Visasi vya JK kwa watu wa Arusha? Ahamishia mkutano wa wakuu wa EAC Dar

Mkuu imenichukua masaa 2 kutoka Mwenge kufika Millenium tower hapo kijitonyama. Hii traffic jam ni balaa hakuna tofauti na India. Nimemchukia sana ****** nilipokumbuka akisema kuongezeka kwa foleni na magari Dar ni sababu ya maendeleo yaliyoletwa na chama chake!!


Duuh!! Hiyo noma, bora kutembea kama ungekuwa unaishia Millenium tower!!!!!!!
 
.....Enzi JK akiipenda Arusha alikuwa akija almost kila weekend kwa safari binafs..ikiwemo kupumzika ngurdoto na dogo dogo zake .....lakini he has made a big U turn ...just kwa sababu za kisiasa...

hata alipoenda kutoa kamisheni za jeshi alitua na ndege monduli na kupaa moja kwa moja...hakuingia arusha ambapo si kawaida yake....

bado nawalaumu watu wa usalama....how does such personality enter the holy place------state house?
 
[/B]


that was too sad ..kweli Banduka alidhalilishwa sana san..hata alipokuja moshi kuna mtu alimruka kumpa mkono pale KIA ..huku anacheka akijifanya hamuoni na kuendelea kupiga soga na wengine kwenye foleni ya mapokezi...unaweza kupatwa na kihoro...imefikia mahali ukijuwa picha hazipandi akija mahali unasepa...

Nakumbuka mkuu wa mkoa wa morogoro MASHISHANGA yeye alistaafu hata kabla kikwete hajaapishwa akijuwa moto ukiokuwa unamfuata...

KINGINE kuhusu Arusha mnaweza kuwasingizia CHADEMA ..lakini mjuwe pia kuzorota kwa mahusiano na Lowassa ni sababu nyingine pia...

Ndugu Philemon
Huyu Banduka alijaribu kutuma Wazee wa CCM kwenda DSM kwa JK (Mwenyekiti CCM Mkoa Lindi na wengine) kuomba msamaha kwa kosa ambalo alikuwa hajui lakini Kikwete alicheka na kusema hana tatizo naye!!!!! Huyu ndiye Rais (smiling president) anayesifiwa.
Anayekataa kuombwa msamaha ni SHETANI. Tuombeni jamani tumevamiwa.
 

HOTUBA YA MWENYEKITI WA CCM TAIFA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KATIKA SHEREHE ZA
KUTIMIZA MIAKA 34 YA KUZALIWA KWA CCM
UWANJA WA JAMHURI, DODOMA
TAREHE 05 FEBRUARI, 2011


CCM Oyee!
Kidumu Chama Cha Mapinduzi!

Ndugu William Kusila; Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dodoma;
Ndugu Lt. Mst. Yusuf Makamba, Katibu Mkuu wa CCM;
Waheshimiwa Wabunge;
NduguViongozi mbalimbali mlioko hapa;
Ndugu Wana-CCM na
Ndugu Wananchi;



Utangulizi:
Naomba nianze kwa kuwashukuru wenyeji wetu, viongozi, wana-CCM na wananchi wa Dodoma kwa mapokezi mazuri na kwa maandalizi mazuri ya sherehe hii. Sherehe zimefana sana. Sisi sote ni mashahidi. Vile vile matembezi ya mshikamano yalikuwa mazuri ingawaje umbali ulikuwa mfupi kidogo. Safari ijayo tufikirie kuongeza umbali.



Utawala wa Sheria
Ndugu Wana-CCM na Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwaka 2010, nilidokeza taarifa ambazo vyombo vya usalama vinazo kuhusu mipango ya makusudi ya uvunjifu wa amani kwa kutumia njia ya migomo na maandamano. Niliwatanabaisha ndugu zangu kutambua njama hizo na kuepuka kushiriki katika maandamano au migomo ya aina hiyo. Wanaoandaa wana agenda yao ya kisiasa iliyojificha nyuma ya jambo linalotangulizwa kama sababu. Wanataka kujitengenezea mazingira ya ushindi mwaka 2015 kwa vurugu. Nilitahadharisha kuwa watu wajiepushe kugeuzwa mbuzi wa kafara kwa kuendeleza maslahi ya kisiasa ya watu fulani fulani.
Niliyoyasema yametokea Arusha na dalili zipo za mipango ya namna ile kuandaliwa kutokea sehemu nyingine hapa nchini. Napenda kurudia tena kuwasihi Watanzania wenzangu msiwasikilize wala kuwafuata wanasiasa hao. Wanawasakizia kwenye hatari ambayo mnaweza kuiepuka. Naomba muwakumbushe tena kuwa wanayo fursa Bungeni na kwenye majukwaa mbalimbali kutoa hoja zao badala ya kuwagombanisha nyinyi na vyombo vya dola. Niwaombe wanasiasa wenzangu kutumia fursa tele walizonazo badala ya njia ya uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha na mali za watu pamoja na kuharibu sifa ya nchi yetu.



Ndugu Viongozi, Wana-CCM Wenzangu na Wananchi Wenzangu;
Ukweli huu ndiyo uliotupatia ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2010 pamoja na vitimbi na mbinu chafu tulizofanyiwa na wapinzani wetu. Wakati mwingine haya yanayoendelea sasa ya vurugu zinazofanywa na wapinzani wetu ni hasira ya hasara waliyoipata, hasa wakikumbuka kiasi walichowekeza, pamoja na ubaya na hujuma mbalimbali walizotutendea bila ya mafanikio. Wanasahau Mola ndiye mtoaji. Akiandika kupata unapata.


Kwa nini tujisikie wanyonge baada ya kupata ushindi mnono kiasi hicho? Nadhani tunatishwa na kelele na propaganda za Chama fulani na Bwana fulani ambazo zinajenga hisia kama vile wako wengi sana na wamepata ushindi mkubwa sana hata kuliko CCM. Hilo si kweli, ingawaje safari hii wamepata viti vingi kuliko uchaguzi uliopita. Ukweli ni kwamba Chama hicho kimepata asilimia tisa tu ya viti vyote vya Majimbo.

Ndugu Wana-CCM na Ndugu Wananchi;
Miongoni mwa mambo mengine ambayo tutayafanya mwaka huu ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya nchi yetu kwa nia ya kuihuisha na hatimaye kuzaa Katiba mpya inayolingana na taifa lenye umri wa miaka hamsini na itakayotupeleka miaka 50 ijayo. Kiserikali matayarisho yanaendelea ya kupeleka Bungeni Mswada wa Sheria wa kuanzisha mchakato huo ikijumuisha kuundwa kwa Tume ya kuongoza mchakato huo.
Hata kama kusingekuwepo mapendekezo ya CUF, CHADEMA na wengineo ilikuwa ni dhamira yetu kufanya hivyo

Utawala wa Sheria
Ndugu Wana-CCM na Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwaka 2010, nilidokeza taarifa ambazo vyombo vya usalama vinazo kuhusu mipango ya makusudi ya uvunjifu wa amani kwa kutumia njia ya migomo na maandamano. Niliwatanabaisha ndugu zangu kutambua njama hizo na kuepuka kushiriki katika maandamano au migomo ya aina hiyo. Wanaoandaa wana agenda yao ya kisiasa iliyojificha nyuma ya jambo linalotangulizwa kama sababu. Wanataka kujitengenezea mazingira ya ushindi mwaka 2015 kwa vurugu. Nilitahadharisha kuwa watu wajiepushe kugeuzwa mbuzi wa kafara kwa kuendeleza maslahi ya kisiasa ya watu fulani fulani.
Niliyoyasema yametokea Arusha[wakati mwingine natamani kuhamisha shughuli na maofisi ya kimataifa pale] na dalili zipo za mipango ya namna ile kuandaliwa kutokea sehemu nyingine hapa nchini. Napenda kurudia tena kuwasihi Watanzania wenzangu msiwasikilize wala kuwafuata wanasiasa hao. Wanawasakizia kwenye hatari ambayo mnaweza kuiepuka. Naomba muwakumbushe tena kuwa wanayo fursa Bungeni na kwenye majukwaa mbalimbali kutoa hoja zao badala ya kuwagombanisha nyinyi na vyombo vya dola. Niwaombe wanasiasa wenzangu kutumia fursa tele walizonazo badala ya njia ya uvunjifu wa amani na kuhatarisha maisha na mali za watu pamoja na kuharibu sifa ya nchi yetu



Asanteni kwa kunisikiliza!

Kidumu Chama cha Mapinduzi!
Hizi zinaonekana ni jazba na hasira za kushindwa kwa CCM kwenye jimbo la Arusha


huyu bwana kwenda ikulu anaita kupata tehetehetehetehete!!!!!
 
Comment kama hii inatoka kwa msomi na ambaye ni mshauri wa Raisi. Tuna safari ndefu sana.....

Jamani kama huyu ni mshauri wa rais yumo humu janvini kwanini hawamwambii bosi wao kuwa JF ni ya kila mwenye nia njema na Tanzania na wao pia wamo humu na sio ya chadema kama consultants wao wanavyowambia. Acheni unafiki hiyo njaa yenu itawafikisha pabaya. Semeni kweli tupu kwani msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
 
Ndugu Philemon
Huyu Banduka alijaribu kutuma Wazee wa CCM kwenda DSM kwa JK (Mwenyekiti CCM Mkoa Lindi na wengine) kuomba msamaha kwa kosa ambalo alikuwa hajui lakini Kikwete alicheka na kusema hana tatizo naye!!!!! Huyu ndiye Rais (smiling president) anayesifiwa.
Anayekataa kuombwa msamaha ni SHETANI. Tuombeni jamani tumevamiwa.

Tumechoka na mambo ya uvumi na ya kufikirika yasiyo hata na msingi. Kwanza kama kupingana na JK ndiyo uadui basi Mwandosya, Mwakyembe, Mary Nagu, Magufuli, Kagasheki na wengine wengi wasingekuwa mawaziri au Njoolay asingekuwa RC, maana hao wote walipinga ugombea wake. Haya ni mambo yasiyo na msingi na hata hili la kuhamisha mkutano kutoka arusha kuja dar es salaam ni porojo zisizostahili hata kutupotezea muda. Kama ingekuwa hivyo basi hata vikao vya Council of Ministers ambavyo vimekuwa vikifanyika mpaka mwisho wa wiki iliyopita vingekuwa vimehamishwa. Suala la mkutano ufanyikie wapi ni suala la convenience na ingewezekana kufanyikia hata Tabora. Hivi Arusha kuna nini cha ajabu alichofanyiwa JK ,mpaka awalipizie visasi maana kama ni wabunge wa upinzani basi Mkoa wa Mwanza una wapinzani wengi kuliko Arusha. Hoja nyingine ni potofu mpaka inakera.
 
Ni dhahiri kuwa kuna siasa za visasi dhidi ya mji wa Arusha kunyang'anya fursa zake kiaina.Lakini kubwa kuliko yote ni hofu ya "mzee wa kaya" kuhusu mwamko wa kisiasa wa wakazi wa Arusha....... labda anadhani wanaweza kumuabisha mbele ya ugeni uliomjia. Lakini atambue hata akifanya kinyongo Arusha ndio makao makuu ya EAC.

Logically huu ndiyo ukweli kwamba anajua swala la umeya bado ni tata na kama president atajisikia embarased kama lolote litatokea kutoka kwa raia wake against yeye ukizingatia media za kimataifa zitakuwepo, so politically it could be difficult kwake kuja kufanya mkutano hapo AR hasa wakati huu ambapo CHADEMA wana utilize fully any political opportunity. Chakujiuliza atakimbia huo ukweli hadi lini?
 
Tumechoka na mambo ya uvumi na ya kufikirika yasiyo hata na msingi. Kwanza kama kupingana na JK ndiyo uadui basi Mwandosya, Mwakyembe, Mary Nagu, Magufuli, Kagasheki na wengine wengi wasingekuwa mawaziri au Njoolay asingekuwa RC, maana hao wote walipinga ugombea wake. Haya ni mambo yasiyo na msingi na hata hili la kuhamisha mkutano kutoka arusha kuja dar es salaam ni porojo zisizostahili hata kutupotezea muda. Kama ingekuwa hivyo basi hata vikao vya Council of Ministers ambavyo vimekuwa vikifanyika mpaka mwisho wa wiki iliyopita vingekuwa vimehamishwa. Suala la mkutano ufanyikie wapi ni suala la convenience na ingewezekana kufanyikia hata Tabora. Hivi Arusha kuna nini cha ajabu alichofanyiwa JK ,mpaka awalipizie visasi maana kama ni wabunge wa upinzani basi Mkoa wa Mwanza una wapinzani wengi kuliko Arusha. Hoja nyingine ni potofu mpaka inakera.

Mmh I doubt kama kweli unapenda kuelewa ukweli ama kwa personal reasons unataka kuleta ushabiki usioweza kuutetea kwa nguvu za hoja. Kumbuka ni rahisi kum contain adui akiwa karibu yako kuliko akiwa mafichoni. Unadhani angewaacha hawa watu angeweza kutawala kwa urahisi huku hawa wakiwa na wafuasi wao sehemu sehemu na bado wako katika system? Ukimwondoa Mwandosya na Mwakyembe Mbeya angeweza kuitawala? Je bila Magufuli na Kagasheki kanda ya ziwa ingekuwaje, angalia tu sasa mambo yalivyo mazito je hao pia wangekuwa ndiyo opposers ndani ya chama ingekuwaje? Impact ya Nagu plus Sumaye ukamweka na Slaa wawe against the government kwenye siasa za mkoa wa Arusha na Manyara unazifahamu na huku Kilimanjaro yote under influence ya Mbowe, Mtei na Ndesamburo mguu wake ungekanyaga huko kaskazini kweli? Kama alivyo sema PM aliangalia wale maadui wasio na impact kubwa lakini pia ambao watapunguza tention sehemu hizo kwa manufaa yake binafsi which is politically accepted any way. Siasa ni mchezo waajabu na wenye ku involve very dirty games kama wanaofanya siasa siyo watu ambao wanaongozwa na morals.
 
Watu mliopewa nafasi nyeti katika nchi lakini mnazitumia kwa maslahi binafsi.
Mchana mnaripoti ofisi nyeti za serikali usiku mnaripoti Chadema. Tunakumbuka thread yako ya matokeo ya uchaguzi.
Mbona huwa hamtumpi na nyeti za hao mafisadi wa huko kwenu wanaoliangamiza Taifa.
Hao akina Banduka, Mashishanga na Mahawa mbona husemi walichokuwa wakikifanya mikoani kwao wakati Kikwete akienda kuomba kura za kupitishwa na CCM kutokana na maelekezo ya Sumaye!
Watu wazima kama ninyi mnakuja kuvipotosha vitoto vya vyuoni na kumeza msemayo!
Huna uzalendo bali chuki tu na kutaka Kikwete aonekani hafai kwa lolote!
PM unajulikana kwa chuki zako. Any way msubiri huyo mkatoliki mwenzio Magufuli kama ulivyomtabiria kuwa Raisi 2015.
Shame on you na miftna yako!

Nungunungu ..umerudi ...??,mswahili na mwenzake wako wapi......ile SI UNIT ya kuchemcha..du i remember those old days here at JF..............WELL THESE IS CRAP .....unahalalisha visasi kwa kina mashishanga....?.........ni kawaida ya watu wajinga wakiiishiwa hoja huja na sababu za kuwa wanaonewa kwa ajili ya dini..hakuna kitu kama hicho ..fanya kazi!!
 
maneno hayooo kama nikweli basi ni hatari. Ila kwani ni J.K. anayepanga eneo au ni watendaji wake?
 
....JUU NIMEWEKA HOTUBA ALIYOSOMA ....MANENO ALIYOTAMKA JUU YA ARUSHA ...ALITAMKA KWENYE MSISITIZO ...JUU YA KILICHOTOKEA ARUSHA ...IWAPO TUTAPATA VIDEO CLIP YA HOTUBA YA RAIS PALE DODOMA TAREHE 5/2/2011 HAYA YATAJIELEZA WAZI....MWENDELEZO WA CHUKI HIZI PIA UMEJIDHIHIRISHA KWENYE TAMKO LA UMOJA WA VIJANA BAGAMOYO AMBAPO MTOTO WA RAIS ALIKUWAPO....

UKWELI NI KUWA KWENYE MKUTANO WA SEKRETARIET YA AFRIKA MASHARIKI ILIYOKETI ARUSHA KUANDAA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI JANA....KULIKUWA NA UBISHI MKALI KUTOKA KWA NCHI WANACHAMA AMBAZO ZILIKWERWA NA UAMUZI WA TANZANIA KUPELEKA MKUTANO DAR BILA KUWASIKILIZA .....WAO WANAONA KUTOKANA NA MISONGAMANO YA DAR NA UZOEFU WA MIKUTANO ILIYOPITA .....INAWAWIA VIGUMU WASHIRIKI KUFIKA SEHEMU KWA WAKATI....HASA WALE AMBAO HAWAPO KWENYE MISAFARA YA VIONGOZI WAO MOJA KWA MOJA....NA KWA UJUMLA PAMOJA NA UKUBWA WA DAR .....MIKUTANO MINGI IMEKUWA USUMBUFU KWAO NA KWA WANANCHI ....HASA PIA KUTOKANA NA MIUNDOMBINU KUTOKUWA RAFIKI...

KAMA DAR INATAKA KUVUTIA MIKUTANO BILA KUWEKA USUMBUFU KWA WASHIRIKI NI BORA WAFIKIRIE KUWA NA VILLAGE AMBAYO ITAJUMUISHA PIA SEHEMU ZA MALAZI ...KAMA ILIVYO KAMPALA,[COMMONWEALTH VILLAGE],NA NAIROBI[GILGIL]..etc.......lakini kama tutaendelea kulazimisha mambo tutapoteza nafasi ya ARUSHA AMBAPO NI ...MAKAO MAKUU YA AFRIKA MASHARIKI,CHUO CHA UONGOZI AFRIKA ,CHUO KIKUU CHA TEKNELOJIA AFRIKA ,MANDELA,SHIRIKISHO LA POSTA AFRIKA,MAKAKAMA YA RWANDA[na hata tuki lobby vema mahakama ya HAGUE wanataka kuweka tawi pale],mahakama kuu ya afrika,mahakama ya afrika mashariki...etc....are we ready to lose everything just kwa ajili ya visasi?????????......narudia tena kama ingekuwa visasi basi Kibaki angeutenga mji wa nairobi....na kulikuWA na hati hati ya makao makuu ya umoja wa mataifa na habitat ihame nairobi....ingeweza kuletwa Arusha au kuhama kabisa ukanda huu....
Sasa kumekucha,asante mkuu sina comment.
 
Katika kile ulifanyalo ni lazima ujieandae na madhara yake,

Arusha ilipokubali kugeuzwa kuwa kitovu cha mapambano ya kisiasa ni lazima wawe tayari kufaidi matamu na machungu yake. Kama kiongozi wa nchi Rais ana wajibu wa kuhakikisha hawaexpose wakuu wa nchi zingine na rabsha za kisiasa ambazo ni vigumu kuzitabiri kutokana na hali ya kisiasa Arusha lakini pia ukichukulia historia isiyo nzuri ya jiji hilo kiusalama huko nyuma.

