Vitendo ndani ya School buses!

MONTESQUIEU

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
847
Reaction score
80
Kuna malalamiko mengi kuwa watoto wanatendewa vitendo visivyo vizuri ndani ya school buses .

Nasikia kuna kesi tele zinalipotiwa na huwa zinamalizwa juu kwa juu, juu ya ukatili wanaofanyiwa watoto wadogo ndani ya hizi school buses.

Je hii ni kweli wanajamii?

Nilichofikiri haraka ni kwamba hizi school buses

Zinaendeshwa na madereva vijana wa mitaani
Kondactors wao ni wavulana ambao wengi ni mateja wa mitaani


KAMA HIZI TETESI NI KWELI

Ni bora kila shool bus condactor wake akawa mwanamke ili kunusuru maisha ya hawa watoto!

Wazazi mhakikishe mazijua bus na mnawajua watu wanao beba watoto wenu alfajiri saa 11 na kuwarudisha jioni saa 12 hata saa moja
 

Hujaeleweka meku
 
kama mtoto wa mwisho kumshusha ni binti au mvulana madereva na konda huwa najisi kwa kuwadanganja watoto na vi chips
 
kama mtoto wa mwisho kumshusha ni binti au mvulana madereva na konda huwa najisi kwa kuwadanganja watoto na vi chips

Na hawa watoto bado ni wadogo hawajui chochote, na wazazi wao ndio hao kutwa kukimbizana na vishilingi habari ya watoto wanajua kulipa school fee na bus fare!
 
Hata watoto wenyewe kwa wenyewe wananajisiana pia....mtoto wa form 6 na wa darasa la 1 wanapand basi moja
 
Mtoto wa jirani yangu, ni wa kiume kanajisiwa na "anko" bus conductor wa school bus...
Very sad
 
Mchakato mzima wa kusaka hela bongo unabidi upitiwe vizuri. Wazee tumeacha kulea tunadhani pesa itatulelea watoto wetu.

Katika nchi isiyo na sheria wala mifumo ya kueleweka, kumkabidhisha mtoto wako kwa dereva wa basi ni sawa na kujinunulia janga.
 
Mtoto wa jirani yangu, ni wa kiume kanajisiwa na "anko" bus conductor wa school bus...
Very sad

Jamani ona sasa, na wanaogopa kureport eti kwa maslahi ya mtoto. Jamani wazazi tuamke tukatae ma uncle kwenye usafiri unao husu watoto hawa malaika
 
thread hii imenigusa sana,ni kweli haya yanayozungumzwa huenda yanafanyika na ni vema kuchukua hatua kukabiliana na vitendo hivi vya kishenzi la sivyo watoto wetu wa kiume kwa wa kike watakuwa katika hatari ya kuharibiwa future yao au hata kuambukizwa magonjwa!
 
.... kweli huwezi kuamini, mtoto wangu wa kike 6 years aliombwa apeleke sh 5,000 na "uncle" wa school bus. na huu ndio ulikiwa mwisho wa school buses kwangu ....
 
.... kweli huwezi kuamini, mtoto wangu wa kike 6 years aliombwa apeleke sh 5,000 na "uncle" wa school bus. na huu ndio ulikiwa mwisho wa school buses kwangu ....

Mh wanawafundisha hata wizi watoto wetu, kwa kweli hawa ma uncle wa school buses hawana maadili yakuweza kuwa wanatubebea waaminifu kutusafirishia hawa malaika
 
Wachangiaji mmechukua hatua gani kuondoa ili tatizo?
 
Hili ni tatizo lingine la kukurupuka. Wazazi wameona school bus ndio mwisho wa matatizo. Hajui mwanawe anachukuliwa na basi gani wala anaendeshwa na nani. Madereva bangi wanakimbiza magari ya watoto hovyo na kupita njia zingine za ajabu ajabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…