Vita vya kuviziana, mwenye uwezo wa kumvika paka kengele bado hajazaliwa

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Maamuzi mengi ya serikali yanapitia kwenye Baraza la Mawaziri chini ya Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Uwajibikaji wa serikali unamlenga waziri mkuu kwa kuwa ndiye msimamizi mkuu wa kazi zote za serikali,na waziri Mkuu huyu atapokea maelekezo toka kwa Rais na si vinginevyo.

Drama inaanzia pale Mwenezi wa chama anapompa msimamizi wa maelekezo ya Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa chama siku Sita kutatua migogoro ya Ardhi kupitia wizara tatu ambayo wizara moja Iko chini ya ofisi ya Rais ambaye ndiye mwenye dhamana ya kupeleka jina la Mwenezi kwenye Halmashauri kuu.

Hii ni zaidi ya drama,anayetafutwa kuangushiwa zigo ndiye mbuzi wa kafara.

Kilichotokea kwa Lowassa Sasa kinajirudia kwa njia nyingine yenye mfanano wa maudhui. Ndiyo maana nasema kama Kuna udhaifu katika serikali,Rais anawajibika Majaliwa atabaki kuwa mbuzi wa kafara tu uzoefu unatukumbusha.

Ndani ya CCM wa kumvika paka kengele bado HAJAZALIWA,rudini kwa wananchi kujua matatizo yao na suluhisho lake, Ngorongoro na Msomera hiyo ni mmoja lakini msafara wa mamba kenge wamo kibao.
 
Screenshot_20231102-112721.png
 
Bado hatujafikia level ya mtindio wa ubongo ukitumwa maji unaleta sigara. Hoja yako Mr. Dudumizi inatofautiana na mada hapo juu
 
Bado hatujafikia level ya mtindio wa ubongo ukitumwa maji unaleta sigara. Hoja yako Mr. Dudumizi inatofautiana na mada hapo juu
Hongera, hata mm Nimemjibu kumrudisha ndani ya chama na Serikali yake.
 
Maamuzi mengi ya serikali yanapitia kwenye Baraza la Mawaziri chini ya Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Uwajibikaji wa serikali unamlenga waziri mkuu kwa kuwa ndiye msimamizi mkuu wa kazi zote za serikali,na waziri Mkuu huyu atapokea maelekezo toka kwa Rais na si vinginevyo.

Drama inaanzia pale Mwenezi wa chama anapompa msimamizi wa maelekezo ya Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa chama siku Sita kutatua migogoro ya Ardhi kupitia wizara tatu ambayo wizara moja Iko chini ya ofisi ya Rais ambaye ndiye mwenye dhamana ya kupeleka jina la Mwenezi kwenye Halmashauri kuu.

Hii ni zaidi ya drama,anayetafutwa kuangushiwa zigo ndiye mbuzi wa kafara.

Kilichotokea kwa Lowassa Sasa kinajirudia kwa njia nyingine yenye mfanano wa maudhui. Ndiyo maana nasema kama Kuna udhaifu katika serikali,Rais anawajibika Majaliwa atabaki kuwa mbuzi wa kafara tu uzoefu unatukumbusha.

Ndani ya CCM wa kumvika paka kengele bado HAJAZALIWA,rudini kwa wananchi kujua matatizo yao na suluhisho lake, Ngorongoro na Msomera hiyo ni mmoja lakini msafara wa mamba kenge wamo kibao.
kama hajatokana na ccm may be anaweza akasema anawajibika kwa Rais Pekee, na nina hakika hata maoni na ushauri wako angeupokea na kuufanyia kazi....

ila kama anatokana na ccm huyo waziri mkuu lakini pia mtendaji mwingine yeyote serikalini anawajibika serikalini barabara na kuripoti chamani ili chama kiweze kupata taarifa hiyo na fursa ya kurudisha fedback kwa wanaCCM walio chagua serikali hiyo.....

There is no escape root kwa waziri mkuu kuwajibika serikalini na kuripoti chamani kwa katibu wa itikadi na uenezi,
no escape root at all....
 
Back
Top Bottom