Kuna vitu viwili ambavyo vinanikera sana hapa Dar,moja ni watu wanavyo gombania kuingia kwenye daladala badala ya kupanga foleni na kuingia kistaarabu bila kukanyagana na kuumizana.Mara nyingine hii husababisha kuchafuliana nguo,kuibiwa na hata kuchaniana nguo.Hili swala la kugombania usafiri halipo nchi za jirani kama Kenya,Malawi hata Zambia likija basi watu wanapanga foleni na kuingia kistaarabu.
Jambo la pili ni jiji kubwa kama hili kuwa na kituo kimoja tu cha zimamoto na moto ukitokea pembezoni ya jiji uwezekano wa kupoteza kila kitu ni mkubwa sana.
Jambo la pili ni jiji kubwa kama hili kuwa na kituo kimoja tu cha zimamoto na moto ukitokea pembezoni ya jiji uwezekano wa kupoteza kila kitu ni mkubwa sana.