#COVID19 Visa vya Corona nchini Uganda vyaongezeka hadi 889

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Wizara ya Afya imethibitisha visa vipya 19 vya CoronaVirus baada ya kupima sampuli 2,170 na maambukizi ya nchi hiyo yamefikia 889.

Katika visa vilivyotangazwa leo, 11 walisafiri kutoka Afghanistan na walikuwa karantini wakati wanafanyiwa vipimo. 7 ni watu waliokuwa karibu na wagonjwa wa COVID19.

Aidha, madereva wa malori 25 raia wa Kenya-15, Tanzania-7, Misri-2 na Burundi-1 wamerudishwa nchini mwao baada ya kukutwa na Corona.

Wagonjwa 819 wamepona na nchi hiyo haijarekodi kifo chochote hadi sasa.

====

1593506402339.png
 
Back
Top Bottom