Wenzetu wanajua mziki mfano mzuri ni nchi ya Nigeria .Burna boy ,davido na Rema ni baadhi ya wanamziki waliofanya show kwenye matukio makubwa .,ufunguzi wa Kombe la dunia na UEFA lakini kama haitoshi Rema amefanya show kwenye tukio kubwa la ugawaji wa tuzo za Ballon d'or ,wanapata hayo mashavu kwa sababu wapo siriasi na mziki kuanzia mavazi mpaka utunzi wao wa mashairi ..mziki unahitaji Branding
Njoo Tanzania sasa,Mbosso ni msanii mkubwa tu tena yupo lebo kubwa ya WCB lakini cha ajabu anakuwa kama upcoming star wa vichochoroni ,hivi tunategemea mziki wetu usikilizwe na kutazamwa kama mwanaume anaingia na kanga stejini !! hichi ni kituko cha mwaka Waandaaji wa tamasha la wasafi Festival ni wabunifu ila wana over think sana ,wasanii wanafanya vitu ambavyo havina ulazima
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.