ya utawala wa sheria.

Mkuu turudi semanini na nne kulikuwa na raha gani? Petroli, sukari,sabuni, viatu (Bora Shoes), etc. kwa foleni. Twende na wakati
 

PM,

Mheshimiwa Rais anatakiwa kuonesha makali yake katika hili. Inasikitisha sana, nini kinaendelea lakini? Kwanini hivi? Kuna watu wanatakiwa kuwajibishwa katika hili. Nina uhakika hali ikiendelea hivi kesho basi uzalishaji jijini Dar es Salaam utakwama kwa kiwango kikubwa.

Kweli Bongo tambarare!
 

kabisa kwa kuanzia ni lazima awafukuze kazi.....waziri wa nishati na madini na naibu wake..kwa kulidanganya taifa ..kwani juzi tu walisimama mbele ya kamera na kuwaambia wananchi wasiwe na shaka kwani makampuni yote kwa ujumla yana akiba ya miezi mitatu...na wakawataka UWURA wachukue hatua..bila kujali...

na kama nilivosema hawa wenye vituo hadi dakika hii ingebiidi wote wawe ndani ...kama kweli tunayo serikali...wakamatwe!!!..wanatishia uhai na usalama wetu!

ichunguzwe kama ewura wana uwezo wa kutosha kukabiliana na hili ....kama kuna uzembe nao kina haruna na wakurugenzi wenzake waendenyumbani....hatuoni faida ya ewura...kazi yao hata TBS ..wangefanya!!!

kuna mtu kasema hili ni deal la wahindi..hapana tusiwe wabaguzi... kwani nimegundua kuwa hata vituo vya mafuta vya wazalendo kabisaaa wamefunga pump zao...wengine kitambo..huu mgomo una kama wiki mbili..ulikuwa unashika kasi taratibu.....wakati huo watu kama kina OTHMAN badala ya kutoa alert ...walikuwa wanakesha kwenye njenje KARIMJEE...!!!...na kwingineko...huu mgomo au ukosefu kwa kweli ulikuwa unazuilika tu!

looosers...!!!
 
Mkuu PM,

Binafsi nimeshangazwa SANA na jambo hili na kujiuliza HIVI TUNAYO SERIKALI KWELI? Nafikia wakati nakata tamaa kabisa.

Issue behind vituo vya mafuta wasibambikizwe wahindi etc, wazalendo wengi tena wanasiasa wanamiliki vituo hivyo kwa migongo ya waarab 'wachukua kamisheni' tu.

Hakuna udhibiti wa soko huria Bongo? Pia siwalaumu wafanyabiashara pekee, nawabebesha lawama zaidi EWURA. Inaelekea hawajui walitendalo, maamuzi yalikuwa ya kukurupuka? Kwa manufaa ya nani? Athari ya hali hii ni kubwa sana kwa uchumi wa taifa. Kifupi ni uhujumu uchumi wa taifa kwa kiwango kikubwa sana. Inasikitisha SANA
 
Philemon Mikael,

..serikali ichukue hatua kwasababu inaelekea hawa waagizaji wa mafuta wako un-reliable.

..hatuwezi kucheza-cheza na sekta muhimu kama ya mafuta.

..uchunguzi ufanyike kubaini kama hii ni hujuma au ni kweli kuna uhaba wa petroli.

..Strategic Oil Reserve inahitaji ushirikiano wa serikali na waagizaji mafuta ktk ku-share information. kama kinachoendelea ni hujuma na migomo, still kunaweza kutokea uhaba kama huu wa sasa hivi.

NB:

..hivi kwanini EWURA walaumiwe ktk hili? hivi wamekosea nini kuteremsha bei ya mafuta?

..wa-Tanzania vigeugeu kweli-kweli. yaani tayari tumeshatishika tunataka tununue mafuta kwa bei ya kuruka!!

..juzi tu hapa tulikuwa tunapiga kelele kuwashinikiza EWURA wateremshe bei na wa-enforce zoezi hilo. sasa wametusikiliza tunadai eti wamekurupuka.
 
....wanafanya hivyo kwa sababu wanajua hakuna serikali pale,hizo kamba zao za kusema stock imekwisha ghafla ni upumbavu wa hali ya juu na uwongo wa kitoto,serikali lazima wapate sababu za kueleweka na zinazokubalika kisheria kwanini hawakuagiza mafuta on time wakati wamepewa hilo jukumu na kama kuna uzembe au any sabotage hawa ng'ombe lazima watiwe adabu,na uchunguzi(physical) kwenye mapipa yao lazima ufanywe sio data zao zao za kupikwa...hakuna mtoto hapa wa kudanganywa na tunajua hizi ni deal zao za kilafi tuu ili kupata super profit,dawa ni kuwafuta kwenye biashara ya mafuta forever na kuwafikisha mahakamani kuwachapa fine za kuwafilisi mpaka mali zao,hatuwezi kuvumilia sabotage kama hizi za kurudisha nchi nzima nyuma kiuchumi na kutishia usalama wetu...inakuwaje leo oil price ikipanda new York nao wanapandisha for the same reason lakini ikishuka eti stock ni ya mwezi uliopita? sasa ni time ya kuwafanya mfano kwa watu wote wenye tabia kama hizi na kuhakikisha hakunasector/mtu atatuchezea kwa namna hii tena...ni EWURA/waziri wa nishati nao watimuliwe kwa uwongo wao wa kusema last week kuna mafuta ya kutosha na Ewura wameshindwa kuwadhibiti hawa walfi wakti kuna sheria kibao zilikuwepo za kuwatia adabu lakini hawakufanya kitu...lazima kuwe na zero tolerance kwenye vitu kama hivi la sivyo tutazidi kuwa maskini tuu.
 
Mkuu turudi semanini na nne kulikuwa na raha gani? Petroli, sukari,sabuni, viatu (Bora Shoes), etc. kwa foleni. Twende na wakati

Mkuu Cynic

Sheria haisemi hayo uliyoandika bali hayo uliyoandika ndiyo yalileta sheria hiyo baada ya watu kuanza "ulanguzi" hii pia ilikuwa inaitwa sheria ya walanguzi yaani wanabania bidhaa ili ku-create excessive demand na kisha kuuza bidhaa kwa bei ya kuruka.

Kamwe hatuwezi rudi katika hali hiyo kwani sasa hivi kuna watanzania wengi na wenye uwezo wa kufanya biashara hiyo ya mafuta, hapa kwa serikali ni kata mti mingine mingi ipo. Hawa watu wahuni wachache wamepigiana simu na kufanya "collusion" wanaamka asubuhi na kukataza mafuta yasiuzwe kwa kisingizio cha stock imeisha dawa yao nao ni kuwaonesha kuwa sheria za nchi ndizo zinawafanya waagize na kuuza mafuta bila bugudha yoyote ya kuhujumiwa mali zao na kuwafanya walale usingizi sasa lazima wazifuate, vinginevyo zitatumika ipasavyo kuwafanya na wengine (watumiaji) kupata mafuta bila bugudha. Kama biashara ya mafuta hailipi waache wakalime tujue moja.
 
JokaKuu,

Tunachoilaumu EWURA ni kutoa statement kwamba mafuta yapo. Ila napata wasiwasi zaidi kwamba mafuta inaelekea yapo, kilichofanyika ni hawa wafanyabiashara kuamua kuigeuzia kibao serikali baada ya wao kufanyiwa uchunguzi na vituo zaidi ya 50 jijini kukutwa kuwa vimekuwa vikiwabamiza wananchi kwa kuminya pumps zao na kuwauzia mafuta kidogo. Inaelekea wakati wanakubali bei mpya hawakutarajia wangechunguzwa pumps zao na kufanyika kwa hili kumewafanya wakasirike na wote GHAFLA wameishiwa mafuta.

Inaudhi sana hii, huu ni mgomo na wala sidhani kama ni suala la kuisha mafuta! Haiwezekani ghafla siku moja vituo VYOTE vimeishiwa mafuta! Ni mpango wa makusudi tu.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…