Vitabu nilivyosoma mwaka 2018 – Zitto Kabwe

Vitabu nilivyosoma mwaka 2018 – Zitto Kabwe

Kila mmoja anaweza kusoma angalau vitabu 12 Kwa mwaka Cha msingi anza na Ratiba ya Siku moja Kwa kuacha kuchezea muda vibaya Kwa porojo zisizo na mashiko
 
Du!. Zitto wewe kiboko!. Mbona vitabu vingi sana, unapata muda kuvisoma vyote saa ngapi?.
Mwenzako analala na mafiles wewe si utakuwa unalala na vitabu?. Kama unalala na vitabu, jee unapata muda wa kulala na 'kulala'?.

P
Ngoja nikifika home namuongezea kingine cha executive intelligence asome mwaka huu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeng'ang'ana na Mtu Kulala na Mafile, Wasukumu Hawana Wivu Wa Aina Hii
Jee unapata muda wa kutosha kupumzika?. Mwenzako anayelala na mafaili mpaka chumbani tunaona matokeo yake frustrations haziishi, wewe unasomea wapi vitabu vyote hivyo isije kuwa chumbani?.

Anyway nimeipenda hii comment yako
"Kama Mtanzania ninayejiandaa kwa majukumu muhimu ya kitaifa nimekuwa nikipenda kupata maarifa Zaidi"
Tuko nyuma yako kwenye kufanikisha majukumu hayo ili mradi isiwe ni "kwa msaada was watu wa Marekani".
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Du!. Zitto wewe kiboko!. Mbona vitabu vingi sana, unapata muda kuvisoma vyote saa ngapi?.
Mwenzako analala na mafiles wewe si utakuwa unalala na vitabu?. Kama unalala na vitabu, jee unapata muda wa kulala na 'kulala'?.

P
Swali zuri sana. mimi pia ni msomaji mzuri wa vitabu. kuna wakati nilikaribishwa kutembelea familia moja ya wazungu huko ughaibuni. aliyenikaribisha ni bwana. mama akaandaa chakula, ambapo tulikuwa tunaongea hili na lile wakati wa kula. mama aliniuliza maswali mengi sana, kuhusu Tanzania, kuhusu vitabu, nk. sasa kuhusu vitabu tulishirikishana vitabu alivyosoma akavipenda na mimi nikamweleza nilivyovipenda. kuna kauli moja alitoa: Haamini kama mtu anaweza kuwa mtu na asisome vitabu. na kwa kuwa yuko bize sana (alikuwa mwanafunzi wa PhD licha ya kuwa mama wa mtoto mmoja na pia ni mke) ametenga muda wa kusoma vitabu vyake ni muda ule anakwenda kulala. kuna taa ya kusomea ipo kando ya kitanda (rejea mafaili!!). Baada ya kuachana naye alinipatia novel tatu za mwandishi ambaye nilisema nilimpenda sana baada ya kusoma novel yake moja tu (Life before Man ya Margareth Atwood)

lakini pia nimeona katika viwanja vya ndege wakati wa kusubiri kupanda ndege (boarding), wenzetu utakuta kila mmoja ana kitabu chake. sisi tupo tupo tu tunang'aa macho. ukiwa msomaji wa vitabu hutakosa muda wa kusoma. utakuwa na kitabu chako kwenye begi na utakisoma wakati unasubiri appointment kwenye maofisi, wakati upo hospitali unasubiri fomu ya bima, wakati unasubiri kuingia kwa daktari, wakati unasubiri vipimo, wakati unasubiri majibu, au kwenye mwendokasi (kama umepata siti), yaani muda wa kusoma upo mwingi sana tu, Pasco. ushindwe wewe tu kusoma vitabu, au huna interest!
 
Uongo huo , unapata mda sangapi kushugulikia kero za watu wako ??
Ndio maana kero za kgm haziishi
kwa kauli yako, unachomaanisha ni kwamba:
1) Kwako wewe Kusoma vitabu ni kupoteza muda
2) wewe husomi vitabu na hupendi haswa
3) Hujui maana ya kusoma vitabu na umuhimu wake

Kinyume na unavyofikiria, Ili uweze kutoa mchango muhimu zaidi katika jamii, inapendeza ukiwa msomaji wa vitabu. Maana ya kusoma vitabu ni kwamba unakuwa na akili pana zaidi. anayesoma vitabu vya waandishi wazuri, ni kama kuishi maisha mara tatu au zaidi, tena katika nchi mbalimbali. fikiria wewe kama kwa hayo unayoyajua sasa, kama ungebaki na akili hiyo hiyo lakini ukarejeshwa umri mdogo uanze upya, bila shaka utaamua baadhi ya mambo tofauti na ulivyofanya mwanzo. vitabu vinakupa fursa ya kuishi maisha mara nyingi bila na kujifunza kwa makosa ya wengine.
 
Hongera sana Zitto, katika list hiyo nimeweza kusoma vitabu vyote vya musiba pekee, hivyo vingine ndo navisikia leo,
Mwaka jana nilipewa zawadi na mkabulu ila Kitabu ni kizito hata nimeshindwa kufungua page ya kwanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Enemy of the people
1546269341808.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefurahi umemsoma Chimamanda Ngozi. Kuna kitabu chake nadhani ni Hibiscus anapoongelea kuhusu vita ya Biafra na bar nyingi zilizoitwa Tanzania bar. Kwetu kijijini tulikuwa na Biafra Bar. Big up.

Mimi nasoma vitabu vya kizee siyo political vya Catherine Cookson na Dickens, Great expectation ndo nimekirudia mara ya tatu. I never stop reading that book.
Kwa wewe inabidi usome hivyo ulivyovitaja maana unajijenga kisiasa. Wengine sisi muda umeisha.
Dickens nilimsoma ktk David Copperfield. Mwaka kesho ntamalizia hiyo Great expectation.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mheshimiwa Zitto Mimi kwa mwaka huu mzima nimesoma Vitabu vyangu hivi Saba ( 7 ) tu hadi vimenichanganya:

1. The whereabout of Afro American Hero Ben Eight
2. Why Bombardier and Dreamliner in Africa
3. The relationship between Cashew nut and Soldiers in Africa
4. Remembrance of Akwilina Akwilina in Africa
5. Why is it so difficult for an African Chemist to travel abroad and overseas?
6. The love of promoting and demoting in Africa
7. Why Infrastructure development is more important than Agriculture, Education and People's welfare in Africa?


Ukivihitaji sema nikuletee uvisome pia kwani vina Madini mengi sana tu.
Ongezea:
8) How to raise the National Payroll without new empoyees and without increasing salaries
9) How to raise the price of sugar while appearing to lower it
10) How to make people cultivate with their teeth
11) How to get people to praise you while you kick them
 
Indeed, Zitto is a very inspirational young politician. His extensive reading is evident in his ability to engage in reflective and independent thinking; something most politicians in the country lack.

But I would challenge Hon. Zittto to reveal his true ideological inclination (and economic school of thought). Though Zitto invariably supports free market economy, he is a self-proclaimed socialist.

I consider socialism a flawed political/economic theory because it advocates for social ownership of the means of production and distribution. As a rule of thumb, socialism is obsessed with wealth redistribution rather than wealth creation and therefore it lacks incentives towards creativity and innovation.

Certainly this is not the path we wish one of our high potential leaders to follow.

Though book reading is healthy, what counts most is the way the central idea and theme of the books shape the reader.


@Zitto na ACT huwa wanasimamia democratic socialism. Unless mwenyewe aeleze si yupo hapa na katika uzi huu naona anajibu badhi ya post.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom