Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,502
- 16,715
Rasi Donald Trump wa Marekani anajaribu kadri iwezekanavyo bidhaa kutoka nje ziwe ghali kiasi kwamba wananchi wake wasizipate kwa urahisi ijapokuwa kwake hazipo.Na kinyume chake.
Mu'az amesimulia: Nimemsikia Mtume wa Allah akisema" Mbaya ni yule anayelundika bidhaa na kuifanya iwe adimu. Kama Allah akifanya bidhaa kuwa rahisi, yeye anachukia na kama Allah akiifanya kuwa ghali, anafurahi, (Razin, Baihaqi).
Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao) Ambao wanapojipimia kwa watu hupokea (kipimo) kamili. Lakini wanapowapimia kwa (kipimo cha) vibaba au mizani (au vinginevyo), wao hupunguza. (83:1-3).
Na timizeni kipimo mpimapo; na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni wema kwenu na bora mwishoni (kwake). (17:35).
Anas amesimulia kuwa wakati mmoja katika wakati wa Mtume wa Allah bei ya vitu ilikuwa ghali. Wakamuomba Mtume: Ewe mtume wa Allah panga bei kwa nafuu yetu. Mtume wa Allah akajibu: Hakika Allah ndiye anayemiliki bei, anapunguza, anatoa kwa wingi, anatoa riziki, na ninapendelea sana nikutane na Bwana wangu katika hali ambayo hapana yeyote kati yenu atakayenifanya niwe na dhima juu ya damu (iliyomwagika kwa sababu yangu) au mali (aliyopunjwa kwa sababu yangu)! (Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah).
Hadithi hii inatupa fundisho kubwa kuwa Uislamu kama usivyoruhusu kukandamizwa na kudhulumiwa mnunuzi ndivyo hivyo hivyo isivyoruhusu kukandamizwa kwa mchuuzi au muuzaji.
Mtume (s.a.w.) akiwa kiongozi mkuu wa Serikali ya Kiislamu, hakuthubutu kutumia madaraka hayo na kuingilia haki za wafanya biashara waliopewa na Allah (s.w.).
Jibu lake kwa namna nyingine lilikuwa "anayepanga bei ni Allah (s.w.) kwa bei". Kutokana na hadithi hii hapana yeyote mwenye haki ya kukaa chini na kumpangia mfanya biashara bei iliyo kinyume na ile iliyojitokeza yenyewe sokoni. Kinachotakiwa kifanywe na nguvu za dola ni kutokomeza njama zote za ulanguzi na vikwazo vyote vya uchumi. Kisha kuwaacha huru wafanya biashara wauze bidhaa zao kwa bei halisi inayokubaliwa katika soko huru.
Mu'az amesimulia: Nimemsikia Mtume wa Allah akisema" Mbaya ni yule anayelundika bidhaa na kuifanya iwe adimu. Kama Allah akifanya bidhaa kuwa rahisi, yeye anachukia na kama Allah akiifanya kuwa ghali, anafurahi, (Razin, Baihaqi).
Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao) Ambao wanapojipimia kwa watu hupokea (kipimo) kamili. Lakini wanapowapimia kwa (kipimo cha) vibaba au mizani (au vinginevyo), wao hupunguza. (83:1-3).
Na timizeni kipimo mpimapo; na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni wema kwenu na bora mwishoni (kwake). (17:35).
Anas amesimulia kuwa wakati mmoja katika wakati wa Mtume wa Allah bei ya vitu ilikuwa ghali. Wakamuomba Mtume: Ewe mtume wa Allah panga bei kwa nafuu yetu. Mtume wa Allah akajibu: Hakika Allah ndiye anayemiliki bei, anapunguza, anatoa kwa wingi, anatoa riziki, na ninapendelea sana nikutane na Bwana wangu katika hali ambayo hapana yeyote kati yenu atakayenifanya niwe na dhima juu ya damu (iliyomwagika kwa sababu yangu) au mali (aliyopunjwa kwa sababu yangu)! (Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah).
Hadithi hii inatupa fundisho kubwa kuwa Uislamu kama usivyoruhusu kukandamizwa na kudhulumiwa mnunuzi ndivyo hivyo hivyo isivyoruhusu kukandamizwa kwa mchuuzi au muuzaji.
Mtume (s.a.w.) akiwa kiongozi mkuu wa Serikali ya Kiislamu, hakuthubutu kutumia madaraka hayo na kuingilia haki za wafanya biashara waliopewa na Allah (s.w.).
Jibu lake kwa namna nyingine lilikuwa "anayepanga bei ni Allah (s.w.) kwa bei". Kutokana na hadithi hii hapana yeyote mwenye haki ya kukaa chini na kumpangia mfanya biashara bei iliyo kinyume na ile iliyojitokeza yenyewe sokoni. Kinachotakiwa kifanywe na nguvu za dola ni kutokomeza njama zote za ulanguzi na vikwazo vyote vya uchumi. Kisha kuwaacha huru wafanya biashara wauze bidhaa zao kwa bei halisi inayokubaliwa katika soko huru.