Visasi vya JK kwa watu wa Arusha? Ahamishia mkutano wa wakuu wa EAC Dar

visasi ni tabia ya kikwete, unajua waliko walio ingia kwenye ligi ya urais naye kutoka ccm??? Ni mwandosya tu yupo lakini baada ya kuonywa huko mbeya!!!!. Waulize akina sumaye, salim ahmed salim. Je waliowaunga mkono sumaye na salim? Nina ushahidi wa kada mmoja aitwaye nicodemus banduka alikuwa mkuu wa mkoa wa lindi 2005.

Banduka alimuunga mkono sumaye kilichompata akisimulia machozi yanatiririka. Nilikuwepo wakati kikwete alipokataa kumpa hata mkono mkuu wa mkoa wakati aliporudi lindi kushukuru. Nilikuwepo wakati anawaadressi mwenyekiti ccm mkoa, wilaya, wakuu wa wilaya na kumwacha mkuu wa mkoa.

Ninakumbuka alivyomleta sadick meck sadick kama mkuu wa mkoa bila kumpa taarifa banduka. Banduka alinyang'anywa gari njiani. Afisa usalama wa mkoa alimtoa kwenye nyumba ghafla.
Banduka alitoroka usiku kuepuka aibu ya ghafla.

Hata mitandao iliyopo ni kwa ajili ya kikwete. Mtandao wake ni kwa ajili ya kuendelea kuwaadhibu wabaya wake tena walio katika chama chake. Kauli za uv ccm bagamoyo na kwingine na matusi kwa wazee wa chama chanzo ni visasi vyake

hafai uongozi wowote hata katibu kata = kikwete ni mtu hatari.

umenishtua aisee, bora mungu amgeuze trekta tu wakamlimie mashambani huko!
 
[/B]


that was too sad ..kweli Banduka alidhalilishwa sana san..hata alipokuja moshi kuna mtu alimruka kumpa mkono pale KIA ..huku anacheka akijifanya hamuoni na kuendelea kupiga soga na wengine kwenye foleni ya mapokezi...unaweza kupatwa na kihoro...imefikia mahali ukijuwa picha hazipandi akija mahali unasepa...

Nakumbuka mkuu wa mkoa wa morogoro MASHISHANGA yeye alistaafu hata kabla kikwete hajaapishwa akijuwa moto ukiokuwa unamfuata...

KINGINE kuhusu Arusha mnaweza kuwasingizia CHADEMA ..lakini mjuwe pia kuzorota kwa mahusiano na Lowassa ni sababu nyingine pia...
Mbona Daniel Ole Njoolay bado ni RC? Ni nani asiye na visasi kwenye SIASA? Mnakumbuka Mkapa alichokifanya kwa Imran Kombe? Mnakumbuka wale makamishna waliokuwa pale makao makuu ya polisi walichofanyiwa?
 
Muulizeni JV Mwapachu kama maandalizi ya mkutano huu yalifanywa na IKULU yetu. Watu wanatafuta hela ya kustaafia ninyi mnamkomalia JK wetu!
 
****** jaman ******....!! wakenya watatuzidi kwa kila kitu, ndo maana wakenya asaivi wanajenga uwanja wa ndege wa kimataifa karibu na ule wa KIA ili wageni waumwage kabisa uwanja wetu, si apinduliwe tu huyu jaman?
 
Hili la mkutano kufanyika Dar badala ya Arusha ni vigumu kulihusisha na ajenda binafsi ya Jakaya. Mikutano ya Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki huwa inafanyika katika nchi mbalimbali na kwa mara ya mwisho nakumbuka mkutano kama huu ulifanyika Bujumbura. Summit moja kwa mwaka ambayo ni ya kawaida (Ordinary) ni lazima ifanyike Arusha yalipo Makao Makuu ya Jumuia. Hii ya sasa si ya kawaida (Extra ordinary) na hivyo inaweza kufanyika sehemu yoyote kama nchi inayoomba kuhost itachukua sehemu kubwa ya gharama. Hii inaongeza visibility ya Jumuia kwa watu wa Afrika Mashariki. Kuna mmoja ametolea mfano wa East Africa Legislative Assembly ambao kila mkutano huwa wanazunguka katika miji tofauti ya Jumuia. Siupendi sana huu mfano kwani binafsi nadhani kitendo cha EALA hakinufaishi jumuia bali ni kutaka kuvuja fedha za Jumuia bila sababu. Kikao hiki cha sasa kimefanyika Dar es Salaam kwa sababu kulikuwa na Mkutano mwingine wa Uwekezaji wa Afrika ambao wakuu wa nchi walikuwa wanahudhuria na hivyo ikaonekana ni vyema ikaungana. Ndiyo maana napata kigugumizi kuhusisha suala hili na ubaguzi wa wazi wa JK. Hata hivyo, anything is possible.
 
****** jaman ******....!! wakenya watatuzidi kwa kila kitu, ndo maana wakenya asaivi wanajenga uwanja wa ndege wa kimataifa karibu na ule wa KIA ili wageni waumwage kabisa uwanja wetu, si apinduliwe tu huyu jaman?

matusi hayasaidii, na hasira za mkisi............?
 
Mwanakijiji na wewe unaingia kwenye mtego huu??? Kwamba ni kisasi?? This is too low. Inamaana Arusha ndio sehem pekee nchi hii panapostahili mikutano yote? Na mikutano haijawahi kufanyikia DSM? Hizi ni hoja za kitoto

You have placed yourself too low. Arusha is the Hq of EAC it is a fact. Arusha has seen uncalled for violence and killings by JK villainous govt. The guilty conscious of what he has done to AR people is pushing JK behavior to abnormality. He is now interfering the operations of EAC as if EAC was his family undertaking. He is scoring negatively because of his previous stupid decisions; I think we have to tune ourselves to more erratic decisions.
 
You have placed yourself too low. Arusha is the Hq of EAC it is a fact. Arusha has seen uncalled for violence and killings by JK villainous govt. The guilty conscious of what he has done to AR people is pushing JK behavior to abnormality. He is now interfering the operations of EAC as if EAC was his family undertaking. He is scoring negatively because of his previous stupid decisions; I think we have to tune ourselves to more erratic decisions.
Mnaweza kuendelea kumchukia kwa mambo mengi mengine. Hili la mkutano huu si lake. Na kwa EAC ya sasa JK hana nia wala uwezo wa kuwaburuza akina Kagame, Nkurunzinza,
 
mbona daniel ole njoolay bado ni rc? Ni nani asiye na visasi kwenye siasa? Mnakumbuka mkapa alichokifanya kwa imran kombe? Mnakumbuka wale makamishna waliokuwa pale makao makuu ya polisi walichofanyiwa?

mnafiki mara zote humuacha aliyekuwa adui mmoja asiyekuwa na madhara ..na kumfanyia monitoring ili kuhalalisha hatua ya kuwatesa wengine .....ndio maana watu kama njolay na nagu wakapona ...ukiacha wachache ambao walienda kutubu binafsi kwa kikwete .........

ishu ya polisi na imran kombe inahusiana na usalama wa taifa ..wanazo taratibu zao za kazi na hatua stahiki kwa anayekiuka ...kuwa extradicted ni moja ya hatua ya kuchukuwa kwa wanaovujisha siri au kushirikiana na wahalifu ..wamaojuwa ishu kama ya kombe wamenielewa!!..ilibidi afe kwa sheria na taratibu za kiasikari....ndio maana alikuwa yuko mbioni kutoroka kwa kuwa alijuwa kosa alilofanya lina adhabu gani kwenye system
 
Mkuu Phillemon Mikael, asumption ni kitu kinachoruhusiwa hata kama asumption hiyo is based on a wrong premes. Ni kweli Arusha ndio makao makuu ya EAC na makao makuu ya kudumu ya EAC yanajengwa pale jirani na ICC, hivyo hakuna tena discusion makao makuu yawe wapi.

Kenya haifanyi tena lobbying kuhodhi makao makuu ya EAC bali wanapiga ndogo ndogo achives za ICTR zihamishiwe Nairobi na hapa lengo sio kuhifadhi achives hizo, bali the life time stream of money toka UN pamoja na kutrap all future research funds on Rwandan genocide.

Mikutano ya EAC, huamuliwa kwenye vikao ifanyike wapi, sio lazima ifanyike Arusha, kama lilivyo bunge la EALA, kikao kinafanyika nchi yoyote ya jumuiya hii na ni host nation itaamua mkutano ufanyike mji gani.

JK akiamua kuikomoa Arusha, atamteu Dr. Burian, RC wa Arusha kama alivyomteau mkuu wa mkoa wa Mbeya baada ya kubwagwa. Subirini tuone!.

Nimeipenda, Shemeji RC Arusha
 
Mnaweza kuendelea kumchukia kwa mambo mengi mengine. Hili la mkutano huu si lake. Na kwa EAC ya sasa JK hana nia wala uwezo wa kuwaburuza akina Kagame, Nkurunzinza,

hAO MNAOWATAJA ..KAGAME NA NKURUZINZA NDIO WASAIDIZI WAO WALIOKUWA ARUSHA KUANDAAA MKUTANO HUU WALIKUWA WAKIPINGANA NA WATU WA SERIKALI YETU KULETA MKUTANO DAR...KWA KUWA UZOEFU UMEONESHA WANAPATA USUMBUFU MKUBWA WAKIWA DAR ,...NA HATA WAO WANAONA USUMBUFU WANAOSABABISHA ..TOFAUTI NA WAKIWA ARUSHA......
KIUKWELI WALISHANGAA SANA KWA NINI SERIKALI ILIKUWA INAWABURUZA KUJA DAR..THAT IS INSIDE STORY ...ANAEWEZA KUPATA MUDA AONGEE NA WATU WA PROTOCAL WA HAYA MATAIFA WATAWAAMBIA,,,...
 
JK WENU KWELI....!! so si wa wote...wengine walie tu!

Nimesema WETU sio WENU. PM, nina kawaida ya kuamini sana mabandiko yako humu. Yule mmiliki wa sasa wa majengo ya MlimaniCity unakofanyika mkutano huu ni mhongaji mzuri sana. AICC wajiandae, waje kivingine kwenye soko hili. Vinginevyo itakufa kama akina NASACO na mabenki ya UMMA yalivyochinjiwa baharini.
 
Hana jipya huyu kashapoteza legitimacy ya kutuongoza WATANZANIA.....:director::director::director:
 
Watu mliopewa nafasi nyeti katika nchi lakini mnazitumia kwa maslahi binafsi.
Mchana mnaripoti ofisi nyeti za serikali usiku mnaripoti Chadema. Tunakumbuka thread yako ya matokeo ya uchaguzi.
Mbona huwa hamtumpi na nyeti za hao mafisadi wa huko kwenu wanaoliangamiza Taifa.
Hao akina Banduka, Mashishanga na Mahawa mbona husemi walichokuwa wakikifanya mikoani kwao wakati Kikwete akienda kuomba kura za kupitishwa na CCM kutokana na maelekezo ya Sumaye!
Watu wazima kama ninyi mnakuja kuvipotosha vitoto vya vyuoni na kumeza msemayo!
Huna uzalendo bali chuki tu na kutaka Kikwete aonekani hafai kwa lolote!
PM unajulikana kwa chuki zako. Any way msubiri huyo mkatoliki mwenzio Magufuli kama ulivyomtabiria kuwa Raisi 2015.
Shame on you na miftna yako!
 
Hii sio kweli, lazima kuna sababu za msingi. Yeye kama yeye hawezi ghafla kubadilisha sehemu ya mkutano kwa kuwa kuna kamati ya maandalizi naye siyo mjumbe.Haiwezekani kabisa.

Kwani kwenye tume ya uchaguzi alikuwa mjumbe?........
 
Mwanakijiji na wewe unaingia kwenye mtego huu??? Kwamba ni kisasi?? This is too low. Inamaana Arusha ndio sehem pekee nchi hii panapostahili mikutano yote? Na mikutano haijawahi kufanyikia DSM? Hizi ni hoja za kitoto

Mkuu inawezekana mkutano huu umehamishiwa dar kwa nia njema!! Mimi na wewe hatujui... Lakini ukweli kuwa rais alitamka maneno kama haya kwenye kadamnasi inaleta walakini...

Kila siku tumekuwa tunasema saaaaana tu, JK, anatuhumiwa kuwa kilaza, lakini naamini tuhuma hizi zinathibitishwa sana na matendo yake!!!:A S 465::spy:
 
Ni dhahiri kuwa kuna siasa za visasi dhidi ya mji wa Arusha kunyang'anya fursa zake kiaina.Lakini kubwa kuliko yote ni hofu ya "mzee wa kaya" kuhusu mwamko wa kisiasa wa wakazi wa Arusha....... labda anadhani wanaweza kumuabisha mbele ya ugeni uliomjia. Lakini atambue hata akifanya kinyongo Arusha ndio makao makuu ya EAC.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom