Vituko vya Rais Kikwete dhidi ya Albino

Vituko vya Rais Kikwete dhidi ya Albino

Hujui kuwa Rais anayo mamlaka ya kutafuta pesa kwenye vyanzo vyake vingine kwa mamlaka aliyonayo na kufanya jambo lolote.

Akipunguza bajeti yake ya safari za kwenda nje kuaga na kununua hayo madawa ndo nitaamini kuwa kweli anayo nia thabiti ya kusaidia hawa ndugu zetu.
 
Kwa bajeti ipi?? Au unafikiri bajeti ya nchi iko kama nyumbani kwako unavyoweza kuamka asubuhi ukaagiza vitumbua kwa mama soph wakati ulipanga chai ipigwe na kiporo??
We kitasa kweli kwani ujenzi wa bomb la gesi ulikuwepo kwenye bajeti ya awali?
 
Naye Jk na CCM yake akawaambia MAWAZIRI wake na wanachama wa CCM

KESHENI mkiomba kwani hamjui siku wala saa atakayokuja Dr
Slaa na UKAWA yake,Nami naenda Ulaya kuwaandalia MAKAZI ya kudumu,ili nitakapokuwa nanyi
muwepo,kwani CHADEMA ikichukua nchi mwaka huu,lazima mafisadi tuhame nchi.

Nanyi muonapo wa-Tz wanaipinga sana CCM na kuisapoti CHADEMA ,huku tume mbalimbali zikiundwa, basi mtambue muda wa wa MATESO kwa MAFISADI
umekaribia.

Wala msitishwe na wingi wa watia nia wenu wa CCM,kwani hata Lowassa mwenye pesa nyingi za KIFiSADI,lakini kamwe hawezi kuwa rais wa nchi hii.

Kisha Lowassa alipoyasikia hayo na kauli za makutano,basiakakwea tena IKULU kumuomba Rais ASIMFILISI,ASIMFUNGE WALA ASIKUBALI LOWASSA AJIUZURU, Lakini kabla ya wananchi hawajamsahau Lowassa na ufisadi wa RICHMOND,EPA,na RADA na ndicho kipindi yule katibu mkuu wa CCM mwizi wa tembo akijiandaa kuanzaa ziara za kuwahadaa wananchi mikoa mbalimbali,
akatokea Kafulila,Mbowe ,Mnyika na Zitto na jeshi lao lote wakaibua ufisadi wa ESCROW,na Kafulila akasema na "Nitakaowabusu hao ndio wezi waliokula pesa za Escrow na kulifisi taifa",basi akiwa bungeni akawataja jaji Werema,Pinda na Chenge nayo kamati ya PAC kupitia Zitto Kabwe ikawataja wengine wengi hata wale waliokuwa wamefichwa na wengine walioiba na kubeba fedha kwenye magunia kule kwenye benki ya Stanbic,bt Ikulu ikawalinda.

Mara AG WEREMA akatoa UPANGA ALANI na kumtishia Kafulila,mfuasi wa UKAWA kutaka kumkata shingo,ndipo PINDA kwa fedheha kubwa akamwambia WEREMA"rudisha upanga wako
alani,KIKOMBE tulichotupiwa na Kikwete hatunabudi Kukinywa.

Moja kati wa mayahudi wale aitwaye Muhongo hakuamini kama Kafulila
anaweza kitikisa serikali,mara TIBAIJUKA akasimama na kusema yeye hakujua kama pesa aliyokula ilikuwa ni ya kifisadi ya Escrow na Rugemalila aliyempa,ati alimpa kama kaka yake kwa ajili ya shule zake za Kajumulo

Basi siku ya3 wezi wakaenda pale ofisini kwa spika na ofisi ya PAC ili waibe nyaraka,lakini wakazikosa.

yule morani waliyemkuta getini
akawaambia mnayemtafuta(document za PAC) hazipo..Kafulila na Zzk wameshapaa nazo kwenda Kigoma na wapo
kuume kwa UKAWA

Basi wanaCCM walipoyaona hayo,kwa masikitiko wakasema"HAKIKA MWAKA HUU LAZIMA CCM ING'OKE NA CHADEMA KUPITIA UKAWA WACHUKUE NCHI"
Sina mbavu!
 
Kwani kwenye bajeti hakuna fungu la madawa? si hilo hilo ndiyo atatenga za hao ndugu zetu.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Kama fungu la dawa lipo kwaajili ya alu ( mseto) atapeleka kwenye dawa nyingine watu wafe kwa malaria???? Au hujui wanakua na takwim za namna yakuagiza madawa
 
Hoja nyingine bwana,mtu kama huna cha kuandika si uache kuliko kujipa ufundi wa kumdhihaki Rais Kuweni na adabu siyo sifa hiyo!

Unajikomba nini kwake wakati alikwishaonesha ni DHAIFU! Wacha nidhamu ya woga huu ni wakati wa digitali!
 
Wakati bajeti ya wizara ya afya imekwisha somwa na kupitishwa bungeni kwa mwaka 2015/16, eti JK atahakikisha vifaa na madawa kwa ajili ya watu wenye albinism yanatengewa fedha na kununuliwa na kwamba vyote vitakuwa bure! Ahadi hii ameitoa leo huko Arusha katika sherehe ya siku ya kimataifa albinism!

Hiki ni kituko kwani waziri wake wa afya hakuzungumzia cho chote kuhusu suala hilo wakati wa bajeti ya afya! Na kama JK atalazimisha kutekelezwa kwa ahadi basi ama bajeti ya wizara itavurugika au itakuwa ahadi mpya ambayo haitatekelezeka hadi anamaliza muda wake October mwaka huu!!

Cha kujiuliza hivi JK hakomi kuahidi ahadi hewa au haoni aibu kwa kutotekelezeka kwa ahadi lukuki alizowaahidi wananchi nchini kote mwaka 2010?!
Nyie chadema hangaikeni na haya kwanza mkiyamaliza mje tuzungumze zitto mwenyewe anawalaza nje.
 
Unajikomba nini kwake wakati alikwishaonesha ni DHAIFU! Wacha nidhamu ya woga huu ni wakati wa digitali!
Unakumbuka kuwa hata chai uliyokunywa katoa yeye kwani bado hujamuuliza mzazi wako wa kike?
 
Huyu mleta mada atakuwa ni miongoni mwa wanaoua maalbino. Sijui kwa nini anawachukia sana kiasi hiki
 
Huyu mleta mada atakuwa ni miongoni mwa wanaoua maalbino. Sijui kwa nini anawachukia sana kiasi hiki

Kwani mauaji ya albino yameanza leo! Hukumbuki hata Pinda alimwaga machozi bungeni!!

Wacha hizo au ndiyo kampeni yenyewe!
 
Hahaahahaha nilisikia eti kuwa "ameapa" kuwalinda Albino, nikacheka sana, yaani kashindwa akiwa Rais ndio ataweza akiwa mtaani??
 
Mkubwa hakosei. Anajua anachosema ndiyo maana kakisema.
 
Kwani kwenye bajeti hakuna fungu la madawa? si hilo hilo ndiyo atatenga za hao ndugu zetu.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Kwa nini aseme atahakikisha madawa na vifaa vinanunuliwa, ina maana hamwamini katibu mkuu na waziri wa afya kuifanya kazi hiyo, kwanza bajeti ya wizara kaisoma na kujua madawa na vifaa vimetengewa kiasi gani? Au ndo anataka 'kuburst' matumizi ya wizara kama alivyo pasua matumizi ya ofisi yake yasemekana kwa asilimia mia tatu? Nakuuliza wewe FF, acha kujikausha kama hujayaona maswali!!!
 
Back
Top Bottom