Lakini pia ni wazi gharama zingekuwa kubwa zaidi kufanya kikao cha wakuu wa nchi Arusha halafu kuwakimbiza katika jiji kitovu cha biashara Dar ili kushiriki kikamilifu katika mkutano wa uwekezaji ambao umetayarishwa na kituo cha uwekezaji chini ya Mwana - Arusha Ole Naiko kwa kushirikiana na Commonwealth

All in all, katika kila ukulima, unavuna ulichopanda. Na ni wajibu wa mpiganaji wa kweli kuembrace ukweli huo badala ya ku-agonise...
Iligeuzwa na nani?na lini na kupambana na nani na mapambano yanaendeleaje?Kwa upeo wako unataka kutushawishi kuwa wageni waliohudhuria mkutano wangeweza kushambuliwa na wanasiasa walioko kwenye mapambano ya kisiasa?ebu tazama kinachotokea ng'ambo ya mto ili kupanua fikira,uondokane na fikira butu kama rangi nyeusi usiite nyeupe,maamuzi yaliyofanywa na jk ni mabaya.LKN NIVIBAYA ZAIDI KW KIJANA KM WW KUYAUNGA MKONO HUKU UKIJUA WAZI KUWA NI YA HOVYO.
 
nashangaa wanaokuja na hoja za protest..watu wanaandamana kwenye mikutano ya G8 Itakuwa huku..tena maandamano ya amani yanaonesha level ya civilialization ipo juu.
 
Mwanakijiji na wewe unaingia kwenye mtego huu??? Kwamba ni kisasi?? This is too low. Inamaana Arusha ndio sehem pekee nchi hii panapostahili mikutano yote? Na mikutano haijawahi kufanyikia DSM? Hizi ni hoja za kitoto

Kwa JK anything is possible!!!
 
Watu mliopewa nafasi nyeti katika nchi lakini mnazitumia kwa maslahi binafsi.
Mchana mnaripoti ofisi nyeti za serikali usiku mnaripoti Chadema. Tunakumbuka thread yako ya matokeo ya uchaguzi.
Mbona huwa hamtumpi na nyeti za hao mafisadi wa huko kwenu wanaoliangamiza Taifa.
Hao akina Banduka, Mashishanga na Mahawa mbona husemi walichokuwa wakikifanya mikoani kwao wakati Kikwete akienda kuomba kura za kupitishwa na CCM kutokana na maelekezo ya Sumaye!
Watu wazima kama ninyi mnakuja kuvipotosha vitoto vya vyuoni na kumeza msemayo!
Huna uzalendo bali chuki tu na kutaka Kikwete aonekani hafai kwa lolote!
PM unajulikana kwa chuki zako. Any way msubiri huyo mkatoliki mwenzio Magufuli kama ulivyomtabiria kuwa Raisi 2015.
Shame on you na miftna yako!

du hili nalo ni limsumari nini limepigiliwa hapa kwenye hread ya PM
 
Kweli KIKWETE ni mtu sumu sana kama alimfanyia Mkuu wake wa mkoa hivyo ,ana visasi vibaya sana,hivi huyu Banduka yupo hai au alikufa hajawahi kusikika tena wakati alikuwa mtu maarufu

Kikwete ni mtu hatari saana akijua unampinga. Nakumbuka alivyokua anapigania uraisi na waziri wa maji (Mwa...) alikwenda Kilimanjaro wakati huo Hilda Ngoye alikua mkuu wa mkoa. Hilda alikua ana msapoti waziri wa maji hivyo hakumpa mapokezi makubwa sana kama alivyompa Mwa.. Kikwete alivyoshinda akamuondoa Hilda Ngoye akamuhamishia Mbeya kwa Mwa... Watu wa Kilimanjaro waliumia saana na toka siku hiyo Kikwete na CCM kilimanjaro haziivi sana. Kikwete amechangia sana kugawanyika kwa wana CCM kwaajili ya fitina na visasi.
 
Logic pekee ni kusema mkutano huo umefanyikia Dar kwa sababu ya Investment Forum na viongozi hao walitakiwa kuhudhuria. Vinginevyo suala la usalama halipo. Ingekuwa hivyo basi viongozi wa EaC na IcTR waliopo wangeondolewa!
 
Wale Makamishna walistaafishwa kwa manufaa ya Mkapa ili mteule wake mpya wakati huo, Omar Mahita, aingie kazini. Imran Kombe alistaafishwa, akafananishwa na jambazi, akapigwa risasi, akafa.

Kwa maana hiyo jk anafanya sahihi kwa sababu mtangulizi wake alifanya hivyo?
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom