Vita Vya Iran: Iran Ina Nuclear

Vita Vya Iran: Iran Ina Nuclear

Kama ina Nuclear basi Marekani alikuwa sahihi kumshambulia na hivyo sisi tuliokuwa tukimuona Marekani mkorofi inabidi tuchutame.
 
Hizi ni sababu tu....

Note. Tuna make move ya Venezuela tunakamata reserve kubwa ya mafuta... Then Iran ambae anasupply mafuta kwa bei rahisi sana na kwa zaidi ya asilimia 80 kwa Mchina.

Tunamuumiza mchina for the long run... Sisi tutaumia kwa muda kidogo ila baada ya hapo ni shangwe. SMART na inahitaji akili ya ziada.
 
Kama ina Nuclear basi Marekani alikuwa sahihi kumshambulia na hivyo sisi tuliokuwa tukimuona Marekani mkorofi inabidi tuchutame.
Mbona Pakistan ana nuclear hajavamiwa? Vipi Israel ina nuclear mbona haijavamiwa na USA? kuwa na nuclear whether bomu au nishati ni haki ya wote haiwezekani mtu mmoja ajipe uhalali na wengine inakua haramu
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Mbona Pakistan ana nuclear hajavamiwa? Vipi Israel ina nuclear mbona haijavamiwa na USA? kuwa na nuclear whether bomu au nishati ni haki ya wote haiwezekani mtu mmoja ajipe uhalali na wengine inakua haramu
Kuna mataifa ambayo ni Nuclear state

Lakini sio mataifa yote yalisaini huo mkataba, hata N. Korea alisaini huo mkataba lakini alikuja kujitoa.
 
Kama ina Nuclear basi Marekani alikuwa sahihi kumshambulia na hivyo sisi tuliokuwa tukimuona Marekani mkorofi inabidi tuchutame.
Kwanini awe sahihi kumshambulia wakati yeye Marekani pia anamiliki?

Yaani wewe uwe na haki ya kumiliki nyuklia halafu mwenzako asiwe na haki hiyo hiyo?

Kama ni nchi iliyopaswa kupogwa marufuku kutokumiliki nyuklia basi ni Marekani kwasababu yeye ndiye nchi pekee iliyowahi kutumia nyuklia dhidi ya raia wasio na hatia.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Waliingia kwenye mkataba wa kutomiliki

So yeah ni kosa
Yaani waliingia na nani?

Kwanini waingie mkataba wa kutomiliki wakati uranium ya kurutubisha nishati ya nyuklia wanayo ya kutosha?

Yaani nchi iingie mkataba wa kutomiliki nyuklia halafu wakati huo huo ijipe tabu ya kutengeneza kwa siri ili iweje?
 
Kwanini awe sahihi kumshambulia wakati yeye Marekani pia anamiliki?

Yaani wewe uwe na haki ya kumiliki nyuklia halafu mwenzako asiwe na haki hiyo hiyo?

Kama ni nchi iliyopaswa kupogwa marufuku kutokumiliki nyuklia basi ni Marekani kwasababu yeye ndiye nchi pekee iliyowahi kutumia nyuklia dhidi ya raia wasio na hatia.
Marekani, China, Urusi, Ufaransa pamoja na Uingereza hayo ni mataifa ambayo tangu mwanzo yalikuwa yana miliki Nuclear kabla hata ya 1967 ambapo huo mkataba kusainiwa.

Makubaliano ya huo mkataba yalikuwa ni kuzuia uongezekaji wa silaha za Nuclear, hivyo wakaafikiana kuwa technology ya nuclear itumike katika kuzalisha nuclear kwa ajili ya matumizi salama kama maswala ya nishati na mambo mengine ambayo ni useful kijamii.

Mtataba haukuwa ni kuondoa silaha za Nuclear kwa nchi ambazo tayari zinamiliki, bali ilikuwa ni Nchi zisizokuwa na silaha (kama Iran) zilikubali kutotengeneza au kupata silaha za nyuklia.

Na zile nchi ambazo zilikuwa tayari zinamiliki hizo silaha (Marekani, UK, france, China na Urusi) ziliruhusiwa kuendelea kubaki na nuclear kwasababu walikuwa nazo kabla ya 1967 lakini zilikubali kufanya mazungumzo ya kupunguza na mwisshowe kuziondoa kabisa.

Mapungufu ya huu mkataba yapo eneo hili

Hayakuweka muda rasmi wa deadline kwa kila nchi kufikia ukomo wa hayo matumizi ya nuclear ili kuhakikisha kuwa pindi tu baada ya kufika tarehe hiyo basi kila nchi iwe haina silaha za nuclear.

Hii inafanya hata wakiulizwa wapate majibu mepesi tu kuwa tunaendelea kupunguza kwasababu hawabanwi na sehemu yeyote kuwa wamevuka ukomo wa muda uliowekwa.
 
Yaani waliingia na nani?

Kwanini waingie mkataba wa kutomiliki wakati uranium ya kurutubisha nishati ya nyuklia wanayo ya kutosha?

Yaani nchi iingie mkataba wa kutomiliki nyuklia halafu wakati huo huo ijipe tabu ya kutengeneza kwa siri ili iweje?
Sababu haikuwa sio kwakuwa wewe una Uranium

Waliangalia athari za hizo silaha zingeweza kuleta maangamizi makubwa endapo tu mtu yeyote akawa na uwezo wa kumiliki.

Kumbuka huo ni mkataba ambao kila mtu ali consent.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom