😂 😂 😂Wazo zuri
Hakuna machungu yanachoma kama kuanguka ukiwa wima.Huyu hana shida. Ni tajiri tayari. Hapo anavuta mshiko mrefu wa posho za ubunge bure tu. Na baada ya miaka mitano miliono 300 zinamsubiri. Na nadhani ni balozi pia...
Tunajifurahisha tu mitandaoni humu tukidhani kuwa hawa jamaa wameanguka lakini ukweli ni kwamba wameanguka huku wakiwa wamesimama!
Mwenyewe amewahi kulisema hili? Kuwa anaumia sana kupoteza hizo nafasi? Ataumia tu kama hajitambui. Wangapi tumewaona wakipoteza hizo nafasi wakakaa kimya halafu wakarudi, tena kwa nafasi za juu zaidi? Tena huyu balozi na mbunge?Hakuna machungu yanachoma kama kuanguka ukiwa wima.
Kumbuka huyu ndugu alikuwa juu ya kila kitu ndani ya CCM, kisha kwa muda mfupi akawa juu ya kila mtumishi serikalini.
Hapo alipo sasa yupo chini kuliko mbunge wa jimbo.
Inauma hiyo ila huioni.
Kuna mazingira hela si kitu mbele ya heshima hasa kwa jamii aliyotokana nayo ndugu yetu huyo

Nimecheka kamandaMwenyewe amewahi kulisema hili? Kuwa anaumia sana kupoteza hizo nafasi? Ataumia tu kama hajitambui. Wangapi tumewaona wakipoteza hizo nafasi wakakaa kimya halafu wakarudi, tena kwa nafasi za juu zaidi? Tena huyu balozi na mbunge?
Simtetei na wala simjui lakini Wabongo tuna tabia mbaya ya kufurahi na kushangilia "wenzetu" wanapoanguka hata kama kuanguka kwao hakutusaidii kwa namna yo yote ile. Tabia hii ipo kuanzia kwenye familia na kwingineko. Ni tabia ya hovyo!




Hana majaribu yo yote huyu. Nyie endeleeni kufurahia kwa sababu ni haki yenu. Ndivyo dunia ilivyo. Hata uwe mwema namna gani siku ukitetereka jua utachekwa tu. Alichekwa Bwana Yesu sembuse mimi na weye Ostaadh? Funzo hapa kwangu na wewe ni kwamba tuishi kwa wema na haki lakini pia tutambue kuwa siku tukianguka watu wengi tu watafurahi; na watacheka. Na kama tuliishi maisha mema na yenye kuliwaza roho zetu na za wengine hilo halipaswi kutuumizaNimecheka kamanda
Watu wanaweza kufurahia kuanguka kwako kama uliwaumiza kwenye utumishi wako.
Hata hivyo kupelekwa bungeni ni sawa na kuhamishiwa field ili aone namna siasa zinavyofanywa kwenye jumba hilo la kutunga sheria.
Kuhusu ubalozi ni sawa, lakini hawezi kulipwa mpaka apangiwe kituo cha kazi.
Kwamba anaweza kuibuka kivingine hilo halina shaka, lakini kwa sasa kuongelea majaribu anayopitia ni haki yetu maana linatuachia funzo kwenye maisha ya siasa.








