Wazee hali ni mbaya
WATU 179 WAUAWA NDANI YA JANUARI PEKEE: Watu 179 wameuawa katika kipindi cha mwezi Januari na tayari Jeshi la Polisi limewakamata zaidi ya watu 150 wakihusishwa na mauaji hayo yanayosababishwa na visasi, wivu, kugombea mali, ushirikikina, ulevi na watu kujichukulia sheria mkononi.
Kufuatia kushamiri kwa mauaji hayo Serikali imeunda Kamati Maalum yenye wajumbe kumi na mmoja kutafuta ufumbuzi wa kudumu na kukomesha matukio haya ikihusisha Wizara ya Mambo ya Ndani, TAKUKURU, Usalama wa Taifa, Polisi na Ustawi wa Jamii.
Taarifa za mauaji katika mwezi Januari zimekuwa zikigongwa vichwa vya vyombo vya habari hatua iliyosababisha kuibuka kwa sokomoko miongoni mwa jamii kila mmoja kiuliza kulikoni matendo hayo yameshika kasi.
Kutokana na hali hiyo na lawama kutupwa kwa Jeshi la Polisi, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ameitisha kikao na kukutana na viongozi wa juu la Jeshi hilo ambapo akatoa takwimu za mauaji mpaka sasa nchini.
#mauaji #takwimu #viongozi #TAKUKURU #Polisi #usalama #ustawiwajamii #wizarayamamboyandani #waziri