Vita ya kiteknolojia ya Marekani inaweka shinikizo kwa biashara zake yenyewe

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111421247647.jpg

Kampuni kubwa ya simu ya Marekani, Apple, inapanga kutoa punguzo la bei la yuan 700, sawa na dola za kimarekani 103 kwa simu zake zote za iPhone 14 Pro zinazouzwa nchini China. Hii ni kwa mujibu wa waraka wa ndani wa SUNPIE, wakala maalum wa kampuni ya Apple nchini China. Na katika baadhi ya majukwaa ya biashara mtandaoni kama JD.com, bei ya simu hizo inaweza kupunguzwa kwa yuan 800.

Kwa mujibu wa jarida la Forbes, punguzo la bei linakuja siku chache baada ya kampuni hiyo kubwa ya teknolojia ya Marekani kutoa ripoti ya fedha kwa robo ya mwisho ya mwaka 2022, ambayo inaonyesha kuwa, kutokana na mauzo hafifu ya iPhones, ambayo ni chanzo kikubwa cha mapato cha kampuni hiyo, Apple ilipata faida ya dola za kimarekani bilioni 117.2 katika robo ya mwaka wa fedha inayomalizikia Desemba 25, ikiwa ni chini kwa asilimia 5 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2021, na ni mara ya kwanza kwa faida ya kampuni hiyo kushuka tangu mwaka 2019.

Kwa kuwa punguzo la bei mara nyingi hutumika kama mbinu ya uhakika ya kuongeza mauzo, mpango wa Apple nchini China safari hii unaonekana kama juhudi zake na kuongeza ushindani wake katika wakati ambao ukuaji wa mauzo ya simu janja umeanza kushuka kutokana na ushindani mkali katika soko.

Ni wazi kuwa kampuni ya Apple imepitia wakati mgumu sana mwaka 2022, kwa mauzo yake kuwa ya chini zaidi tangu mwaka 2008 kwa kupoteza asilimia 27. Mauzo hafifu yametokana na mahitaji ya iPhone 14 kuwa ya chini kuliko matarajio ya wawekezaji, na pia kushuka kwa mauzo ya simu janja duniani huenda kukachukua nafasi katika mauzo hafifu ya iPhone. Mwaka jana, mauzo ya simu janja duniani yalishuka kwa asilimia 11.3 ikilinganishwa na mwaka 2021 kwa uniti bilioni 1.21, na kuwa kiwango cha chini zaidi katika mwongo mmoja.

Hata hivyo, ni muhimu kuweka wazi kuwa, soko la simu janja za teknolojia ya juu bado liliendelea kukua mwaka jana. Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa, wakati mauzo ya bidhaa za kampuni ya Apple yakishuka, chapa nyingine za simu kama Huawei, Samsung, Vivo, na Xioami zilishuhudia mauzo makubwa.

Wakati China ikiendelea kuwa soko kubwa la simu janja na bidhaa nyingine za kielektroniki, mwelekeo unaokua ni kwamba, kiasi na fursa za mnyonyoro wa kiviwanda nchini China unaziwezesha kampuni za China kuboresha ushindani wao, hivyo kampuni kubwa za teknolojia za Marekani kama Apple zitakabiliwa na changamoto ya soko kubwa la ushindani la China.

Mauzo ya bidhaa za Apple nchini China bado ni makubwa, na katika mwongo mmoja uliopita, Apple imeongeza uzalishaji wa bidhaa zake na upatikanaji nchini China, ikiwa ni matokeo ya wazi ya maendleo ya uchumi na teknolojia nchini China, na pia soko kubwa la watumiaji. Mafanikio ya kampuni ya Apple katika soko la China yamechochewa na kuongezeka kwa mahitaji kutoka kwa watumiaji wa China, huku mnyororo wa ugavi nchini humo ukipelekea maendeleo ya kasi ya uvumbuzi wa kiteknolojia na utafiti wa soko katika kampuni za China.

Kwa mtazamo huo, soko la China na mnyororo wa ugavi wa China ni muhimu kama kampuni ya Apple inataka kuboresha ushindani wake. Lakini, kama Marekani itaendelea kuongeza kile kinachoitwa “msukumo wa kutengana”, ni wazi kuwa hatua hiyo itaathiri maendeleo ya baadaye ya kampuni ya Apple.

Jaribio la Marekani la kuingiza siasa katika mnyororo wa ugavi na uzalishaji chini ya msukumo huo wa kutengana umeleta athati hasi kwa biashara nchini humo. Vikwazo vya kiteknolojia vilivyowekwa na Marekani dhidi ya China sio tu vimeongeza ushindani kati ya kampuni za Marekani, bali pia kudhoofisha ushindani wa bidhaa za teknolojia za nchini Marekani katika soko la China, ikilinganishwa na bidhaa zinazotoka nchi za Jpan, Korea Kusini na bara la Ulaya.

Zaidi ya yote, jaribio kama hilo halitabadilisha ukweli kuwa, soko kubwa la watumiaji wa bidhaa za kielektroniki na bidhaa nyingine za teknolojia ya juu wako nchini China. Hivyo, jaribio hili halitazuia kukua kwa uchumi na teknolojia ya China kama ambavyo wanasiasa wa Marekani wanataka, na yeyote atakayekiuka sheria za kiuchumi, hatimaye atameza kidonge kichungu!
 
Sizani kama hii taarifa ina ukweli.. yaani iphone ipate faida ya tril 224 na hapo wamepata faida kidogo...

Hii taarifa haiba ukwel hata
 
Sizani kama hii taarifa ina ukweli.. yaani iphone ipate faida ya tril 224 na hapo wamepata faida kidogo...
Wanapiga mafaida mengi sana. Huduma zao tu za mtandaoni zimeingiza faida ya tillions of money.

Naona computer ndizo zinawaingizia faida kidogo zaidi. Ila simu na huduma zao nyingine zina make profits nyingi sana.
 
Back
Top Bottom