Visa na Vibweka vya Sumbawanga.

Visa na Vibweka vya Sumbawanga.

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
78,121
Reaction score
165,984
Hizi ni stori za Sumbawanga, tumekuwa tukizisikia sana lakini hatujazithibitisha.
Miongoni mwa stori hzi ni kwamba kuna mkuu mmoja wa mkoa aliteuliwa enzi za Nyerere. Alipoenda kujitambulisha kwa wazee kwenye mkutano ulio fanyika kwenye ukumbi wa almashauri ya mji, akashangaa wazee wana tundika makoti yao hewani na hayaanguki.
Jamaa aka resign ndani ya masaa 24
 
Kuna mizimu ya Katabi na Katavi watu wamekutana nayo sana kwenye mbuga ya Katavi ati Sumbawanga na Mpanda. Ukikutana na mizimu hii unaweza kuwehuka au kufa kabisa.
 
jamaa mwenyewe aliyeteuliwa na Nyerere ni huyu
261822_10150211287861022_636196021_7577714_3886452_n.jpg
 
Hizi story nilikuwa nazisikia sana kama;

1.Jamaa aliamua kuwekeza sumbawanga mjini, akaamua kujenga, akanunua tofali,mbali na site, alikodi vijana wambebee matofali ya kuchoma kupeleka site, kesho kuamka anajikuta kaamkia site, hoi mchafu kishenzi kumbe yeye mwenyewe kabeba tofali.

2.Nyingine jamaa alikataa mimba ya binti ikawa kizaa zaa.

Nadhani story nyingi zilikuwa ni za kutunga, maana toka kuwe na mawasiliano ya uhakika hatusikii tena hizi legend. Nyingi zilikuwa za zamani na zilikuzwa zilipokuwa zinahadithiwa, kwani nyingi zinafanana ila zinatofaitiana kwa masimulizi
 
WENGI wetu tukisikia jina Sumbawanga ni
wazi kuwa fikra zinakwenda moja kwa
moja kuwa ni uchawi, ushirikina na pengine
kifo. Ukweli ni kwamba ni jina lililotoholewa
kwenye neno Sumbu wanga, likiwa na
maana ya tupa uchawi , na lilianzishwa na
mtawala mmoja wa zamani wa eneo hilo
aliyeitwa Mwene Ngalu.
Sumbawanga ni makao makuu ya mkoani
Rukwa, uliopo Nyanda za Juu Kusini
Magharibi mwa Tanzania. Mkoa huu
unapakana na nchi za Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Zambia,
Burundi na mikoa ya Tabora na Mbeya na
una jumla ya watu milioni 1.5, kwa mujibu
wa sensa ya mwaka 2002. Ulianzishwa
rasmi mwaka 1972.
Mkoa huo una makabila mbalimbali ila kabila
kubwa na la asili ni Wafipa ambao ndiyo asili
ya jina Sumbawanga, mji ulioanzishwa
mwaka 1803, chini ya chifu wa kwanza wa
Ufipa aliyeitwa Kapufi ambaye alitawala
miaka ya 1885. Chifu Kapufi wa Kwanza
alianza milki yake ndani ya Ufipa yote na
makao yake makuu yalikuwa Kijiji cha
Kisumba nje kidogo ya mji wa Sumbawanga.
Mke wake aliitwa Mwene Wakulosi ambaye
walijaliwa kupata watoto watatu, wa
kwanza wa kiume na wawili waliofuata wa
kike ambao ni Mwene Kiatu wa pili aliitwa
‘Mwene Ngalu Chisichaafipa’ (jina la utawala)
na wa tatu aliitwa Mwene Mwati.
Baada ya kifo cha Chifu Kapufi wa Kwanza,
milki ilitawazwa kwa mwanae wa kwanza,
Mwene Kiatu ambaye alihamia kijiji cha
Lwiche ambako kwa mila na desturi za
kiutawala, ukitawazwa kuwa chifu ni lazima
uhame na kwenda kuanzisha kijiji chako
kama alivyofanya Mwene Kiatu.
Katika kipindi chake cha utawala wa eneo la
ufipa, chifu Mwene Kiatu hakujaliwa kupata
watoto na alipokufa, milki ilichukuliwa na
dada yake, Mwene Ngalu ambaye ndiye
mwanzilishi wa Sumbawanga.
Chifu Mwene Ngalu alikuwa mtu mwenye
upendo na hakupenda uchafu wa aina
yoyote ukiwamo uchawi, hivyo kabla ya
kuingia kijiji cha Sumbawanga
alichokianzisha, aliwataka wananchi
waliomfuata watupe uchafu wote kwenye
mto Lwiche pamoja na uchawi kisha
waingie wakiwa safi.
Kutokana na imani hiyo watu walitupa
uchawi wote na taka nyingine kisha
wakaingia kijiji cha Sumbawanga wakiwa
wasafi. Aliyekiuka amri hiyo na kuvuka mto
Lwiche kutaka kuingia kijiji kipya cha
Sumbawanga alikufa katika mto huo.
Hapo ndipo ikawa asili ya Sumbawanga na
kijiji kikawa na watu walio wasafi na
hakukuwa na matatizo na utawala wa
Mwene Ngalu. Alipendwa na kila ilipotokea
ishara ya matatizo ndani ya ufipa ilikuwa
rahisi kutatuliwa kwa kuwa Chifu Mwene
Ngalu aliomba na majibu yalipatikana
haraka, hasa kwa imani ya usafi waliokuwa
nao.
Hata hivyo Chifu Mwene Ngalu alijaliwa
kupata watoto saba ambao wote aliwazalia
katika nyumba yake ya utawala iliyojengwa
kwa kipindi cha miaka miwili katika mwaka
1918 hadi 1920 chini ya usimamizi wa
Mabruda wa dhehebu la Roma yaani
wakatoliki ambao walikuwa Wajerumani.
Nyumba hiyo hivi sasa imebomoka na
limebaki gofu ambalo kwa nje kuna sehemu
ya makaburi yanayotumika kuzika kizazi cha
utawala huo, na jambo la ajabu kwenye
gofu hilo wapo nyuki waliojenga kwenye
pango na wapo kwa muda mrefu tangu
kipindi cha uhai wa baadhi ya watawala wa
kizazi hicho.
Watoto wa Mwene Ngalu ni Maria wa Ngao,
Joseph Kapufi wa Ngao, Thadeo wa Ngao,
Teresia wa Ngao, Jacob wa Ngao, Victoria
wa Ngao na Antony wa Ngao, ambao baada
ya kifo cha mama yao, mtoto wa kwanza
Joseph wa Ngao alitawazwa kuwa Chifu wa
kizazi hicho na kupewa jina la Joseph wa
Ngao-Kapufi wa Pili.
Chifu huyo aliyejaliwa watoto wanne, ambao
ni Olanda Joseph, Adolf Joseph, Veneranda
Joseph na Yovita Joseph na alipofariki dunia
nduguye ambaye ni mdogo wake wa
mwisho, Antony wa Ngao alitawazwa
mwaka 1989, kuwa Chifu wa Ufipa na
kupewa jina la Kapufi wa Tatu.
Kapufi huyo wa tatu, Antony wa Ngao,
alitawala ufipa tangu mwaka 1989 hadi
Desemba 6 mwaka jana alipofariki dunia na
kuzikwa kwenye eneo la makaburi ya kizazi
cha utawala huo, karibu na jengo la Mwene
Ngalu ambalo hivi sasa limebaki gufo tu.
Katika kipindi cha utawala wake, Chifu
Kapufi wa Tatu, alijaliwa kupata watoto
watatu ambako mkewe wa kwanza alijaliwa
kupata mtoto mmoja wa kike aliyeitwa Ntalu
na mke mdogo alijaliwa kupata watoto
wawili wa kiume ambao ni Oscar na
Apolinary. Hata hivyo baada ya kifo cha
Kapufi wa Tatu, hivi sasa ukoo huo wa
kichifu uko kwenye mchakato wa kutafiti
mrithi wa kiti hicho.
Msemaji wa familia ya akina Kapufi Adolf
Joseph (61), ambaye ni mtoto wa Chifu
Joseph wa Ngao wa Pili, anasema jinsi ya
kumpata mrithi huyo ni kwa njia ya
kuwashirikisha wazee wa mji huo (wa
zamani) walio hai hivi sasa pamoja na wale
wa vijiji vya karibu kisha kuteua majina
kadhaa na kuyachambua kupata
anayestahili.
Anasema jina la mrithi likipatikana sherehe
za kumsimika kuwa Chifu wa kabila hilo
huanza kufanyiwa maandalizi, na kwa
kawaida hufanywa nje ya mji kwa
kutengeneza sehemu maalumu ya
kumpitishia ambayo huiita mzingo. Pia
huvuka mto Lwiche kwa imani kuwa ni
moja ya hatua za kudhihirisha kiwango cha
usafi wake kabla ya chifu mtarajiwa
kutawazwa.
Baada ya sehemu hiyo kukamilika
kutengenezwa chifu mtarajiwa hupitishwa
kwa nyuma kuingia kwenye mzingo huo
huku akipuliza filimbi tatu, ya kwanza
ikikataa kulia hupewa ya pili nayo ikigoma
hupewa ya tatu ambayo nayo ikigoma ni
dalili kuwa hafai kuwa chifu, hivyo
huenguliwa na kutafutwa mwingine.
Adolf anasema ikiwa filimbi moja au mbili
zikilia na moja kugoma watampa utawala
wa muda huku wakijiandaa kumtafuta chifu
mwingine, kwa imani kuwa filimbi zote
lazima zilie kwa sababu ni ishara ya sifa
njema za utawala za kiongozi anazopaswa
kuwa nazo ndipo apewe mamlaka.
Wakati mchakato huo ukiendelea, wa
kumpata mrithi wa kiti hicho, mavazi ya
Chifu Kapufi wa Tatu, Antony wa Ngao
amepewa Vicent Kafumu ambaye ni mjukuu
wa Chifu Mwene Ngalu kwa mzaliwa wake
wa kwanza aliyeitwa Maria wa Ngao.
Pamoja na hayo yote pia enzi za utawala wa
viongozi hao walitumia silaha mbalimbali
ambazo hadi leo baadhi yake zimehifadhiwa
ili mtawala ajaye akabidhiwe kwa ajili ya
kudumisha mila. Zana hizo ni upinde
(ulapwa), mishale (ncheto), fimbo (wasi),
mkuki (ilawa) na chombo cha kubebea
mishale (untontowaancheto). Silaha
nyingine ni shanga (inkasi) zinazovaliwa
mikononi na shingoni kwa chifu, kiti cha
miguu mitatu (kisumbi) na vazi la kujifunga
kiunoni na mabegani (seketa) ambayo
husukwa kwa pamba.
Anasema mabadiliko ya dunia na teknolijia
na mapinduzi ya kilimo kwa kiasi kikubwa
zilibadilisha mtazamo na fikra za wakazi wa
Sumbawanga ambako muingiliano wa watu
ulipoanza imani ya uchawi na ushirikina
zilipungua na watu wakaingia katika
shughuli za uzalishaji mali ingawa baadhi
yao wanaendelea na ushirikina kama zilivyo
sehemu nyingine nchini.
Mabadiliko hayo pia yalipunguza nguvu ya
kuabudu mizimu iliyokuwapo hapo awali
kwa kuwa misitu mingi ilifyekwa kwa ajili ya
shughuli za kilimo na ufugaji hivyo, imani ya
kuwapo mizimu iliondoka kwa asilimia
kubwa na watu wakabakia kuabudu katika
nyumba za ibada kufuatana na imani ya dini
zao, anasema Adolf.
Hata hivyo bado kuna sehemu au vijiji
vyenye kuendelea kuamini mizimu na
ushirikina kama vile kijiji cha Chipu kilicho
kilomita kama 30 kutoka Sumbawanga mjini
na vijiji vya Milanzi na Kalambo ambavyo
bado imani ya uchawi na vitendo vya
kishirikina vinaendelea kwa baadhi ya
wakazi wake.
Kwa kijiji cha Milanzi baadhi ya wakazi wake
hutumia mapango yaliyo kwenye mlima
uitwao Itwelele kwa kufanya matambiko na
mambo mengine ya kishirikina kwa imani
kuwa mizimu iliyopo huko huwasaidia
kutekeleza mahitaji yao na kumdhuru mtu
au watu waliotenda makosa na kuyakana.
Adolf anasema hilo siyo tatizo kubwa kwa
sababu hakuna anayemdhuru mgeni
anayeingia mkoani hapo kwa kufanya
shughuli zake kama vile biashara au kilimo.
Ila kwa wale ambao hawajafika
Sumbawanga hudhani kuwa huo ni uchawi
na ushirikina tu, dhana ambayo si ya kweli
kwa kuwa maendeleo yanayopatikana
katika karibu makabila yote nchini hivi sasa
yapo pia Sumbawanga
 
Makala ndefu lakini nzuri, nimeipenda na asante kwa kutujulisha historia ya Sumbawanga na watawala wake wa jadi.
 
Kama uliamini wachawi na wazee vikongwe,
Simbeye atayabadili mawazo yako. Anasema
uchawi aliurithi kutoka kwa babu yake, na
akiwa na miaka kumi na nne alikuwa
mchawi maarufu mjini Sumbawanga
alikozaliwa mwaka 1961. Msikie: " Hata
masomo yangu yalikatizwa na safari za kila
mara kwenda kuzimu na kurudi duniani"
Pengine hiyo ni nzito kwako kama
ilivyokuwa kwa mwandishi wa habari hizi
alipotembelewa na Simbeye katika Ofisi za
GTV Nairobi Kenya. Tulipotaka kujua
kwamba Kuzimu alikuwa akienda kwa
usafiri upi? Yeye alijibu: "Mimi unayeniona
hapa, nilikuwa na uwezo wa kujibadili kuwa
chochote. Ningeweza kujibadili niwe Nyoka
ama mbuzi ili mradi niwe mwepesi kwenda
kuzimu bila Mke wangu Mrs. Medhodia
Muzare kujua." "Wao wangeona mbuzi ya
jirani shambani, na wakijaribu kuifukuza
inapotea bila wao kujua imeelekea wapi."
Kwangu safari ya Kuzimu ilikuwa imeanza."
Maneno ya kuzimu hayakunivutia sana kama
pale aliposema kwamba wateja wake
walikuwa wengi ni Wahubiri. "Kazi yangu ya
uchawi sikuwa naifanya kinjaa njaa."
"Wateja wangu walianzia mawaziri
wabunge na hata wahubiri walitaka nguvu
kutoka kuzimu ziwasaidie kujaza makanisa
yao." Hata mimi nilishawishika kama wewe
kuuliza anitajie wahubiri hao. Alisema: "Japo
sasa nimeokoka na kujiunga na mhubiri wa
kike Joyce Wairimu Maina, haitakuwa busara
kwangu kuwataja wateja wangu wa
zamani, lakini wengi walikuwa wakija
niwasaidie uchawi wa kuangusha watu
wanapoombewa ionekane kwamba ni
nguvu za Mungu."Kwa Simbeye anaedai
Kaokoka, Tena chini ya Mchungaji Joyce
Wairimu Maina wa Kericho ambaye kanisa
lake limefurika watu wanaotaka kumuona
Mchawi kutoka Tanzania, Halafu uangalie
ibada kanisani hapo inapoendeshwa,
Mambo yote aliyokuwa akiyafanya wakati
akiwa mganga wa kienyeji, sasa
ameyageuzia kwa Yesu, utashawishika
kusema bado Uganga wa kienyeji
umehamishiwa kanisani. Lakini mwenyewe
anadai:"Hii tunayoifanya kanisani kwa Mama
Joyce Maina ni tofauti na ile inayofanywa na
wachungaji niliokuwa nikiwauzia uchawi."
Tena wahubiri waliokuwa wakija kununua
uchawi kwangu ni wale walioajiriwa na
Wanawake Matajiri walioacha mabwana zao
na kuanza mradi wa kuhubiri. Hao ndio
hununuliwa dawa za kusababisha miujiza
na wanaifanya hiyo kama kazi nyingine."
"Isitoshe Wamama hao matajiri hununua
dawa za kuwafanya wahubiri vijana
wakubali kuwaoa." "Kuna vijana wengi
walioolewa na wamama hao na sasa
huduma zao zimetekwa nyara na wamama
hao na huwatumikisha kama watumwa.'
"Asubuhi mchana na jioni lazima wahubiri
na kufanya miujiza FEKI ili waumini watoe
pesa ambazo huchukuliwa na wamama hao.
' Wahubiri hulipwa kidogo, na kununuliwa
mavazi ya kuvutia washirika.
 
Kuna mizimu ya Katabi na Katavi watu wamekutana nayo sana kwenye mbuga ya Katavi ati Sumbawanga na Mpanda. Ukikutana na mizimu hii unaweza kuwehuka au kufa kabisa.
Mizimu hiyo ni Katabi na mkewe Wamwelu, inasemekana mpaka sasa huwa wanaonekana katika mbuga ya Katavi.
 
Kama uliamini wachawi na wazee vikongwe,
Simbeye atayabadili mawazo yako. Anasema
uchawi aliurithi kutoka kwa babu yake, na
akiwa na miaka kumi na nne alikuwa
mchawi maarufu mjini Sumbawanga
alikozaliwa mwaka 1961. Msikie: " Hata
masomo yangu yalikatizwa na safari za kila
mara kwenda kuzimu na kurudi duniani"
Pengine hiyo ni nzito kwako kama
ilivyokuwa kwa mwandishi wa habari hizi
alipotembelewa na Simbeye katika Ofisi za
GTV Nairobi Kenya. Tulipotaka kujua
kwamba Kuzimu alikuwa akienda kwa
usafiri upi? Yeye alijibu: "Mimi unayeniona
hapa, nilikuwa na uwezo wa kujibadili kuwa
chochote. Ningeweza kujibadili niwe Nyoka
ama mbuzi ili mradi niwe mwepesi kwenda
kuzimu bila Mke wangu Mrs. Medhodia
Muzare kujua." "Wao wangeona mbuzi ya
jirani shambani, na wakijaribu kuifukuza
inapotea bila wao kujua imeelekea wapi."
Kwangu safari ya Kuzimu ilikuwa imeanza."
Maneno ya kuzimu hayakunivutia sana kama
pale aliposema kwamba wateja wake
walikuwa wengi ni Wahubiri. "Kazi yangu ya
uchawi sikuwa naifanya kinjaa njaa."
"Wateja wangu walianzia mawaziri
wabunge na hata wahubiri walitaka nguvu
kutoka kuzimu ziwasaidie kujaza makanisa
yao." Hata mimi nilishawishika kama wewe
kuuliza anitajie wahubiri hao. Alisema: "Japo
sasa nimeokoka na kujiunga na mhubiri wa
kike Joyce Wairimu Maina, haitakuwa busara
kwangu kuwataja wateja wangu wa
zamani, lakini wengi walikuwa wakija
niwasaidie uchawi wa kuangusha watu
wanapoombewa ionekane kwamba ni
nguvu za Mungu."Kwa Simbeye anaedai
Kaokoka, Tena chini ya Mchungaji Joyce
Wairimu Maina wa Kericho ambaye kanisa
lake limefurika watu wanaotaka kumuona
Mchawi kutoka Tanzania, Halafu uangalie
ibada kanisani hapo inapoendeshwa,
Mambo yote aliyokuwa akiyafanya wakati
akiwa mganga wa kienyeji, sasa
ameyageuzia kwa Yesu, utashawishika
kusema bado Uganga wa kienyeji
umehamishiwa kanisani. Lakini mwenyewe
anadai:"Hii tunayoifanya kanisani kwa Mama
Joyce Maina ni tofauti na ile inayofanywa na
wachungaji niliokuwa nikiwauzia uchawi."
Tena wahubiri waliokuwa wakija kununua
uchawi kwangu ni wale walioajiriwa na
Wanawake Matajiri walioacha mabwana zao
na kuanza mradi wa kuhubiri. Hao ndio
hununuliwa dawa za kusababisha miujiza
na wanaifanya hiyo kama kazi nyingine."
"Isitoshe Wamama hao matajiri hununua
dawa za kuwafanya wahubiri vijana
wakubali kuwaoa." "Kuna vijana wengi
walioolewa na wamama hao na sasa
huduma zao zimetekwa nyara na wamama
hao na huwatumikisha kama watumwa.'
"Asubuhi mchana na jioni lazima wahubiri
na kufanya miujiza FEKI ili waumini watoe
pesa ambazo huchukuliwa na wamama hao.
' Wahubiri hulipwa kidogo, na kununuliwa
mavazi ya kuvutia washirika.
source???
 
Hizi ni stori za Sumbawanga, tumekuwa tukizisikia sana lakini hatujazithibitisha.Miongoni mwa stori hzi ni kwamba kuna mkuu mmoja wa mkoa aliteuliwa enzi za Nyerere. Alipoenda kujitambulisha kwa wazee kwenye mkutano ulio fanyika kwenye ukumbi wa almashauri ya mji, akashangaa wazee wana tundika makoti yao hewani na hayaanguki.Jamaa aka resign ndani ya masaa 24
Alienda mkuu mwingine,yeye kidogo alikuwa njema,akiwa mkutanoni walimfanyia mchezo huo huo wa kutundika makoti hewani naye akajibu mapigo kwa kutundika lake pia hewani.Baada ya kikao,wale wazee walichukua makoti yao lakini yule mkuu alipotaka kuchukua koti lake akagundua limeliwa na mchwa!
 
Alienda mkuu mwingine,yeye kidogo alikuwa njema,akiwa mkutanoni walimfanyia mchezo huo huo wa kutundika makoti hewani naye akajibu mapigo kwa kutundika lake pia hewani.Baada ya kikao,wale wazee walichukua makoti yao lakini yule mkuu alipotaka kuchukua koti lake akagundua limeliwa na mchwa!


nakumbuka miaka ya 2005 mwishoni iliwahi kutangazwa kuwa HUKO SUMBAWANGA mwewe alionekana angani akiwa amenyakua ng'ombe KAMA ANAVYOWANYAKUA VIFARANGA! SIKUFUATIKIA ZAIDI KUTOKANA NA UKWELI KUWA NILIKUWA SHULE NJIA ZA HABARI ILIKUWA ADIMU KIDOGO NA MUDA ULIKABA! KAMA KUNA MTU ALISHAWAHI KULISIKIA HILO ATUJUZE ZAIDI
 
Ana shida gani?? kikao kikiisha anapata posho zake!!!!!Pia siku hii alikuwa akimuwakilisha waziri mkuu kwa maana waziri mkuu hakuwepo siku hiyo ya tarehe 21 bungeni!!Mwamsheni mumuulize swali la pupa kwa pupa (papo kwa papo) ujionee majibu yakeMf. Mbona unalala bungeni? Jibu la kwanza mimi sijalala, nasikuliza wachangiaji kwa umakini sana, kwanza nani kukwambia unipige picha? mara kofi, ngumi, mara umeliwa sikio!!!!!!!!!This is Mr Tyson bwana!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom