Vituko vya Mfugaji kwa mwandishi wa habari

Dr. Wansegamila

JF-Expert Member
Feb 3, 2012
2,858
7,847
Mkulima amejiwa na mwaandishi wa magazeti kumuhoji ... kuhusu maisha ya shambani,na mkulima huyu hawapendi
waandishi wa habari akaona bora amchoshe katika kujibu maswali,
na mambo yakawa hivi;
MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?,
MKULIMA: Ng'ombe yupi Mweupe au Mwekundu?
MWANDISHI: Ng'ombe mweupe
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi,
MWANDISHI: Na mwekundu??
MKULIMA: vilevile nyasi na viguta vya mahindi,
MWANDISHI: ahaa sawa,na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Mweupeee!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee,
MWANDISHI: na mwekundu?
MKULIMA: vilevile ninamlaza na mwenziwe!!!!
MWANDISHI: Hii sehemu yote majumbamengi,Na wakienda
kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Woooteeee!!!! {kwa hasira}
MKULIMA: Mweupe nina mfunga kambana kumzungusha
malishoni na kumrudisha,
MWANDISHI: na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu?,mweku ndu ninamfunga kamba na
kuzunguka nae kama mwenziwe!!!
MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma
za ng'ombe zako unaniuliza mweupe au mwekundu
halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa?????,
MKULIMA: Kwasababu Ng'ombe mweupe ni wangu,
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Ni wangu vilevile!!!!!!
MWANDISHI HOI..!!
 
hehe Huyo Ng'ombe Mweupe atakuwa kazaliwa Tanga Siku moja na Nazjaz
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom