Vituko vya Rais Kikwete dhidi ya Albino

Vituko vya Rais Kikwete dhidi ya Albino

duuuh apo anaongea akili yake inawaza newyork..usishangae kesho unaambiwa yupo majuu
 
Hivi unaamini kabisa bajeti inayosomwa bungeni ndio inayotekelezwa? Kama ulikuwa hujuwi zaidi ya asilimia 60 ya fedha za miradi ya maendeleo zilizopitishwa na bunge 2014/2015 hazijapelekwa kwenye halmashauri.kwa hiyo jk ni haki yake kutoa ahadi hiyo.kusoma bajeti ni kukamilisha ratiba tu na kulipana posho.
 
Hivi Mlisho kichwani uwa hakumbuki chochote.Ahadi kibao mpaka leo bado na nyongeza tena.Mlisho noma kweli
Eti amewaahidi walimu kuwa atamkabidji rais ajaye baadhi ya madai yao!
 
Yaan watu wanatuona sisi mazuzu kweli, ahadi juu ya ahadi zisizo tekelezeka!
 
Wakati bajeti ya wizara ya afya imekwisha somwa na kupitishwa bungeni kwa mwaka 2015/16, eti JK atahakikisha vifaa na madawa kwa ajili ya watu wenye albinism yanatengewa fedha na kununuliwa na kwamba vyote vitakuwa bure! Ahadi hii ameitoa leo huko Arusha katika sherehe ya siku ya kimataifa albinism!

Hiki ni kituko kwani waziri wake wa afya hakuzungumzia cho chote kuhusu suala hilo wakati wa bajeti ya afya! Na kama JK atalazimisha kutekelezwa kwa ahadi basi ama bajeti ya wizara itavurugika au itakuwa ahadi mpya ambayo haitatekelezeka hadi anamaliza muda wake October mwaka huu!!

Cha kujiuliza hivi JK hakomi kuahidi ahadi hewa au haoni aibu kwa kutotekelezeka kwa ahadi lukuki alizowaahidi wananchi nchini kote mwaka 2010?!

Mkuu Ileje,

Wala hata hii usiite kituko, pia sioni kwamba ni ajabu kwangu mimi. Mwaka jana watu walikaa kwenye bunge kama hilihili, wakapitisha mambo kibao tu. Umesikia mwaka huu walivyosema? kama hujasikia basi ni kua HAKUNA lolote lililopitishwa mwaka jana likaenda kama lilivyopangwa.

Kifupi ni kua kikao cha bajeti ni formality na kutafuna hela tu, hua hakuna linalopangwa pale likaenda hivyohivyo. Serikali ndio inayoshikilia pesa. Inagawa pesa pale inapojisikia, sio kuangalia bajeti inasema nini.
 
Last edited by a moderator:
Rais jk ametokwa na machoz wakati akisikiliza wimbo wa masikitiko ya watoto wenye ulemavu wa ngozi(albino) na kueleza kuwa ni upambavu kuamini kuwa viungo vyao vinateta utajiri. Chanzo gazeti la mwananchi. Swali la kujiuliza hapa! Nikua mh! Rais tatizo hili ukuliona awal mpaka wazir mkuu alilia bungen? Na kwa nini mkiwa kama viongoz mnashindwa kuchukua uamuz mgumu? Hapa ndipo mzee wa maamuz magumu anapochukua point! Ikiwa mkuu wa nchi unalia na wazir mkuu analia hv hawa wauwaj wanajesh? Kama mkulu na team yako mnashindwa kuwalinda hawa ndugu zetu wachache hao milion 45 mtaweza?
 
Mkuu Ileje,

Wala hata hii usiite kituko, pia sioni kwamba ni ajabu kwangu mimi. Mwaka jana watu walikaa kwenye bunge kama hilihili, wakapitisha mambo kibao tu. Umesikia mwaka huu walivyosema? kama hujasikia basi ni kua HAKUNA lolote lililopitishwa mwaka jana likaenda kama lilivyopangwa.

Kifupi ni kua kikao cha bajeti ni formality na kutafuna hela tu, hua hakuna linalopangwa pale likaenda hivyohivyo. Serikali ndio inayoshikilia pesa. Inagawa pesa pale inapojisikia, sio kuangalia bajeti inasema nini.

Wenyewe wanasema tunatekeleza dharura tu, hii miradi mingine huwa inasimamiwa na wafadhili moja kwa moja
 
Last edited by a moderator:
si wako wanaotakiwa kunyongwa?.
si uwanyonge kabla hajaondoka!
 
ukimuona mtu analia hana uwezo wa linalotokea mbele yake, ndio maana hakuna namna ya kufanya mtu anapokufa zaidi ya kulia tu,
 
Wenyewe wanasema tunatekeleza dharura tu, hii miradi mingine huwa inasimamiwa na wafadhili moja kwa moja

Na madhara yake ni kua wafadhili wakigoma kama walivyogoma bajeti inayoisha sababu ya ESCROW SAGA tunakosa dollar zao kwenye mzunguko kiasi cha kufanya dollar ziadimike na kua ghali.
 
Acha kumkejeli rais.unaonesha ulivyo na upeo Mdogo wa kutafsiri mambo haswa mambo ya uongozi
 
Na madhara yake ni kua wafadhili wakigoma kama walivyogoma bajeti inayoisha sababu ya ESCROW SAGA tunakosa dollar zao kwenye mzunguko kiasi cha kufanya dollar ziadimike na kua ghali.

Na moja ya sababu ya kupanda kwa dolar vs shillingi kwa sasa ni kupungua kwa miradi hiyo iliyokuwa inaleta dolar nyingi nchini.
 
Hivi unaamini kabisa bajeti inayosomwa bungeni ndio inayotekelezwa? Kama ulikuwa hujuwi zaidi ya asilimia 60 ya fedha za miradi ya maendeleo zilizopitishwa na bunge 2014/2015 hazijapelekwa kwenye halmashauri.kwa hiyo jk ni haki yake kutoa ahadi hiyo.kusoma bajeti ni kukamilisha ratiba tu na kulipana posho.

Niko pamoja na wewe. Hivi vikao vya bajeti vingefutwa ili hizo fedha wanazolipana zikajenge shule, hospital, madawa, etc.
 
President anauwezo na mamlaka kikatiba kutamka lolote na likatekelezwa...over!

Kwenye fiscal policy Rais HAWEZI kutamka kitu ambacho hakipo kwenye bajeti ya Wizara wala kwenye bajeti kuu!La sivyo apeleke pesa zilizotengwa kwa MAAFA kwenye albino

JK huwa ana ahaidi tu!Kyela alituhaidi meli mpya na barabara Kikusya-Matema Beach hadi leo hamna kitu
 
Watoto wanalia mama analia baba naye analia nani atawabembeleza, au tusubiri majirani waje kutuambia nini cha kufanya?
 
Kwenye fiscal policy Rais HAWEZI kutamka kitu ambacho hakipo kwenye bajeti ya Wizara wala kwenye bajeti kuu!La sivyo apeleke pesa zilizotengwa kwa MAAFA kwenye albino

JK huwa ana ahaidi tu!Kyela alituhaidi meli mpya na barabara Kikusya-Matema Beach hadi leo hamna kitu

Mma ngafu. Hata upembuzi yakinifu haujafanyika?
 
Mma ngafu. Hata upembuzi yakinifu haujafanyika?

Mbala pala fibo kikolo!
Ahadi zake hizi Kyela tulikesha barabarani kishangilia maana tukajua meli mpya na barabara hadi Matema utaimairisha uchumi wetu!Hiyo ilikuwa 2005

Ahadi hizi hazitekelezwa,hatujaona meli mpya wala hata survey ya barabara ya Matema haijafanywa

JK ni Rais mzushi pengine kuliko wote hapa duniani
 
Back
Top Bottom