Vitunguu kutoa mabomba na maua - Msaada

Vitunguu kutoa mabomba na maua - Msaada

The Giant

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2012
Posts
504
Reaction score
96
Wakuu habari,
tumetoka kupiga dawa ya ukungu, vitunguu vishaanza kutoa mabomba na maua msaada ni kitu gani kinahitajika nifanye kwa sasa?
 
Hayo mabomba baadae yatafanya kitunguu kuharibika(kwasu) yani yanashuka had I ndani ya kitunguu na ukivunq kitunguu lile bombs linakauka hata upikeje haliivi

Fanya kukata mapema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini chanzo cha vitunguu kutoa mabomba(bolting)?

Kwa kawaida vitunguu hutoa maua mwaka wa pili wa maisha yake. Usipovivuna ule mwaka wa kwanza ukaendelea kuvitunza na hali ya hewa ikiwa nzuri vitatoa maua mwaka wa pili na kuzalisha mbegu.
Kwa hiyo vitunguu havipaswi kutoa mabomba (bolting) na hatimaye maua katika msimu wa kwanza. Vikifanya hivyo jua kuna tatizo.

Kwa nini vitunguu hutoa mabomba(flower stalks) katika msimu wa kwanza?
Kuna sababu 2: Joto kali au baridi kali.
Mmea wa kitunguu unapokabiliwa na hali ngumu- kutokana na joto au baridi- kwa jinsi ulivyoumbwa "hupata hofu" kuwa utakufa bila kuacha watoto! Kwa hiyo haraka haraka huanza kutengeneza maua hatimaye mbegu ili uweze kuacha uzao kabla haujafa.
Jinsi ya kupunguza tatizo la kutoa mabomba
*Kama kuna hali ya joto ni muhimu kumwagilia vitunguu ili kupunguza joto na kuvipa maji ya kutosha ili visihisi kuwa kuna tatizo.
*Kama ni baridi kwa kweli hapa huna la kufanya labda ukwepe msimu wa baridi kali kabla hujapanda. Lakini kama hali ya baridi itatokea bila kutarajia basi hakuna jinsi.
Ili kuepuka hali mbaya ya hewa unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha green house.
Kama vitunguu vimetoa mabomba yaondoe mapema maana bila hivyo chakula chote kitaelekezwa kwenye maua na mbegu(watoto).
Vitunguu vilivyotoa mabomba havifai kuhifadhi kwani vinaharibika haraka kwa hiyo vivune na kula/kuuza mara moja
 
Asante sana kwa maoni yenu wakuu. shukrani tena sana.
 
Back
Top Bottom