Taarifa minimum
Shinyanga, Dar, Pwani, Mafia,Tanga, Mwanza, Geita, Mara, Simiyu, Kigoma na Kagera tujiandae, kutakuwepo na Pacific El nino na Atlantic El nino, mvua zitakuwa kubwa na hatari sana, Mungu atunusuru. Hali ya hewa tayari imebadilika kuanzia juzi, upepo umeanza katika bahari za Atlantic, Pacific na Hindi, Wavuvi wameanza kuzuiwa kwenda kuvua na Meli za tafiti zimeanza kukumbana na dhoruba kali sana Baharini, picha za satellite sio nzuri kabisa. Tunatarajia magonjwa ya Kuharisha, Dengue, Malaria na Homa kuongezeka, tuchukue tahadhari mapema.
Tuangalie nyumba zetu kama zinavuja, turekebishe, tununue Neti za Mbu, tuangalie miundombinu ya maji taka kwenye nyumba zetu. Tununue Jik na water guard kwa ajili ya kuweka kwenye maji ya kunywa, kumbuka kipindi hicho umeme utakatika sana kwa hiyo tununue taa za kuchaji. Sehemu za nyumba ambazo sio imara turekebishe. Tuweke akiba ya chakula na dawa.
Tununue dawa za Mafua, dawa za Watoto za Mafua na Kuharisha, na dawa za Malaria. Tuhifadhi vyakula vikavu kwa mfano nafaka kwa wingi na tununue vitu vya kuhifadhia vyakula. Shinyanga, Dar, Pwani, Tanga zitapata mvua za kiwango cha juu zaidi (above normal to normal)
Send as received