Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

FB_IMG_1674582158692.jpg
 
MWAMBIENI MAGANGA AACHE KUBISHANA NA MFUMO AKARIPOTI.

Na Thadei Ole Mushi.

Katibu Mkuu wa CWT aliyeteuliwa kama nilivyowaambia Asubuhi anataka kugomea uteuzi wa Rais. Amelala na Maruweruwe kaamka akatangaza kwenye group la CWT HQ kuwa yeye bado ni Katibu Mkuu wa CWT.

Kutema Milion 7.6 za mshahara na ukijumlisha na allowance nyingenezo anakuwa na milioni 10 plus si kazi ndogo halafu unamwambia akasuluhishe migogoro ya wafugaji na wakulima huko Kerwa lazima alale akiwa anaota ndoto za ajabu ajabu.

Kosa kubwa analolifanya ni kushindana na Mfumo unaomhitaji . Soon huo U DC anaukosa na huo U KM unapeperuka. Mliopo karibu naye mwambieni akaripoti mara moja na aanze kazi ya kutekeleza Ilani ya CCM.

Always nawaambiaga never outshine the Master …. Yaani asijifanye ana akili kuliko waliomteua. Sisi walimu tunachoweza kukisema kwa Mh Rais ni kumshukuru kwa kuleta TIBA kwenye hiki Chama Chetu cha Walimu.

Ole Mushi
0712702602.
 
Back
Top Bottom